Featured Post

TUNATOA HUDUMA YA KUPIMA UWEPO WA MAJI ARDHINI NA KUCHIMBA VISIMA!



MABADILIKO ya Tabianchi yameleta athari kubwa katika maendeleo duniani ambapo kwa sasa ni vigumu kupatikana kwa vipindi vya mvua za uhakika kama ilivyokuwa miaka 50 iliyopita.
Maeneo mengi Tanzania yana shida ya upatikanaji wamvua za uhakika na hivyo kuongeza uhaba wa maji hata kwa matumizi ya kawaida.
Kilimo cha kutegemea mvua sasa kimepitwa na wakati kwa sababu ya mabadiliko ya tabianchi, hivyo ili kujiletea maendeleo ni vyema kugeukia KILIMO ENDELEVU CHA UMWAGILIAJI.

Tunapoelekea kwenye TANZANIA YA VIWANDA tutambue kwamba kilimo ndicho kinachozalisha malighafi, kwahiyo basi ni vyema tugeukia kilimo cha umwagiliaji ambacho sasa tunaweza kukifanya kwa uhakika kwa kuchimba visima virefu salama.
Taasisi za fedha zinazosapoti kilimo nazo hazitoi mikopo kwa wakulima wanaotegemea anga linune mvua inyeshe, bali wanatazama watu wanaofanya kilimo endelevu cha umwagiliaji ambacho ni cha uhakika zaidi. Kwahiyo kuchimba kisima ndiyo suluhisho pekee linaloweza kutukomboa wakulima – iwe mmoja mmoja au kwa vikundi vya ushirika.

KUPIMA MAJI
Tunapenda kuwaarifu wana-maendeleo wote kwamba tunatoa huduma za kupima uwepo wa maji ardhini kabla ya kuchimba kisima.
Kumbuka kwamba, hata ukienda hospitalini, muuguzi lazima atautafuta ulipo mshipa ili aweze kukudunga sindano. Kamwe hawezi kuchoma kila sehemu ya mwili kwa sababu kufanya hivyo siyo tu anamuumiza mgonjwa, lakini pia hawezi kutoa tiba sahihi kwa sababu dawa inapaswa kuingia katika mfumo wa damu kupitia kwenye mshipa wa damu wa Vena.
Ndiyo sababu utakuta watoto wadogo wakati mwingine wauguzi hulazimika hata kuwachoma sindano kichwani baada ya kuuona mshipa wa damu kwa sababu mtu anapoumwa mara nyingi mishipa ‘hupotea’ au huwa haionekani kwa urahisi.
Vivyo hivyo, kuchimba kila mahali ardhi kwa nia ya kutafuta maji ni kuharibu ardhi pamoja na kuingia gharama zinazoepukika kwa sababu mchimbaji wa kisima ukishamwambia kwamba achimbe mahali na mmekubaliana gharama kwa kila meta moja, yeye atachimba na hata kama maji hayatapatikana lazima ulipe gharama tu!
Sasa kwa kuepuka gharama hizi, sisi tunapima uwepo maji katika ardhi unapotaka kuchimba kisima tukitumia vifaa vya kisasa kabia.
Vifaa vyetu vina uwezo mkubwa wa kupima uwepo wa maji katika eneo la urefu wa meta 2000, yaani kilometa 2 (Long range water location measurement) na kila cha meta 1200 yaani kilometa 1.2 (Geophysical) ambacho ni kirefu sana.
Vifaa vyetu vina uwezo wa kutambua AINA YA MAJI kama MAJI BARIDI (Fresh Water) au MAJI CHUMVI (Natural Water), wingi wake, mahali yanakopatikana (kina) pamoja na wiani wake (density). Vifaa vyetu vinapima kabisa hali ya chumvi (WATER SALINITY).
Tukishapima pia tunakupatia ushauri wa PUMP bora pamoja na huduma nyingine kabla ya kuanza kuchimba.

Hasara za kutopima
Hasara za kutokupima kabla ya kuchimba ni kwamba, mtu anaweza kuchimba na kupata maji, lakini kwa kuwa hakupima na kujua kiasi cha maji, basi visima vingi utakuta vinakauka haraka wakati tayari watu wamekwishaingia gharama. Matukio haya ni mengi sana.
Inawezekana kabisa kwa sababu amechimba bila kupima, maji yaliyopatikana ni katika mikondo midogo iliyo ardhini (small underground streams) ambayo inaweza kukauka. Lakini kama wangalipima na kujua kwa uhakika wangeweza kujua maji yanapatikana katika kina gani.
Baadhi ya watu pia hukwepa gharama kuchimba visima virefu na mara wanapochimba na kupata maji katika mikondo ya juu, basi huona hawana haja ya kuendelea zaidi chini.

Kumbuka:
Upatikanajji wa maji ardhini unategemea na mikondo iliyopo na ardhi yenyewe. Mfano, anayechimba bondeni kwenye mkondo wa maji anaweza akachimba mita chache kulinganisha na anayechimba katika nchi kavu mbali na bonde au mto. Hata maeneo ya mwambao wa Pwani nayo pia yanatofautiana – mmoja anaweza kuchimba na kupata maji katika kina cha meta 60 lakini mwingine akapata maji katika kina cha meta 100. Jambo mhimu hapa ni kupima. Tukikwambia kwamba maji yatapatikana baada ya kupima ujue ni uhakika wa asilimia 90% utapata maji ya uhakika kwa sababu vipimo vyetu ni vya kisasa na vya uhakika.

Muhimu:
Siyo kila mahali kunaweza kupatikana maji, hivyo tunapogundua hivyo tunatoa ushauri wa kutochimba na kama kuna eneo jingine mbadala unaweza kulipima.
Kama utahitaji tukufanyie utafiti peke yake (geo-physical survey) halafu utatafuta mchimbaji (Driller) wewe mwenyewe hakuna shida pia. Lakini tutakupa ushauri wa uhakika utakaokusaidia ili kisima chako kiwe cha kudumu.

GHARAMA
Gharama zetu ni nafuu sana na tunaweza kwenda mahali popote mkituhitaji. Aliye tayari kwa kupimiwa MAWASILIANO YETU NI 0656-331974, 0787-426161, au +255 716 775334. Barua-pepe: maendeleovijijini@gmail.com.

GHARAMA ZA UCHIMBAJI
Kwa ujumla, gharama za uchimbaji wa kisima zinategemea utafiti wa vipimo ulivyofanya.
Kwahiyo gharama za kuchimba kisima zinategemea mambo kadha wa kadha:
  1. Kina cha maji
Kama nilivyosema awali, mahali pengine maji yanapatikana katika kina kifupi tu cha meta 60, lakini sehemu nyingine unaweza kwenda hata meta 120 kulingana na vipimo vinavyoonyesha yanakopatikana maji pamoja na wingi wake – water quantinty.

  1. Aina ya udongo
Hili ni jambo la msingi sana. Mahali unakotaka kuchimba kisima ni lazima ijulikane ni udongo wa aina gani. Gharama za uchimbaji zinatofautiana kutokana na aina ya udongo. Kuchimba kwenye udongo wa mfinyanzi (CLAY SOIL) na udongo mchanganyiko (MIXED SOIL) ni kazi kubwa kuliko kuchimba kwenye udongo wenye miamba (ROCKY SOIL) au udongo wa kichanga/tifutifu (SANDY/LOAM SOIL).

Zipo mashine mbalimbali zinazotumika katika kuchimba visima na katika maeneo yenye utata mashine yenye nyundo (HAMMER RIG) ndiyo inayofaa, hasa kwenye miamba.

MAWASILIANO YETU NI 0656-331974, 0787-426161, au +255 716- 775334. Barua-pepe: maendeleovijijini@gmail.com.


Comments