Featured Post

MAAJABU YA ALOE VERA (MSHUBIRI), UNAWEZA ‘KURUDISHA’ BIKIRA!

MSHUBIRI au msubili ni jina la mimea ya jenasi Aloe katika nusufamilia Asphodeloideae ya familia Xanthorrhoeaceae ambayo ni aina za sukulenti, yaani mimea yenye majimaji.
Huu ni mmea maarufu sana duniani kutokana na kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mengi, na pia unapatikana sehemu nyingi za dunia hasa zile ambazo hazina baridi. Vipodozi vingi vya ngozi vinachanganywa na mmea huu ili kuvipa uwezo zaidi wa kutunza ngozi.
Majani ya mishubiri na dawa zilizotengenezwa kutoka hiyo huitwa shubiri.
Mimea au miti hii ya mishubiri ina shina fupi au haina shina kabisa, isipokuwa spishi zilizo miti. Majani ni marefu na mapana na yanatoka katika shina karibu na wenziwe kama yalivyo majani ya mkonge; lakini majani ya mshhubiri yana miiba kingoni mwao. 
Maua yana umbo la mrija mfupi na yanaweza kuwa ya rangi nyekundu, huzurungi, ya machungwa, njano au nyeupe ambapo mara nyingi ypo mwishoni mwa kikonyo chenye vitawi au bila vitawi. 
Utomvu utokao kwenye majani haya ndio hutumika kutengeneza dawa.
Spishi ambayo inajulikana sana ni mshubirimani (Aloe vera), ambao unapandwa sana duniani na hutumika kwa kutengeneza dawa za uganga au za mitishamba.
Spishi nyingine inayopandwa sana katika Afrika na nchi nyingine za Tropiki ni mshubiri mwekundu (A. ferox).
Mmea huu unatumika zaidi kama majani ingawa shina na mizizi yake nayo ni dawa pia, mmea huu huwa na umbo la mkonge au mmea wa nanasi ila wenyewe ni mdogo kidogo na huwa laini zaidi.
Majani yake yana sehemu mbili, kuna ganda la nje na maji ya ndani (jelly) ganda la nje lina kemikali za kutibu zaidi na ule utando wa ndani una virutubusho vingi sana ambavyo ni kinga za mwili.
Mshubiri ni mmea wenye ‘miujiza’ ya kutibu maradhi sugu kama Saratani, Kisukari, lehemu (cholesterol), malaria sugu, ugonjwa wa kuvimba sehemu ya mwili, vidonda, muwasho wa ngozi na harara, husaidia kusaga chakula, hupunguza uvimbe, na magonjwa mengine mengi.
Hivi sasa watu wengi wamekuwa na utamaduni wa kuweka Aloe ndani ya familia zao kutokana na mmea huo kuwa na faida za kutibu magonjwa mbalimbali.
Si hivyo tu, pia hivi sasa kuna bidhaa nyingi zinazotengenezwa kwa kuchanganya aloe vera kama sabuni za kuogea, dawa za meno, mafuta ya kulainisha ngozi (lotion) na bidhaa nyinginezo nyingi.
Kwa zama nyingi, jamii mbalimbali katika Tanzania na Afrika zimekuwa zikitumia mshubiri kwa mambo mengi, hata inapofikia mama anataka kumwachisha ziwa mtoto hupaka maji maji ya mshubiri kwenye chuchu zake.
Mtoto anaponyonya na kuonja ladha chungu huwa hawezi kurudia tena kunyonya, na hapo huendelea kutumia chakula mbadala.
Binafsi hata mama yangu aliniambia kwamba niliacha nyonyo baada ya kupakaza shubiri, ambapo kule Dodoma wanauita ‘Litembwe’.
Kama unasumbuliwa na homa ya malaria mara kwa mara, chukua majani mawili yaliyo komaa, yaoshe vizuri na kata kata katika vipande vidogo.
Changanya na maji vuguvugu kisha saga kwa kutumia kisagio au twanga kwenye kinu kidogo, chuja na kisha ongeza maji hadi upate bilauri nzima, unaweza kuhifadhi dawa hii kwenye jokofu.
Kunywa vikombe viwili mpaka vitatu kwa kila siku kwa siku 5 - 7. Hii itakusaidia kuongeza kinga ya mwili wako maradufu na unaweza kurudia dozi hii mara baada ya miezi 3 - 4.
Zifuatazo ni faida lukuki za Aloe Vera, yaani mshubirimani:
1. Husaidia kukaza uke
Mara kadhaa imeelezwa kwamba kuna wanawake ambao ‘wananunua bikira’ ili waendelee kuonekana bado kabisa! Lakini huko walikokuwa wananunua yawezekana kuna watu walikuwa wanatengeneza ama wanaendelea kutengeneza fedha kwa miti shamba, na mti wenyewe ni mshubiri.
Shubiri husaidia kukaza misuli iliyolegea. Kwamba unaweza kuchukua aloe vera fresh, chukua jeli yake (maji maji yake) na upakae huko ndani kutwa mara 2 mpaka 3 kwa wiki 3 mpaka mwezi mmoja hivi utaona matokeo yake yataonekana.
Wapo wanawake ambao wanaeleza kwamba, baada ya kutumia ama kupaka aloe vera katika sehemu zao za siri mara nyingi wanasema maumbile yao hukaza na kurejea kwenye ‘usichana’ kana kwamba bado wangali bikira.
2. Hutibu maambukizi katika uke
Unaweza kutibu maambukizi katika uke kwa kupakaa jeli ya aloe vera kwa nje na kwa kuinywa jeli kupata faida yake ya kutibu fangasi. Mililita 70 mpaka 100 za jeli ya aloe vera kila siku zinaweza kusaidia kutibu maambukizi na fangasi katika uke na ikiwa utaendelea kuinywa kwa muda mrefu kunaweza kuzuia maambukizi zaidi kutokujirudia baadaye.
Pia hutumika kurudishia uke uliolegea, pakaa tu huko jeli fresh ya aloe vera kila siku na hutakawia kuwa binti mdogo tena. Dawa nyingine kwa ajili hii ya kurudisha uke uliolegea ni unga wa mbegu za maembe.
3. Hulainisha sehemu kavu za siri
Aloe Vera hufanya kazi kama kilainishi bora kabisa cha asili katika maeneo ya siri kwa jinsia zote mbili na kutoa unyevunyevu wa asili.
4. Hutibu bawasiri
Ile ile sifa moja iliyonayo ya kutibu uvimbe ambayo inaweza pia kutibu malengelenge na uvimbeuchungu kwenye mwako wa mwili, ndiyo hiyo hiyo pia husaidia kutibu au kupunguza maumivu ya bawasiri. Chana tawi la aloe vera freshi na upate jeli yake, kisha pakaa eneo linalosumbuliwa na bawasiri mara mbili mpaka tatu kwa siku kwa wiki kadhaa hasa kama bawasiri imejitokeza sehemu ya nje hadi hapo uvimbe huo utakapopotea.
5. Ni tiba kwa matatizo ya tumbo
Kama utainywa, hutibu vidonda vya tumbo na kiungulia, na kwa ujumla ni kuwa husafisha mfumo wote wa mmeng’enyo wa chakula. Chukua jeli ya aloe vera nusu kikombe (ml 125) changanya na maji ya kawaida nusu kikombe tena kupata ujazo wa  robo lita, changanya vizuri mchanganyiko huu na unywe kutwa mara 2 kwa siku 3 hadi wiki 1 kujitibu matatizo ya tumbo kama kuum, kuondoa sumu, kuunguruma, kuhara na hata kutibu malaria.
Madhara ambayo yameripotiwa kutokana na kunywa aloe vera ikiwa freshi kupita kiasi ndani ya tumbo ni pamoja na kuharisha na matatizo kwenye figo.
6. Huondoa Makeup
Kwa usalama kabisa huondoa makeup kwenye jicho na ni nzuri kwa ngozi laini inayozunguka jicho lako.
7. Husafisha ngozi na kuondoa alama zitokanazo na kuungua na jua
Chunusi, ukurutu na kuungua kwa ngozi kutokana na jua vyote hivi vinatibika kirahisi kwa kutumia aloe vera. Pakaa mara 2 hadi 3 kwa siku katika ngozi mpaka uone umepona kabisa. Mshubiri pia una sifa ya kupoza kama ilivyo menthol ambayo unaufanya mshubiri kuwa dawa ya asili nzuri zaidi katika kutibu alama zitokanazo na kuungua na jua.
8. Ni jeli ya asili ya kunyolea na baada ya kunyoa
Aloe Vera ni dawa ya asili katika kutibu michubuko asante kwa vimeng’enya vyake ambavyo huwa na kiasi kingi cha maji ambayo ni mhimu kuzuia kukauka kwa ngozi. Wakati unanyoa ndevu pakaa jeli ya aloe vera na hata baada ya kunyoa pakaa kama after shave jel kuzuia na kuponya michubuko itokanayo na kunyoa.
9. Huondoa makunyanzi na mikunjo ya ngozi
Ngozi hupenda sana Vitamini C na E ambazo zote zinapatikana katika aloe vera na kusaidia kuboresha unene wa ngozi na kuiacha katika hali ya umajimaji. Ikiwa utachanganya jeli ya aloe vera na mafuta ya asili ya nazi utapata krimu nzuri ya kuongezea viinilishe, mafuta mhimu na unyevunyevu katika ngozi.
Jeli ya Aloe Vera hupenyeza katika ngozi kwa haraka mara nne zaidi ya maji ya kawaida na sifa yake ya kulainisha ngozi husaidia ngozi kubaki na unyevunyevu muda wote.
10. Hutibu homa, malaria na mafua
Jeli ya Aloe Vera huongeza kinga ya mwili. Mshubiri una viinilishe vingi sana mhimu kwa afya ya binadamu. Ina Vitamini A, B, C, na E. Mmea huu una orodha ndefu ya madini mhimu kwa mwili na vimeng’enya vingine mhimu.
11. Vitamini B12 kwa wale wasiotumia nyama (Vegans)
Matumizi makuu ya aloe vera kimatibabu ni kusaidia na kuboresha uundwaji wa bakteria wazuri. Kwa kuongezea aloe vera huwa na jumla ya madini ambayo bakteria huyahitaji katika kutengeneza Vitamini B12.
12. Huongeza nguvu mwilini
Matumizi mengine ya kitabibu ya aloe vera ni kuongeza usawa wa nguvu mwilini. Hii ni kutokana na uwepo wa vitamin b 14 na viinilishe vingine ambavyo husaidia kubadili asilimia kubwa ya chakula katika tumbo lako na kuunda nguvu.
13. Huondoa mba kichwani
Changanya jeli ya asili ya aloe vera na shampoo yako, dakika chache kabla ya kwenda kulala pakaa vizuri mchanganyiko huo kwenye nywele zako na uache zikauke kidogo na usafishe nywele zako asubuhi.
14. Huondoa maumivu wakati wa hedhi
Changanya jeli ya Aloe vera na pilipili manga ya unga kidogo, meza kijiko cha chakula kimoja mara tatu kwa siku kila siku hadi maumivu yatakapoacha.
15. Hulainisha nywele
Jeli ya Aloe vera ni nzuri katika kutibu tatizo la nywele kujisokota na ni mbadala mzuri kwa bidhaa nyingi za madukani zenye gharama kwa ajili ya nywele.
16. Ni dawa ya asili ya kusafishia mdomo
Changanya jeli ya aloe vera ml 100, vijiko 3 vya chai vya baking soda, maji ml 100 na kijiko 1 kidogo cha juisi ya limao. Changanya vizuri vyote kwa pamoja na utumie kama dawa yako ya asili ya kusafishia mdomo.
17. Hutibu matatizo katika mmeng’enyo wa chakula
Juisi ya Aloe vera ni nzuri sana katika kurekebisha matatizo katika mmeng’enyo wa chakula, hurekebisha kuvurugika kwa tumbo na kiungulia. Itumie kama ilivyoelezewa kwenye kutibu matatizo ya tumbo hapo juu namba 4.
18. Hushusha lehemu (Cholesterol)
Tafiti zimeonyesha kuwa kunywa juisi ya aloe vera kwa kipindi kirefu kunaweza kushusha kiwango cha lehemu mwilini. Itumie kama ilivyoelezewa kwenye kutibu matatizo ya tumbo hapo juu namba 4.
19. Hutibu chunusi
Aloe Vera huondoa chunusi kwa kuziondoa seli zilizokufa katika ngozi na hivyo kuvifungua vishimo katika ngozi na kuondoa mafuta yaliyoganda katika hivyo vishimo. Pakaa jeli ya aloe vera moja kwa moja katika eneo lililoathirika na chunusi. Pia makovu yaliyoachwa kutokana na chunusi yanaweza kuondolewa kwa kupakaa jeli ya aloe vera pekee.
20. Hutibu ukurutu na upele
Ukurutu ambao ni matokeo ya juu ya tetekuwanga kwa kawaida hutokea kwa watu wazima wenye kinga ya mwili pungufu. Aloe Vera inaweza kutumika kutibu tetekuwanga zinazosababishwa na kirusi aina ya herpes virus. Kwa kupakaa jeli ya aloe vera moja kwa moja kwenye sehemu zilizowazi hutanua mishipa ya damu jambo linalosaidia kutibu vidonda.
21. Huzuia ngozi kuunguzwa na jua (Sunscreen)
Kupakaa jeli ya Aloe Vera katika mwili hulinda ngozi dhidi ya miale yote ya jua kutua moja kwa moja kwenye ngozi na hivyo kukufanya usizeeke mapema, pia ni dawa nzuri kwa ngozi inayofubaa.
22. Huziimarisha kucha dhaifu
Kwa taratibu pakaa majimaji ya aloe vera juu ya kucha zako sehemu zote juu na chini kila siku na uzitazame baada ya siku kadhaa uone zitakavyokuwa zimerudisha ule uzuri na ugumu wake wa mwanzo.
23. Hutibu vidonda katika mdomo
Mshubiri unazo vitamini na asidi amino ambazo husaidia kuzitengeneza upya tishu zilizoharibika. Tafiti zimeonyesha kuwa watu wanaosumbuliwa na vidonda mdomoni waliotumia jeli ya aloe vera walifanikiwa kutibu karibu asilimia 50 haraka zaidi kuliko wale ambao hawakutumia jeli ya aloe vera.
24. Huzuia na kuondoa michirizi ya tumbo itokanayo na ujauzito
Anza kwa kupakaa majimaji ya mshubiri juu ya tumbo lako na ufanye kama upunaji (massage) hivi taratibu juu ya tumbo mara 2 kwa siku katika kipindi chote cha ujauzito na baada ya kujifungua kwa miezi michache mpaka michirizi ipotee yote.
25. Huondoa uvimbe katika jicho
Weka kiasi kidogo cha majimaji ya aloe vera freshi kisha kuamka asubuhi, acha kwa dakika kadhaa kisha jisafishe. Uvimbe lazima ukimbie. Pia unaweza kuloweka pamba katika majimaji ya mshubiri na kisha jisafishe katika jicho lenye uvimbe.
26. Husaidia wawindaji
Wawindaji wa wanyama katika barani Afrika mara kwa mara hupakaa jeli ya aloe vera katika miili ili kupunguza kutokwa jasho na kuondoa harufu yao ya asili katika mwili isisikike na wanyama.
27. Suluhisho kwa watafuna kucha
Burashi kucha za mtoto anayependa kutafuna kucha na jeli ya aloe vera, ile ladha ya uchungu katika aloe vera itamfanya aache kuzitafuna kucha zake.
28. Hutumika katika kupunguza uzito
Watafiti wameweza kugundua kuwa kunywa juisi ya aloe vera husaidia kupunguza sukari kwenye damu jambo mhimu kwa wale wenye kisukari cha aina ya pili. Wanasayansi wanaamini kuwa kuweka kiwango cha sukari chini hupunguza uzito.
29. Hutibu upungufu wa damu (Anemia)
Kunywa jeli ya aloe vera kunasaidia uzalishaji zaidi wa seli nyekundu za damu katika mwili wako na hivyo kutibu tatizo la kupungua kwa damu.
30. Huondoa maumivu ya mishipa
Kutokana na sifa yake ya kutibu uvimbe, unaweza kutibu uvimbechungu (inflammation) katika maungio yanayopelekea maumivu katika mishipa kwa kupakaa jeli ya aloe vera katika eneo unalosikia maumivu.
31. Hutibu maumivu katika sikio
Matone kadhaa ya aloe vera yakinyunyizwa sikioni yanaweza kuleta nafuu kubwa kama unapatwa na maumivu katika masikio. Hii ni nzuri pia kwa masikio yanayotoa usaha na maumivu mengine katika masikio.
Hapa chini tazama video juu ya namna ya kuandaa jeli ya mshubiri nyumbani kwako na kuinywa kama juisi. Ingawa huyu dada kwenye video analiondoa lile ganda lake la juu lenye rangi ya blue, bado unaweza kuisaga pamoja na maganda yake (isipokuwa ile miiba yake) na bado ikawa nzuri zaidi.


Comments