Featured Post

NAIBU WAZIRI MABULA ACHOCHEA KASI YA UJENZI SHIRIKA LA NYUMBA KATIKA MJI WA SERIKALI MTUMBA


 NAIBU WAZIRI MABULA ACHOCHEA KASI YA UJENZI SHIRIKA LA NYUMBA KATIKA MJI WA SERIKALI MTUMBA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akiingia katika jengo la Wizara ya Viwanda na Biashara wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi katika Mji wa Serikali Mtumba mkoani Dodoma, katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba Dkt Sophia Kongela na kushoto ni Mkurugenzi Dkt Maulid Banyani.

Na Munir Shemweta, DODOMA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amechochea kasi ya ujenzi wa ofisi za serikali katika eneo la Mtumba mkoani Dodoma unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Kasi hiyo inatokana na ziara za mara kwa mara zinazofanywa na Naibu Waziri huyo wa Ardhi katika eneo hilo kwa nia ya kuhakikisha ujenzi wake unakamilika katika muda uliopangwa.
Akiambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa .Dkt Sophia Kongela pamoja na Mkurugenzi wa Shirika Dkt Maulid Banyani jana, Naibu waziri Mabula alijionea maendeleo makubwa ya ujenzi huo ambapo sasa umefikia hatua ya kuezeka.
Mbali na kufikia hatua hiyo, kazi nyingi katika ujenzi huo zinaenda kwa pamoja kama vile kuweka njia za umeme, tiles, utengenezaji madirisha ya nondo pamoja na mashimo ya choo  jambo linaloonesha Shirika limejipanga kukamilisha kazi mapema tofauti na makampuni mengine ya ujenzi yanayofanya kazi kwenye eneo la Mtumba.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akiangalia tiles katika jengo la Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika eneo la Mji wa Serikali Mtumba mkoani Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Dkt Maulid Banyani.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akipita katika moja ya maeneo ya ujenzi wa ofisi katika Mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma alipokwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi zinazosimamiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).Wanaomfuatia kwa nyuma ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba Dkt Sophia Kongela na Mkurugenzi Dkt Maulid Banyani.


Kampuni ya Ujenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa katika eneo hilo la Mtumba inajenga majengo ya ofisi nne za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maenendeleo ya Makazi, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Fedha na Mipango.
Akizungumza  baada ya kukagua kwa mara ya pili ujenzi wa ofisi hizo, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Mabula alisema kasi inayooneshwa na Shirika la NHC katika ujenzi huo ni ishara tosha kuwa shirika hilo kupitia kampuni yake ya ujenzi lina uwezo mkubwa wa kujenga majengo kwa haraka na yenye viwango.
Alisema, hata kama ujenzi wa ofisi zinazosimamiwa na shirika hilo katika eneo la Mtumba utachelewa kidogo lakini ucheleweshaji huo utatokana na MHC kutaka kujenga majengo ya uhakika na yenye ubora unaotakiwa.
Dkt Mabula ameendelea kutoa sifa kwa Ofisi ambazo majengo yake yanasimamiwa na shirika la Myumba la Taifa kutokana na ukaribu inaouonesha katika kipindi chote cha ujenzi kwa nia ya kuwa na majengo yanayokidhi mahitaji ya Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA) na ofisi husika kwa kuwa mawazo ya pande zote yatakuwa yamejumuishwa katika kutekeleza ujenzi huo.
Meneja wa Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Serikali kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Haikameni Mlekio akimuonesha Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba Dkt Sophia Kongela na Mkurugenzi wa NHC Dkt. Maulid Banyani maendeleo ya ujenzi katika ujenzi wa ofisi katika Mji wa Serikali Mtumba mkoani Dodoma.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akiangalia shimo la choo katika wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi za Serikali katika Mji wa Serikali Mtumba mkoani Dodoma.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akiangalia moja ya vyumba katika ofisi zinazojengwa katika Mji wa Serikali Mtumba mkoani Dodoma wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi hizo.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akiangalia madirisha ya nondo ambayo yako tayari kupachikwa wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi za serikali katika eneo la Mtumba. Kulia ni Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Dkt Maulid Banyani.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula akiingia katika eneo la jengo la Wizara ya Fedha na Mipango alipowasili kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa katika Mji wa Serikali Mtumba, kulia ni Mkurugenzi wa Bodi ya NHC Dkt Sophia Kongela na wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Dkt Maulid Banyani.



Comments