Featured Post

INTANETI ITARAHISISHA MAWASILIANO VIJIJINI



NA MWANDISHI WETU
MAENEO ya mijini yameshatoka kwenye mahitaji ya mawasiliano ya mtu mmoja kwenda kwa mwingine na hali hiyo imezifanya shughuli za mawasiliano kutoa mchango mkubwa kwenye shughuli za uchumi na maendeleo.
Lakini maeneo ya vijijini yamebakia nyuma licha ya kwamba yapo mawasiliano mazuri ya simu na kufikiwa kwa teknolojia za kisasa za mawasiliano ya elektroniki kunaweza kuwa ni fursa ya kufikia hatua ya maendeleo kama ilivyo mjini.

Fikiria kuwa kuna mtandao mkubwa wa barabara duniani ambazo zinaruhusu magari kuwa kwenye mwendo wa kasi kwa usalama yakiwa yamebeba mizigo na kuifikisha kwenye maeneo husika bila kukwama.
Hali hiyo inafanya biashara kuendelea kwani malighafi zinazoagizwa zinawasili kwa haraka, kwa wakati, uzalishaji na huduma za viwandani zinaenda kwa ufanisi.
Aidha bidhaa zinazozalishwa pamoja na bidhaa nyingine zinawekwa kwenye orodha ya ushindani wa bei na kufikishwa kwa walaji sehemu mbalimbali duniani.
Kila mtu iwe mkulima anayeishi mwishoni mwa barabara au meneja mauzo wa kampuni kubwa ya biashara ambaye yuko karibu na  uwanja wa ndege anaweza kuunganishwa kwenye mtandao huo.
Hata hivyo hili  linaonekana kuwa wazi kinadharia lakini kiutendaji kuna alama za kuchepukia kwenye  barabara  hiyo  hususani miongoni mwa nchi zinazoendelea.
Kama alama  hizo za kuchepukia  zikiondolewa  kutakuwa na athari gani kwenye maendeleo vijijini?
'Mtandao wa barabara'  unaozungumziwa hapa ni mtandao wa intaneti na  magari  yanayosafiri kwa kasi ni mafurushi ya takwimu za habari. 
Faida kubwa ya intaneti dhidi ya  njia nyingine za mawasiliano  ni kwamba  watu wanaweza 'kuzungumza' na mwingine bila kujali yeye ni nani na yuko  umbali kiasi gani.
Mawasiliano hayo ni rahisi, ya haraka na ya njia mbili tofauti na redio, televisheni au machapisho mengine na wingi na habari tofauti ambazo zinaweza kuhamishwa mara moja zinapeperushwa.
Wakati mtu anapozungumza kwa kutumia simu, sehemu moja ya mfumo wa simu huwa unajielekeza kwenye kuita, ikimaanisha kuwa pindi watu wengi wanapotaka kutumia mfumo wa simu kwa wakati huo mmoja uwezo wake unakuwa hautoshi na huwa hakuna njia inayokuwa wazi.
Pindi watu wawili wanapotumia njia moja kwa mawasiliano ya intaneti mawasiliano hayo hufungwa kwenye vifurushi vidogo vya takwimu ambavyo hutiririka kama mkondo wa magari kwenye  mtandao.
Vifurushi hivi vya takwimu ambavyo huwa vimejichanganya na  takwimu za watu wengine husafirishwa hadi kwenye njia panda  na hata hivyo mawasiliano yanaweza kumegwa kwenye vifurushi tofauti vya takwimu kila kimoja kikifuata njia yake na mpokeaji hupokea ujumbe uliokamilika.
Kwa kuwa mtumaji na mpokeaji wanakuwa na kompyuta, modemu, na vifaa sahihi, njia ya simu na uelewa wa namna ya kutumia kifaa, wanaweza kubadilishana habari.
Hata hivyo watumiaji pia wanahitaji kufahamu namna ya kutumia vizuri yale yote yanayotolewa kupitia intaneti.
Wakulima wanaweza kupata habari kuhusu bei za mazao yao wanayouza nje kuwa ni ya juu kuliko kuuza mazao hayo kwenye soko la mji jirani.
Wanaweza kutaka kufahamu  ni njia gani ya usafiri  itakayotumika kusafirisha mazao hayo  na  itagharimu kiasi gani cha fedha na iwapo  mtiririko huo utakuwa na faida.
Kwenye biashara nyingi jinsi kiwango cha kuhabarishwa kinavyokuwa kikubwa ndivyo muuzaji anavyokuwa na fursa nzuri ya kupata bei nzuri.
Mkulima wa matunda anaweza kutaka ushauri wa kiufundi ili aweze kuamua ni kipindi gani cha kuvuna mazao yake.
Watafiti wa kilimo wanaweza kuhitaji  habari inayohusiana na kazi zao na ambayo wanajua itapatikana tu kwenye vyuo vikuu  sehemu nyingine duniani.
Wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotaka kurudi vyuoni kuendelea na shahada ya juu kwenye vyuo vya ng'ambo wanaweza kuwa na  mawasiliano na wakufunzi au wasimamizi wao ili waweze kumalizia kazi zao za utafiti au maprofesa wa vyuo hivyo vikuu  wanaweza kuhitaji kujifunza kutoka kwa waliokuwa wanafunzi wao.
Intaneti pia inatoa fursa za mafunzo ya elimu-masafa kupitia  sifa rasmi  ambazo zinaweza kutumika kujisomea nyumbani  kwa kutumia mafunzo kwa njia ya intaneti.

Rambaza au zama
Intaneti ni lazima ichukuliwe kama  miundombinu ya mawasiliano  na kwa kuitumia kwa njia mbalimbali huduma kadhaa zinaweza kupatikana kama  vile mtandao mpana duniani (www), barua-elektroniki na habari. 
Mtandao mpana ni huduma kuu ya kutumia katika kujitafutia habari binafsi. Barua- elektroniki (barua pepe) inatumika  kuwasiliana na mtoa habari  moja kwa moja, kuliko ilivyo kwa simu au faksi ambazo hutumwa kwa mtu binafsi au shirika.
Kupatikana kwa habari kwa namna moja  ni kama ubao wa matangazo  ambapo  mtu yeyote, mahali popote  anaweza kuangalia na ambapo  mtu yeyote anaweza kubandika  tangazo lake. Ni njia ya  kuuliza na  kujibu maswali  kutoka kwa watu wanaotaka kuelewa kuhusu  jambo husika.
Watu wengi wanaweza kufaidika na huduma hii kama mashirika  ambayo yanafikia mtandao wa intaneti yanatawanya habari kwa wale ambao hawana namna ya kufikia habari hizo kwa  kuchapishwa au kupitia redio.
Thamani ya habari inategemea na mwenendo wake na hivyo thamani ya swali ambalo inatarajiwa kujibu. Kama swali limejibiwa kwa usahihi hatua hiyo kidogo inaonekana kama ya kimashine jambo ambalo linaifanya kompyuta kuwa ni njia nzuri katika kazi hiyo. 
Kama unatuma maswali kwenye makundi ya majadiliano kwenye mtandao kwa mfano unaweza kupata jibu zuri na sahihi. Kuuliza  swali sahihi kunahitaji stadi zaidi, uelewa na ueledi kuliko kutuma maswali tu.
Kwa mfano katibu wa chama cha wakulima anaweza kuulizwa na wanachama wake kuperuzi kuhusu matumizi ya mbolea ya chumvi chumvi kwa kipindi cha msimu wa mazao ya mahindi.
Jibu linaloweza kutolewa ni kilo 50 za Naitrate kwa hekta, Oksaidi ya fosiforasi kilo tano kwa hekta, Potasiamu kilo 50 kwa hekta;  ambapo  habari inayotakiwa ni 'kila baada ya wiki tatu'. 
Kompyuta ni nzuri katika kutoa majibu lakini ni mbaya katika maswali ya kubuni. Katika kutafuta jibu kwenye mtandao mpana (www) kwa mfano utatoa majibu mengi na njia mbadala ya kupata  majibu shughuli ambayo inaweza kuwa ya kuchosha na hivyo kuachana nayo.
Kuwepo kwa njia ya simu ambayo kwa vyovyote ni muhimu katika kupata intaneti ni vyema kwa katibu huyo kupiga simu kwa duka la pembejeo lililopo karibu na kuulizia ni lini mbolea itapatikana na gharama yake itakuwa ni kiasi gani.
Kama ilivyo kwa njia nyingine za mawasiliano ni muhimu kufahamu namna ya kufafanua ni habari ipi unayoihitaji na namna gani ya kuwasiliana au kuwasilisha matakwa yako.  

Comments