Featured Post

TRUMP ATISHIA KUICHUKULIA HATUA GOOGLE, TWITTER NA FACEBOOK


 Trump hafichi hisia zake juu ya vyombo vya habari, na hata alipokutana na Rais wa Fifa katika ikulu ya White House, japo kwa utani, aliwaonesha wanahabari kadi nyekundu.



NEW YORK, MAREKANI
RAIS wa Marekani Donald Trump amezionya kampuni za mawasiliano ya mtandao Google, Twitter na Facebook kwa kile alichokiita kuminya taarifa zake na za mrengo wa kihafidhina.

Trump ameitaka mitandao hiyo kuwa makini baada ya awali kuishutumu Google kwa kupindua matokeo ya taarifa pale mtumiaji wa mtandao huo anapotafuta habari kumhusu Trump.
Hata hivyo, Google wamekanusha shutuma kuwa mtandao wao unaupendeleo na kusema hawafungamani na itikadi yoyote ya kisiasa.
Akiongea na wanahabari katika ikulu ya White House, Trump amesema, "Google wamekuwa wakihadaa watu wengi, ni jambo zito sana."
Akaziongeza pia kata lawama Twitter na Facebook, "inawapasa wawe makini, hauwezi ukawafanyia watu mambo haya…tunapokea maelfu ya malalamiko juu ya jambo hili."
Rais Trump hatahivyo hajabainisha ni hatua gani hasa ambazo utawala wake unapanga kuzichukua.
Awali mshauri wa Trump wa masuala ya uchumi, Larry Kudlow amesema utawala kwa sasa unaangalia ni namna gani wataliendea suala hilo kwa kuangalia kanuni za udhibiti.
Hatua gani Trump atachukua dhidi ya mitandao?
Wachambuzi wa mambo wanasema ni vigumu kwa Trump kuthibitisha madai yake na haieleweki hasa namna gani atalishughulikia suala hilo.
Hoja iliyopo ni kuwa, hatua yoyote ya kuiubadilisha mtandao wa Google itapelekea kuvunjwa kwa katiba ya Marekani hususan uhuru wa habari, japo yawezekana hatua zikachukuliwa kibiashara zaidi.
Akitumia mtandao wake pendwa wa Twitter, Trump aliishutumu Google kwa kuzipa kipaumbele habari hasi kutoka kwenye vyombo vya habari alivyovitaja kama vya mrengo wa kushoto (waliberali).
Juma lililopita Trump pia aliishutumu mitandao ya kijamii kuwa "inabagugua moja kwa moja sauti za Republican/kihafidhina," na kuahidi kuwa "hatokubali kuacha hilo liendelee."
Facebook na Twitter bado hawajatoa mrejesho juu ya shutuma hizo ila Google wamezipinga vikali.
"Kusaka taarifa kwenye mtandao wetu hakutumiki kuweka agenda za kisiasa na hatufanyi upendeleo wowote kwa itikadi za kisiasa," imesema taarifa ya Google.
Mhadhiri mwandamizi wa teknologia za kidijiti kutoka chou cha King's College London Mercedes Bunz, ameiambia BBC kuwa haiyumkiniki kuwa Google wamekuwa wakipangilia taarifa katika mtandao wao kwa upendeleo wa kisiasa.
Kwa mujibu wa mtaalamu huyo, mpangilio wa mtaandao huo huangalia zaidi uhalisia wa taarifa na ukaribu wa kijiografia wa watumiaji wake.



Comments