Featured Post

ZAWADI YA MAGUFULI KWA OBAMA NA UKOO WAKE MZIMA ULIVYO

DAR ES SALAAM, TANZANIA
RAIS mstaafu wa Marekani Barack Obama amekuwa kwenye ziara barani Afrika ambapo sehemu ya ziara hiyo imekuwa ya faragha na nyingine ya wazi.
Kuna mambo mengi sana ambayo ameyatenda na kuyasema wakati wa ziara hiyo yake ya kwanza Afrika tangu alipostaafu urais mapema mwaka jana.
Obama alianza ziara yake kwa usiri mkubwa, mapumzikoni katika hifadhi ya taifa ya Serengeti nchini Tanzania.

Picha zake akiwa mbugani zilianza kuenezwa mitandaoni mwanzoni lakini hakukuwa na thibitisho rasmi kwamba alikuwa nchini humo.
Kilichofahamika wazi tu ni kwamba alitarajiwa kuwa nchini Kenya mnamo 15 Julai kukutana na Rais Kenyatta na baadaye 16 Julai afike nyumbani kwa babake Kogelo, Siaya magharibi mwa Kenya.
Serikali ya Tanzania ilisalia kimya kuhusu uwepo wake Tanzania hadi pale alipoondoka nchini humo na kutua jijini Nairobi.
Ni hapo ambapo Msemaji Mkuu wa Serikali, kupitia mtandao wa Twitter alipakia picha mbili za Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Dkt Augustine Mahiga akiwa na Bw Obama katika uwanja wa ndege.
Ujumbe ulioambatana na picha hizo ulikuwa: "Rais Mstaafu wa Marekani @BarackObama amehitimisha mapumziko ya siku 8 pamoja na familia yake katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti nchini."
Fasiri ya ujumbe hiyo ilikuwa kwamba picha hizo zilikuwa za wakati wa kumuaga baada yake kukamilisha ziara yake ya siku nane nchini humo.

Obama alikuwa na mke na watoto


"Amefurahi sana kuja, yeye mkewe na watoto wake. Na amekuwa hapa nchini kwa siku nane. Nilimpokea hapa, akaomba kwamba mapokezi haya yawe kimya kimya kwa sababu angependa awe na faragha huko mbugani," alisema Dkt Mahiga kwenye video fupi iliyopakiwa katika ukurasa wa Twitter wa msemaji wa serikali ya Tanzania.
Baadhi ya picha ambazo zimekuwa zikienea mitandaoni zinamuonesha mke wa Obama, Michelle, akiwa pamoja na mumewe.
Michelle hata hivyo hakusafiri na mumewe Kenya na wala hakuonekana nchini Afrika Kusini.
Bw Obama alipozuru Kenya akiwa rais mwaka 2015 pia hakuandamana na mkewe na watoto ingawa nchini Tanzania mwaka 2013 alikuwa ameandamana na Michelle.
Badala ya kuingia Kenya, Michelle na watoto wao Malia na Sasha walifululiza hadi Ulaya kuhudhuria tamasha ya muziki ya Jay-Z na mke wake Beyonce jijini Paris, Ufaransa.
Michelle aliketi karibu na mamake Beyonce, Tina Knowles Lawson, kwenye viti vya mbele wakati wa tamasha hiyo in the front row - and even getting a quick onstage smile from Jay-Z. Wakati mmoja alisimama kucheza akiwa na binti yake Sasha, ingawa hakuna taarifa kumhusu Malia.
Familia ya Jay-Z ambaye jina lake halisi ni Shawn Corey Carter na ya Obama zina urafiki wa karibu. Barack Obama alishiriki kwenye sherehe ya kumuingiza Jay-Z kwenye orodha ya watunzi nyimbo maarufu, Songwriters Hall of Fame, na kumweleza rapa huyo kama "kitu halisi cha Marekani".
"Nafikiri mimi na Bw Carter tunaelewana vyema," alisema. "hakuna mtu yeyote ambaye alituona tukiwa vijana angetarajiwa tuwe hapa tulipo leo."

Zawadi ya Magufuli

Jumapili Mahiga alialikwa pia kumuaga Obama, ambapo pia alimpokeza zawadi kutoka kwa Rais wa Tanzania.
"Nimemkabidhi zawadi kutoka kwa mheshimiwa rais ambayo imechorwa na kijana wetu ambayo inaonyesha wale nyumbu wanapovuka Mto Mara ambayo inaitwa The Great Migration, moja ya maajabu ya dunia," alisema Dkt Mahiga.
Kwa mujibu wa waziri huyo, Obama alisema picha hiyo itamkumbusha kitu adimu na adhimu ambacho alikishuhudia mbugani.
Kiongozi huyo alisema kwamba angependa kurejea na kwamba atawashawishi marafiki zake wafike pia kutembea.

Kukutana na Kenyatta na Odinga

Alipowasili nchini Kenya, Obama alilakiwa na dada yake Auma Obama - ambaye ana uhusiano wa karibu sana naye - pamoja na baadhi ya maafisa wa serikali na mara baadaye akaelekea ikulu ambapo alikutana na Rais Uhuru Kenyatta na naibu Rais William Ruto.
Kiongozi huyo wa zamani wa Marekani baadaye alikutana na kiongozi wa upinzani Kenya waziri mkuu wa zamani Raila Odinga katika inayoaminika kuwa mgahawa wa Villa Rosa Kempinski katika mtaa wa Westland, Nairobi na huenda ndiko alikolala kabla ya kuelekea Kogelo Jumatatu asubuhi.
Obama aikuwa amezuru nchini Kenya mara tatu 1987, 1992 na 2015 wakati alipokuwa akihudumu kwa awamu ya pili ya urais.

Kukumbuka mapokezi ya nyumbani siku ya kwanza

Obama aliongoza ufunguzi wa kituo cha vijana cha elimu kwa jina Sauti Kuu, ambacho kilianzishwa na dada yake Auma Obama, kilichofufua kumbukumbu ya safari yake ya kwanza kabisa nyumbani mwa baba yake akiwa na miaka 27.
Alisimulia "baada ya kutua Nairobi nilipanda treni ya kasi ya chini sana kisha nikaliabiri basi lililokuwa limebeba kuku na viazi vitamu kando yangu," aliongeza kuwa alipanda gari la uchukuzi la umma lililokuwa limejaa watu kuliko basi kwenda nyumbani mwa Mama Sarah Obama, bibi yake wa kambo.
Alisimulia jinsi alivyooga nje na alivyomshika kuku kuwa kitoweo cha jioni alipohisi njaa wakati akiwa ameenda kuzuru kaburi la baba yake.
Alizungumzia pia ufisadi ambao umekithiri katika mataifa mengi ya Afrika na mivutano ya kisiasa.
Ujumbe mkuu kwa Afrika na Dunia hotuba ya Mandela
Shughuli kuu zaidi ya ziara ya Obama Afrika ilikuwa kutoa mhadhara wa Nelson Mandela kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 100 tangu kuzaliwa kwa rais huyo wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini ambaye alipigana vikali dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo.
Ilikuwa mara yake ya kwanza kutoa hotuba kuu jukwaani duniani tangu alipoondoka madarakani mapema mwaka jana na kukabidhi mamlaka kwa Rais Donald Trump.
Mandela Day is about taking action to change the world for the better. In these young people, I see Madiba's example of persistence and hope. They are poised to make this world more peaceful, more prosperous, and more just. pic.twitter.com/GJDuOs1hkH
— Barack Obama (@BarackObama) 18 Julai 2018
Obama alionekana kukosoa utawala wa Bw Trump alipozungumzia kuibuka tena kwa viongozi wababe ingawa pia huenda aliwalenga baadhi ya viongozi wa Afrika. Alizungumzia pia ubaguzi na kueleza matumaini kwa vijana.
Haki miliki ya picha AFP Inakadiriwa watu 15,000 walihudhuria mhadhara huo
Obama alisema kwamba Marekani changamoto dhidi ya utandawazi mwanzoni zilitoka kwa wanasiasa wa mrengo wa kushoto na kisha zikaanza kutokea kwa wanasiasa wa mrengo wa kulia.
Alisema madhara ya kudorora kwa uchumi wa dunia mwaka 2008 - na kutomakinika kwa wasomi na watawala - vilizifanya ahadi zilizotolewa kwa watu kuwa hewa tu.
"Siasa za kuwatia watu hofu na kutoridhika na kuwa na misimamo mikali zilianza kuwavutia watu. Na siasa za aina hiyo sasa zinashika kasi," Obama amesema.
"Viongozi wenye nguvu kuu kisiasa wameanza kuchipuka...wale walio mamlakani hujaribu kuhujumu kila taasisi au utamaduni unaoipatia demokrasia maana," aliongeza.

Ubaguzi na Ufaransa kushinda Kombe la Dunia

Katika mhadhara huo wa Mandela,Bw Obama alisema hushangaa sana kwamba wakati huu ni lazima kwake kuwakumbusha watu kuhusu kuwaheshimu watu wa rangi, asili, dini na wapenzi wa jinsia moja.
Amesema anashangazwa na hilo kwamba linafanyika miaka mingi baada ya Nelson Mandela kuondoka gerezani.
"Inaonekana ni kama tunaelekea kwa siasa za kukaripiana, mapambano ya kuhakikisha haki za msingi bado hayakamilika kwa kweli. Ni lazima tuwe macho dhidi ya watu wanaojaribu kujitukuza kwa kuwashusha hadhi wengine," amesema.
Barack Obama alisema usawa katika jamii huwezesha vipaji vya kila mmoja kuifaa jamii.
"Itazame timu ya taifa ya kandanda ya Ufaransa," amesema. "Si wote walionekana kama wa asili ya zamani ya Ufaransa, lakini wote ni Wafaransa - ni Wafaransa."
Ufaransa walishinda Kombe la Dunia Jumapili kwa mara ya pili katika miaka 20, wakiwa na kikosi ambacho wengi wa wachezaji ni wahamiaji au wazazi wao walikuwa wahamiaji.

Vitabu sita anavyotaka watu wasome kwa sasa

Obama huwa kawaida anatoa ushauri kuhusu vitabu anavyovisoma, nyimbo anazozisikiliza na vitabu ambavyo angependa watuwasome.
Ijumaa wiki iliyopita, katika kilichoonekana pia kama njia ya kuficha alikokuwa, alidokeza kwamba angefanya ziara Afrika na kutoa orodha ya vitabu vilivyoandikwa na Waafrika na kuhusu Waafrika ambavyo angependa watu wavisome.
This week, I’m traveling to Africa for the first time since I left office – a continent of wonderful diversity, thriving culture, and remarkable stories. As I prepare for this trip, I wanted to share a list of books that I’d recommend for summer reading: https://t.co/W4Jc0N23iy
— Barack Obama (@BarackObama) 13 Julai 2018
Vitabu hivyo ni Things Fall Apart cha Chinua Achebe, A Grain of Wheat cha Ngugi wa Thiong'o, Long Walk to Freedom cha Nelson Mandela, Americanah cha Chimamanda Ngozi Adichie, The Return cha Hisham Matar naThe World As It Is cha Ben Rhodes.

Comments