Featured Post

VIDEO: AGIZO ALILOTOA WAZIRI KIGWANGALLA MKOANI SIMIYU, LIPO LA KUMTAKA MUWEKEZAJI KUSALIMISHA HATI



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa miezi mitatu kwa muwekezaji wa hoteli ya kitalii ya Kijereshi Tented Camp kurudisha kwa Kamishna wa Ardhi hati miliki ya kipande cha ardhi chenye ukubwa wa hecta 464 kilichopo ndani ya pori hilo kwakuwa ni batili.
Aidha, amewapa siku 45 wananchi wanaoishi kinyume cha Sheria ndani ya eneo la kinga (bufer zone) za Pori la Akiba Kijereshi kuondoka kwa hiari yao wenyewe kabla ya kuanza operesheni ya kuwaondoa kwa nguvu.

Comments