- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
MAMA yake mwanamuziki nyota Afrika Mashariki, Diamond
Platnumz, Sandra, hatimaye amemtambua mjukuu wake wa tatu aliyezaliwa na
mwanamitindo Hamisa Mobetto kutoka Tanzania.
Sandra amedaiwa kukataa kutambua uhusiano wa mwanawe na
Hamisa Mobetto, hatua iliomfanya Diamond kumuomba mamake hadharani kuwapenda
wajukuu wake wote kwa usawa.
Na wakati wa siku yake ya kuzaliwa, Sandra alirekodiwa
katika kanda ya video akisema, ''Si Dylan ni mume wangu?"
Familia yake ambayo ilikuwa imekusanyika katika hafla hiyo
ya kukata keki walimpigia makofi wakisherehekea.
Sandra baadaye aliendelea na kukata keki ya Dylan ambayo
alikuwa ameletewa kusherehekea siku hiyo ya kuzaliwa kwake.
Sandra hupendelea sana kuchapisha kanda za video na picha za
wajukuu wake wawili Tiffa na Nillan waliozaliwa na mfanyibiashara wa Uganda
Zari Hassan.
Amekuwa akikosolewa kwa kumpuuza Daylan na kutochapisha
picha zake katika akunti yake.
Diamond alivyoingilia
kati
Ilimlazimu mwanawe Diamond kuingilia kati kwa yeye kuweza
kumtambua mwana aliyezaliwa na Mobetto.
Katika chapisho lake la mtandao wa instagram Diamond alimrai
mamake kuwapenda wajukuu zake wote bila upendeleo wowote akisema kuwa hawana
hatia wala hawajui chochote.
Aidha, alimtaka Sandra kutojiingiza katika maswala ya
kibinafsi kati yake na mama za wajukuu zake akisema kuwa yeye ndio wa kulaumiwa
kwa hayo yote.
Vilevile aliwataka mashabiki wake kutopendelea upande wowote
katika swala la wanawe watatu akisema wote ni wake na kwamba hakuna anayepaswa
kumtenga mwana wa Mobetto.
Hivi ndivyo alivyoandika katika mtandao wake wa Instagram:
"Diamond
Platnumz: I can't Stop Wishing you Happy Birthday Mom... Coz i Love you So
Much, na Najua kias gani pia Unanipenda Mwanao, Unanipenda kias kwamba hata
Unachukia yoyote anaejaribu kufanya kitu cha kuniharibia Katika Maisha
Yangu...Utanilinda na kunitetea Hata kama pengine mgomvi nilikuwa ni mimi
Mwanao, ila you will always be on my side......Katika Kusheherekea siku yako
hii kuu ya kuzaliwa, ningeomba Pia, kama Unipendavyo Mwanao pia Uwapende
wajukuu zako wote, kwani ni wadogo na Hawana hatia wala hawajui
chochote...Najua wakati mwingine wazazi wao wanakukwazaga sana, kutokana na
Issue zetu Binafsi za mimi na wao kukuingiza wewe ama kukuletea lawama wewe
ilhali maskini ya Mungu hata napowatoaga hujui, unaonaga tu na wewe ghafla niko
na flani.... na kwa umri nilofikia hata kama hupendezwi kias gani, ila huwezi
nichapa viboko ama kunicontrol kuwa eti kwanini niko na fulani....hivyo ni kosa
langu mimi binafsi ila wao wanatakaga kukupa lawama kama wewe jaji wa mahusiano
yangu... ila kwa Upendo wako kwangu naomba Unisamehe mie kwani ndie Chanzo cha
Hayo yote... na Uwapende Wajukuu zako wote kwani ni watoto na hawajui
chochote.....Na wakukwazapo Wazazi wao Wakuwahukumu wao hata wakitumia ngao ya
watoto kukukwaza.......Watu wa Mitandaoni watasheherekea na kuunda timu kwa
faida za Mam za watotoila si kwa faida za watoto maana hakuna hata mkoja alowai
nichangia hata ela ya pempaz kwanhawa watoto, na wakimaliza kuchonganisha
familia yetu kupitia mitandao, wao wanarudi makwao kukaa na nafamilia zao huku
weww wnakutengenezea matabaka katika familia yao.....Mama angu kipenzi familia
nilokuletea Mwanao ni @deedaylan @princess_tiffah @princenillan, hao ndio
familia yako tokea kwangu, na siku nikioa huyo ndio atakuwa mwengine kwenye
Familia..... Nakupenda sana na Nakutakia Maisha maref yenye furaha na Afya Tele
Mama💕💖💕💖@mama_dangote💕💖💕💖"
Tayari baadhi ya mashabiki wake wamepongeza hatua hiyo ya
mamake kumkubali mjukuu wake wa tatu licha ya uhusiano wake na Mobetto.
Comments
Post a Comment