- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Ripoti ya Global Innovation Index (GII) 2018 Imetolewa mjini
New York nchini Marekani, katika toleo lao la 11 ambalo linalenga kuwasaidia
watunga sera kuelewa namna ya kuchochea shughuli za uvumbuzi na ubunifu ambazo
zinaweza kusukuma gurudumu la maendeleo ya watu na uchumi.
Ripoti hiyo imetoa orodha ya mataifa yanayofanya vyema
kwenye masuala ya uvumbuzi duniani, Kenya, Rwanda, Afrika Kusini na Mauritius
zikiwa nchi zinazofanya vizuri kusini mwa jangwa la Sahara.
Ripoti hii imezitazama nchi 126 duniani kwa kuzingatia
viashiria vya mazingira ya kisiasa, elimu,miundombinu, biashara na uchumi.
Afrika Kusini
Ni nchi ya kwanza kwenye orodha hiyo kwenye eneo la kusini
mwa jangwa la sahara na nafasi ya 58 duniani.Imeonyesha nguvu yake kwenye sekta
ya masoko na biashara, pia katika masuala ya mikopo ya kibenki, ubora katika
tafiti mbalimbali za kisayansi kwenye vyuo vikuu vyake hasa Cape Town , Chuo
kikuu cha Witwatersrand na Stellenbosch.
Mauritius
Imeifuatia Afrika Kusini, kutokana na nguvu iliyoonyesha
kwenye masuala ya kibiashara, mazingira ya ukopeshaji, usalama na uimara
kisiasa, pia imekuwa ikiwezesha kusomesha wanafunzi wa sekondari, umahiri
katika matumizi ya nishati na biashara.
Kenya
Kenya imefanikiwa kwa kiasi kikubwa ukiwa ni muendelezo
tangu mwaka 2011, ikionyesha mafanikio kwenye utoaji mikopo kwa wafanyabiashara
wadogowadogo na wajasiriamali, usafirishaji wa biashara ya bidhaa zitokanazo na
ubunifu kama vile uchongaji na uandishi.
Nchi nyingi za kiafrika hazijaonekana wenye ripoti hii
kutokana na changamoto mbalimbali ambazo wataalamu wa masuala ya kiuchumi
wameziweka wazi.
Tanzania ni Miongoni wa nchi za Afrika Mashariki ambazo
hazimo katika ripoti hii.
''Kwa sehemu kubwa ripoti hizi hutolewa kutokana pia na kasi
ya kujitangaza, lakini pia serikali yetu ina wabunifu wengi sana lakini tatizo
ni kuwa hawapati nafasi ya kuendelezwa baada ya uvumbuzi , hakuna taasisi
zinazowajibika kuwaendeleza watu wanafanya vizuri katika kazi mbalimbali za
ubunifu na uvumbuzi na kuwawezesha kwa kuboresha na kutangaza kazi zao ndani na
nje ya mipaka ya Tanzania'' ameeleza mchambuzi wa masuala ya kiuchumi na
kijamii, Betty Masanja.
''Maendeleo yeyote yanakuja kutoana na tafiti mbalimbali
ambazo hufanywa na kufanyiwa kazi na serikali husika ili kusaidia katika
kusukuma maendeleo ya nchi husika kwa mfano katika fani za sayansi, uchumi na
biashara''.
''Iwapo serikali zetu zitaishia kuweka tafiti hizi kwenye
makablasha basi upigaji hatua katika kuyafikia maendeleo utakuwa mgumu''
alieleza.
Comments
Post a Comment