- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Kamati ya maandalizi ya shindano la Warembo wa Morogoro (Miss
Morogoro 2018) imeanza kutoa misaada mbalimbali kwa jamii ambapo kwa imetoa
bati 35 katika shule ya msingi Muungano
iliyopo kata ya Mafisa manispaa ya Morogoro.
Mkurugenzi wa Miss Morogoro Farida Kulususu akizungumza
wakati wa kukabidhi mabati shuleni hapo,alisema wao kama kamati kwa
kushirikiana na warembo wao wameonelea kutoa mabati hayo kwa ajili ya kuezeka
chumba cha darasa moja ambalo lilikuwa wazi kwa muda mrefu.
Farida ambaye pia ni mkurugenzi wa Nyumbani Park/Samaki Spot
Morogoro, alisema pamoja na kuwepo kwa changaamoto nyingi katika shule za
msingi hasa katika ujenzi wa madarasa, na uhaba wa madawati aliwaomba wahisani
wengine kujitokeza kusaidia katika maeneo hayo kwa shule hiyo na shule nyingine
zenye mahitaji.
“Sisi kama kamati yaa Miss Morogoro kwa kuanzia tumeona
tutoe mchango wetu wa bati ambazo zitasaidia kwa darasa moja na tutajitahidi
kusaidia katika maeneo mengine kwa kadri tutakavyo jaliwa,”alisema Farida.
Kaimu mwalimu mkuu wa shule ya msingi Muungano Clemence
Mgana akishukuru baada ya kupokea bati hizo alisema, shule bado imekuwa
ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya kutokamilika kwa majengo manne
ya vyumba vya madarasa.
Mgana alisema shule hiyo pia inakabiliwa na uhaba wa
madawati kwa darasa la tatu ambao baadhi yao wamekuwa wakikaa chini.
“Madawati yaliyopo sasa ni 305, mahitaji ni 503 upungufu 196
huku wanafunzi walioandikishwa kwa darasa la kwanza 2018 ni 296,hatuna ofisi ya
walimu kwani kwa sasa walimu wanatumia darasa moja wapo,” alisema Mgana.
Mmoja wa wanafunzi katika shule hiyo Fatuma Athumani
alizungumzia tatizo la maji katika shule hiyo ambayo imedumu kwa muda mrefu
jambo linalowalazimu wanafunzi kubeba maji kwenye dumu ndogo na kwenda nayo
shule.
Comments
Post a Comment