Featured Post

GEREZA LA KWITANGA KUWA KITUO KIKUU CHA MICHIKICHI-MAJALIWA


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mazao ya michikichi yaliyokuwa  
yakikamuliwa kuwa mafuta ya kula wakati alipotembelea Gereza la Kwitanga 
mkoani Kigoma kujionea kilimo cha michikichi na uzalishaji wa mafuta ya 
mawese katika gereza hilo Julai 29, 2018. Kushoto ni Waziri wa Elimu, 
Sayansi, Teknolojiwa na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, Kulia ni Naibu 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamadi Masauni na kulia kwa 
Waziri Mkuu ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba. (Picha na 
Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeliteua Gereza la Kwitanga 
lililopo wilayani Kigoma kuwa kituo kikuu cha uzalishaji wa zao la 
michikichi nchini.
Hivyo ameuagiza uongozi wa gereza hilo 
waongeze nguvu katika uzalishaji wa michikichi kwa kupanua mashamba na 
kuongeza askari wenye ujuzi wa kilimo cha michikichi na kupanda miche 
mipya ya michikichi na kukata ya zamani. Waziri Mkuu ameyasema 
hayo leo (Jumapili, Julai 29, 2018) wakati alipotembelea gereza hilo 
akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi yenye lengo la kufufua 
zao la michikichi mkoani Kigoma.
Amesema Serikali imedhamiria 
kwa dhati kufufua kilimo cha zao la michikichi mkoani Kigoma, hivyo kila 
mwananchi lazima awe na shamba la michikichi.Katia hatua nyingine, 
Waziri Mkuu ameuagiza Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kigoma Bw. Sabas Matolo 
kuhakikisha Gereza la Kwitanga linawezeshwa kwa kuwa na zana bora na za 
kisasa za kilimo yakiwemo matrekta na vifaa vya kuvunia ili waweze 
kuongeza uzalishaji wa mafuta. 
Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Bw. 
Matolo awahamishe askari ambao ni wataalamu wa kilimo wenye ujuzi wa 
zao la michikichi kutoka kwenye Magereza mengine mkoani Kigoma na 
kuwahamishia katika gereza la Kwitanga ili kuimarisha uzalishaji.
Waziri 
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kitalu cha kuzalisha miche ya Michikichi 
cha Asasi ya Seed Change katika kijiji cha Simbo kwenye jimbo la Kigoma 
Vijijini Julai 29, 2018. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi hiyo, 
Alex Chetkovic.
Wananchi 
wa Kijiji cha Kazuramimba wilayani Uvinza wakimshangilia Waziri Mkuu, 
Kassim Majaliwa wakati aliposimama kijijini hapa kuwasalimia Julai 29, 
2018. Alikuwa njiani kwenda Uvinza kuendelea na ziara ya mkoa wa 
Kigoma. 
Waziri 
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Kazuramimba 
wilayani Uvinza alipokuwa safarini kwenda Uvinza akiwa katika ziara ya 
mkoa wa Kigoma Julai 29, 2018.

Comments