- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Iwapo unazungumzia kuhusu fedha, kuhusu muziki bora, tuzo na
ushawishi basi Diamond ndio mwanamuziki mwenye ufanisi Afrika mashariki.
Kifedha msanii huyo wa muziki wa bongo anamiliki mali
Tanzania mbali, biashara zilizofanikiwa, na ameteuliwa na kushinda mataji
kadhaa ya kimataifa kama vile BET na MTV.
Ushawishi wa msanii huyo unaweza kupimwa na mashabiki wake
katika mitandao ya kijamii: Kwa mfano ana mashabiki milioni 4.8 katika mtandao
wa Instagram, milioni 2.5 katika mtandao wa facebook na milioni 1.3 katika
mtandao wa Youtube mbali na wafuasi elfu 574 katika mtandao wa Twitter.
Na hivi majuzi msanii huyo wa wimbo 'Iyena' na 'sikomi'
alichapisha orodha ya watu waliokuwa kiungo muhimu katika ufanisi wake.
Alimuorodhesha mamake Sanura Kassim, AY TID, Dully Sykes,
Jay Z , P Diddy, Usher Raymond miongoni mwa wengine kama watu waliochangia sana
katika kukuwa kwa muziki wake.
Sanura Kassim
Mamake Diamond Platinumz
AY
Ambwene Allen Yessayah, kwa jina maarufu A.Y. ni msanii wa
muziki wa Hip Hop nchini Tanzania.
Alizaliwa tarehe 5 mwezi July, 1981, mjini Mtwara, Kusini
mwa Tanzania.
Alianza usanii na kundi kwa jina S.O.G. mwaka 1996.
Mwaka 2002 aliamua kufanya muziki akiwa pekee.
Amewahi kushinda mataji kama vile Channel O Music Video
Awards, Pearl of Africa Music Awards.
Vilevile amewahi kuteuliwa kuwania mataji ya MTV Africa
Music nyimbo bora ya Hip Hop.
Aligonga vichwa vya habari baada ya kanda ya video ya wimbo
wake 'Zigo' alioimba na Diamond Platinumz kupigwa marufuku nchini Tanzania.
Video hiyo ilipogwa marufuku kutokana na picha zake za
utupu.
TID
Ni mwanamuziki wa Tanzania ambaye jina lake kamili ni Khalid
Mohamed.
TID ina maana ya 'Top In Dar es Salaam' mjini anakoishi.
Anajulikana sana kwa nyimbo zake 'Zeze' na 'siamini'.
Alianza kuimba mwaka 1994 na kundi kwa jina Black Gangsters.
Alianza kuimba pekee miaka mitano baadaye akiwa na umri wa
miaka 21 baada ya kuandikisha mkataba na Poa Records.
Wimbo wake wa kwanza 'Mrembo' ulitolewa 2002.
Aliwahi kuigiza katika filamu ya Girlfriend.
Dully Sykes
Msanii huyo anayejulikana kikamilifu kama Abdul Sykes
alizaliwa tarehe 4 mwezi Disemba 1980.
Ni msanii wa Tanzania anayejulikana kuwa miongoni mwa
waanzilishi wa muziki wa bongo fleva nchini humo.
Pia akijulikana kuwa Mr Misifa ama Mr Chicks amezuru
Uingereza na ni mmoja wa waanzilishi wa muziiki wa kiswahili wa dance Hall
katika maeneo ya maziwa makuu.
Ni maarufu kwa nyimbo zake Julieta, Salome, Historia ya
Kweli na Leah.
Mr. Blue
Khery Sameer Rajab alizaliwa tar. 14 Aprili 1987.
Ni msanii wa muziki wa R&B na Bongo Flava kutoka nchini
Tanzania.
Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Mr. Blue.
Alifanikiwa kujizolea umaarufu mkubwa huku akipendwa na
wapenzi na mashabiki wa muziki, mara tu baada ya kuingia katika fani ya muziki
na wimbo wake 'Mr Blue' ambapo baadaye ikaja kuwa kama ndiyo jina lake la
kisanii.
Mr Blue alikuwa gumzo wa wimbo 'Mr Blue' kabla ya kuja
kupata umaarufu zaidi na wimbo wake wa 'Mapozi', ambao ndiyo uliomzidishia
kupendwa kutokana na mpangilio wa mashairi na sauti aliyotumia pamoja na ujanja
wa ala ya muziki wenyewe.
Q Chila
Eric Shigongo
Eric Shigongo ni mjasiriamali ambaye alijikita katika
uandishi wa vitabu.
Amezaliwa mnamo tarehe 10- 8-1969.
Mpaka sasa ana vitabu vingi kamaː
Malkia wa Masokwe, Damu na Machozi, Raisi Anampenda Mke Wangu, Siri Iliyotesa
Maisha Yangu na mwisho Maisha ya Mike.
Jay-Z
Akijulikana kwa jina Shawn Corey Carter (alizaliwa mnamo
tarehe 4 mwezi Disemba 1969) akijulikana kama Jay-Z.
Ni mwanamuzi wa wa aina ya Rap , mtunzi, mwandishi,
mtayarishaji na mfanyibiashara.
Ni miongoni mwa wasanii ambao muziki wao umeuzwa sana
duniani na mmoja wa wanamuziki wakubwa wa mtindo wa Rap.
Ameshinda tuzo 21 za Grammy Awards, pamoja na Kanye West..
Joseph Kusaga
Ni mkurugenzi wa Cloud Media nchini Tanzania
Joseph Kusaga ni mjasiriamali mwenye mawazo makubwa na ujuzi
aliyependa muziki.
Awali Joe aliwahi kuwa DJ na alishiriki katika hafla tofauti
za muziki katika maeneo mengi nchini Tanzania akicheza muziki.
P Diddy
Kwa jina Sean John Combs (alizaliwa mwezi Novembea 4, 1969),
kwa jina maarufu kama Puff Daddy, Puffy, P. Diddy, Diddy.
Ni msanii wa Marekani, mwimbaji, mtunzi, muigizaji,
mtayarishaji na mfanyibiashara.
Alizaliwa mjini New York na kulelewa katika eneo la Mount
Vernon, mjini New York.
Alifanya kazi kama mkurugenzi wa vipaji katika kampuni ya
Uptown Records kabla ya kuanzisha kampuni yake ya Bad Boy Entertainment 1993.
Albamu yake ya kwanza No Way Out (1997) iliuza mara milioni
saba
Usher Raymond
Usher Raymond IV (alizaliwa mnamo mwezi Oktoba tarehe 14,
1978).
Ni msanii wa Marekani , mwandishi na mchezaji densi.
Alizaliwa mjini Dalls, Texas ma kulelewa katika eneo la Chattanooga, Tennessee
hadi alipoelekea Atlanta, Georgia.
Akiwa na umri wa miaka 12, alimuigiza katika shindano la
kuimba kabla ya kuvutia kampuni ya muziki ya A&R kutoka LaFace Records.
Alitoa albamu yake, Usher (1994) lakini alipata umaarufu
miaka ya 90 alipotoa albamu yake ya pili My Way (1997).
Shah Rukh Khan
Shah Rukh Khan (alizaliwa na kupewa jina Shahrukh Khan;
tarehe 2 mwezi Novemba 1965).
Akijulikana kama SRK, ni muigizaji wa filamu na
mtayarishaji.
Akijulikana katika mtandao kama "Badshah of
Bollywood", "King of Bollywood", "King Khan", ameigiza
katika takriban filamu 80 na kushinda mataji kadhaa ikiwemo lile la 14 Filmfare
Awards.
Khan ana ushabiki mkubwa barani Asia pamoja na nchini India.
Ametajwa kuwa mmojawapo wa waigizaji waliofanikiwa zaidi
duniani.
Said Bakhresa
Said Salim Awadh Bakhresa (alizaliwa 1949 Zanzibar). Ni
mfanyibiashara wa Tanzania.
Ndio mwanzilishi na mwenyekiti wa kampuni za Bakhresa Group
Of Companies.
Ni mfanyibishara nchini Tanzania na kisiwa cha Zanzibar.
Comments
Post a Comment