- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NEW YORK, MAREKANI
NYOTA wa zamani wa kipindi cha Keeping Up With the
Kardashians, Kylie Jenner, ana thamani ya Dola milioni 900 akiwa na umri wa
miaka 20, kulingana na Forbes.
Jarida hilo la biashara limesema kuwa nyota huyo wa mtandao
wa kijamii anaelekea kuwa bilionea mwenye umri mdogo duniani.
Nyota huyo wa mitindo ambaye, ndio mwana mdogo wa familia ya
Kardashian, alizindua kampuni ya vipodozi miaka miwili iliopita.
Akilinganishwa na dada yake wa kambo, Kim Kardashain West
mwenye umri wa miaka 37, thamani ya msichana huyo imeipiku ile ya dadake mkubwa
kwa takriban $350m.
Jenner ambaye hajafikisha miaka hata ya kunywa pombe nchini
Marekani atafikisha umri wa miaka 21 mnamo mwezi Agosti, huku toleo jipya la
jarida la Forbes lenye picha yake katika ukurasa wa mbele likitolewa.
Kile ambacho dadake Kim Kardashian West alifanyia upasuaji
ili kuongeza makalio yake, Jenner alifanyia upasuaji midomo yake ili kuongeza
ukubwa wake, Forbes iliandika, ikielezea umaarufu wake.
Mapema wiki hii Jenner-mama ya mtoto mmoja wa kike kwa jina
Stormi alitangaza kuwa atasita kudungwa sindano za kuongeza ukubwa wa midomo
yake , kwa jina Dermal Fillers.
Jenner alikiri katika kipindi kimoja cha Keeping Up With The
Kardashians mwaka 2015 kwamba midomo yake imekuwa kitu ambacho kimekuwa
kikimshusha hadhi hivyobasi angependelea kubadilisha ili kuongeza ukubwa wake.
Baadaye alizindua chapa yake ya vipodozi kwa Jina Kylie
Cosmetics , ambayo ilishirikisha msururu wa bidhaa za midimo.
Upasuaji wake wa midomo ulivumbua mtindo mpya ambao
umewafanya wasichana zaidi kuomba midomo yao kuongezwa ukubwa kulingana na
madaktari wa upasuaji.
Kampuni ya Jenner anayomiliki ina thamani ya $800m,
kulingana na Forbes.
Ameorodheshwa na Forbes katika nafasi ya 27 ya wanawake
waliojitengezea utajiri nchini Marekani, akimpiku Barbra Streisand ($400m),
Beyonce Knowles ($335m) na Taylor Swift ($320m).
Jenner anaelekea kuwa bilionea mapema zaidi ikilinganishwa
na Mark Zuckerberg, mwazilishi wa mtandao wa facebook, ambaye alifanikiwa kuwa
bilionea akiwa na umri wa miaka 23.
Evan Spiegel, mmiliki wa Snapchat, pia alikuwa bilionea
katika miaka yake ya 20, lakini bado haijulikani ni vipi aliafikia hilo.
"Wow. Siamini jarida la Forbes litakuwa na picha
yangu," aliandika katika mtandao wake ulio na wafuasi milioni 110 siku ya
Jumatano.
"Ahsante kwa makala hii na kutambulika. Nimebarikiwa
kufanya kile ninachopenda kila siku. Sikudhania kwamba hili linaweza
kufanyika''.
Tovuti ya Dictionary.com ilituma ujumbe katika twitter
kuhusu habari hiyo ya Forbes:: "kujifanikisha kunaamanisha kufanikiwa
katika maisha bila usaidizi."
Jenner mara ya kwanza alijipatia umaarufu akiwa na umri wa
miaka 10 wakati alipoonekana na familia yake katika kipindi hicho chaKeeping Up
With the Kardashian.
Katika mitandao ya kijamii, watumiaji kadhaa waliikosoa
Forbes kwa kutumia neno ''alijijenga", akidai kwamba wazazi wa Jenner
tayari walikuwa matajiri na maarufu.
Comments
Post a Comment