Featured Post

DK. MNDOLWA AMALIZA ZIARA YAKE KATIKA MIKOA YA KANDA YA ZIWA NA MKOA WA SINGIDA


Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dk. Edmund Mndolwa akipata maelezo kuhusu eneo lenye madini la Jumuiya hiyo lililopo katika Kijiji cha Bigigi, alipokagua eneo hilo akiwa katika ziara ya kikazo mkoani Singida, jana. Anayempa maelezo ni Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Singida Mjini Ali Balo (Wapili kushoto) na kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati Sosthenes Masola. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi na Mjumbe wa NEC- CCM Christina Joramu na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa upande wa Zanzibar Haidar Haji abdallah. Dk. Mndolwa ameagiza uongozi wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Singida kuharakisha kulitafutia leseni na kuliwekea vigingi vya mipaka eneo hilo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa akisalimia baadhi ya viongozi wa Jumuiya hiyo baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Singida, kuanza ziara ya kikazi mkoani humo, jana. 
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa akishiriki kucheza ngoma, iliyokuwa ikitumbuizwa wakati akipokewa kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Singida alipofika kwenye ofisi hiyo kuwanza ziara ya kikazi mkoani humo jana.
 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi Tanzania na Mjumbe wa NEC- CCM Christina Joramu akimtuza msanii wa kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitumbuiza wakati wa mapokezi ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Dk. Edmund Mndolwa katika Ofisi ya CCM mkoa wa Singida jana.
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa na Makamu Mwenyekiti wake upande wa Zanzibar Haidar Haji Abdallah wakisaini vitabu vya wageni katika Ofisi ya CCM mkoa wa Singida, jana.
 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi Tanzania na Mjumbe wa NEC- CCM Christina Joramu akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM mkoa wa Singida, jana.
 Katibu wa CCM mkoa wa Singida Jimson Mhagama akisoma taarifa ya Chama ya mkoa.
 Kamishna Msaidizi wa Madini kanda ya Kati Sosthenes Masola (wapili kulia), akiwa na baadhi ya viongozi na maofisa wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Singida
 Baadhi ya maafisa kutoka Makao Makuu ya Jumuiya ya Wazazi Tanzania wakifuatilia wakati Dk. Mndolwa alipongia katika Ofisi ya CCm mkoa wa Singida kusaini vitabu vya wageni.
 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Singida Mashigani Kija akisoma taarifa ya jumuiya hiyo mbele ya Dk. Mndolwa
 Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dk. Edmund Mndolwa akipata maelezo kuhusu eneo lenye madini la Jumuiya hiyo lililopo katika Kijiji cha Bigigi, alipokagua eneo hilo akiwa katika ziara ya kikazo mkoani Singida, jana. Anayempa maelezo ni Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Singida Mjini Ali Balo.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Comments