Featured Post

TAHLISO YATOA TAMKO KUHUSU WANAFUNZI WANAOTAKA MWIGULU AJIUZULU KWA KIFO CHA AKWILINA


Mwenyekiti wa Tahlisi George Albert  Mnali  wa pili kutoka kulia akizungumza na baraza Kuu la Senate leo  kushoto ni Katibu Mkuu wa Tahliso John Mboya kulia ni Katibu wa Baraza hilo Faidhaa Msangi na kulia ni Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Rais wa Chuo cha Zanzibar University.

Simu:
0767 309 331 / 0658 008 804
Baruapepe:
Anwaniya Posta
MWENYEKITI,
TAHLISO.
P.O.BOX 2920,
DAR ES SALAAM-TANZANIA
JUMUIYA YA TAASISI ZA VYUO VYA ELIMU YA JUU TANZANIA
(TAHLISO)
OFISI YA MWENYEKITI TAHLISO
TAARIFA KWA UMMA
Nduguwaandishiwahabaritunawashukurusanakwakukubaliwitowetuwakujakujumuikapamojanasisi. Leo tarehe 3/3/2018 tumekuta na viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kwa ajili yakujadili changamoto zinazotukabili. Kikao hiki ni cha TAHLISO BarazaKuu (SENATE) kinacho husisha Maraisi wa serikali za wanafunzi wa VyuoVikuunchini.
Tunatambuakwambakunakifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina Akwilini,mwanafunziwachuo cha NIT kilichotokea mwezi wa pili. Tunawashukuruwanafunziwenzetukwautulivumkubwanamshikamanowaliouoneshatangumsibaulipotokea, wakatiwakipindi cha majonzihadikufikiasasa.
TunamshukuruMhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muunganowa Tanzania kwa kuingilia kati suala hili na kuagiza uchunguzi ufanyike na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika na kifo cha AkwilinaAkwilini. 
VileviletunaishukuruWizarayaElimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukaribu waliouonesha katika kipindi chote cha msiba.Tunaomba wanafunzi waendelee kuwa watulivu wakati maagizo yaMh. Raisi yakitekelezwa.
Aidha tunapenda jamiii tambue kuwa TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima Tanzania na sio kikundi kingine chochote kile. 
Vipovikundivingivimejitokezanakutoamatamkombalimbalibaadayakifohikikutokea, vikundivinginevikaendambali Zaidi kwakuwataka baadhiya watendajiwa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo yaNdani kujiuzulu jambo ambalo linaashiria vikundi hivyo kuongozwa ama kutumika namakundiyakisiasa, haiwezekani kutaka watendajiwa Serikali wajiuzulu wakati uchunguzi bado unafanyika na matokeoya uchunguzi huo bado hayajatoka.
 Sehemu ya Marais wa Vyuo Vikuu nchini wakiwa kwenye mkutano huo
Jambo la kusikitisha Zaidi kuna baadhi ya vikundi vimejitangaza kwamba vinaungwa mkono na Maraisi waVyuoVikuu jambo ambalo sio la kweli, Marais wote waVyuo Vikuu tuko hapa Dodoma tunaendelea na vikao vyetu vya kujadili changamoto zinazowakabili wanafunziwa VyuoVikuu.
Tunatoa wito kwa vikundi vyote vinavyojihusisha nakutumia mwamvuliwa Marais waVyuoVikuu kama kinga yao ili kuu hadaaUmma kwamba wanaungwa Mkono, vikundi hivyo viache tabia hiyo vinginevyo tutawachukulia hatua za kinidhamu.
TAHLISO tunasubirimatokeoya Uchunguzi unaofanyika juu ya kifo cha Akwilina na tunaimani wahusika wote watachukuliwa hatua kali zakisheria. 
Tunawaombawanafunzi wote tuendelee kuwa watulivu wakati tukisubiri matokeo hayo na kujiepusha na maandamano na vitendo vyovyot e vitakavyo sababisha uvunjifu wa Amani nakuleta mgawanyo miongoni mwawanafunzi.
Hata hivyo namna bora yakufikisha hoja nikutumia njia ya majadiliano kama wasomi badala ya kutumia nguvu ama maandamano kwakutofuata taratibu na madhara yake ni kusababisha vuruguzi sizotakiwa na hatimaye kuhatarisha usalama na hivyo kuathiri jamii kwaujumla wake.
Vurugu zozote zitokanazo kwakutozingatia taratibu zinaweza kudhorotesha shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Uchumiwa Taifa letu. Vile vile zinapoteza mvuto kwawawekezaji wanje na wandani, ikiwemo shughuli za utalii nchini ambazo zinachangia pato la Taifa letu.
Athariza Vurugu na kukosekana kwa amani zipo wazi natunaziona kwa nchi nyingine zikiwemo baadhi ya nchi jirani zetu ambao wamekua wakimbizi nchini kwetu kila siku.
Tunaona kuwa kama wanataaluma tunajukumu kubwa la kuelimisha jamii na kuwamfano bora wakutumia njia za majadiliano katika kujenga hoja zetu ilizitatuliwe kuliko kutumia njia ya maandamano au vurugu zisizo na ulazimawowote.
Taasisi hii ndio yenye dhamana ya kutetea nakusimamia maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo na vyuovikuu Tanzania na si vinginevyo.
………………………………….
GEORGE ALBERT MNALI
MWENYEKITI TAHLISO

Comments