Featured Post

RC MRISHO GAMBO AWAPIGA TAFU WAJASIRIMALI WANAWAKE 600 KWA KUWAPA MIKOPO


Na Richard MwangulubeOfisi ya Waziri Mkuu imeupongeza Uongozi wa Serikali wa Mkoa wa Arusha kwa kuwa Wabunifu katika kutekeleza kwa Vitendo maelekezo ya Serikali ya kuyawezesha makundi maalum.
Pongezi hizo zimetolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mjini Arusha  Jenista Mhagama (MB) alipokabidhi mikopo kwa Wanawake 600.


Mikopo hiyo imetolewa na Serikali ya Mkoa wa Arusha kupitia mradi maalum uliobuniwa na kuanzishwa na Serikali ya Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo katika Mkoa huo kwa ajili ya kuyawezesha makundi maalum wakiwemo Wajasirimali wadogo wadogo wa ngazi ya chini.
Waziri Mhagama amesema Viongozi wa Mkoa wa Arusha chini ya Mkuu wa Mkoa huo Mrisho Meshaki Gambo na Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) pamoja na Mkuu wa Wilaya  ya Arusha Gabriel Dagarro wanastahili pongezi kutokana na kuwa  wabunifu kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali  wadogo wadogo.
Waziri Mhagama amesisitiza kwamba Viongozi hawa   wamestahili pongezi hizo kutokana na kutafsiri kwa Vitendo maelekezo ya Rais Dkt John POMBE Joseph Magufuli ya hapa kazi tu.
Amesisitiza kwamba Viongozi hawa pia  wameisaidia Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli ya kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi katika jamii kwa kuwasaidia  wananchi wanyonge wa ngazi ya chini kuwawezesha kiuchumi.
Waziri Mhagama amesemaMkoa wa Arusha umekuwa Mkoa wa mfano nchini katika kutekeleza  maelekezo ya Rais Magufuli kwa kushirikisha Wadau mbalimbali wa maendeleo wakiongozwa na Kamanda wa Mkoa Kijana mchapa Kazi na Jemedari Mkuu wa Mkoa huo Mrisho Meshack Gambo katika mapambano haya.
Waziri huyo Ofisi ya Waziri Mkuu amefafanua kuwa  Viongozi hawa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo wameongoza safari ndefu ya mabadiliko katika Jamii ya Wananchi wa Mkoa wa Arusha.
Ujenzi wa uchumi na  maendeleo ya Mkoa wa Arushana Tanzania unachangiwa na ushiriki kikamilifu wa Wananchi wote  bila kujali Itikadi zao za Kisiasa ama dini.Amesisitiza Waziri Mhagama.
Umoja uliopo katika Mkoa wa Arusha baina ya Chama cha Mapinduzi,Serikali na Wananchi umejenga nguvu ya pamoja katika kufikia mafanikio yanayotarajiwa na Serikali ya awamu ya tano.Amesisitiza Waziri Mhagama.
Waziri huyo  amesema kutokana na umoja uliopo hivi sasa katika Mkoa wa Arusha  Watanzania katika kona zote  wanshuhudia  Makundi yaliyosahaulika  wakiwemo Vijana (boda boda, Walemavu na Wanawake) Wanawezeshwa  mikopo hivi sasa kupitia mradi huu maalum uliobuniwa na Serikali ya Mkoa,Wilaya, Jiji l Arusha n Washirika mbalimbali wa Maendeleo katika Mkoa huu.
Hata hivyo Waziri Mhagama amesisitiza kuwa mafanikio  yanayoonekana  hivi sasa yanatokana na hali ya Utulivu, amani na hali ya Usalama uliosimamiwa kikamilifu na Viongozi wa Mkoa.
Amesema   siku ya nyuma  Vijana na Wanawake  walitumika   na baadhi ya Wanasiasa katika maandamano na vurugu  hususani katika Jiji hili la Arusha mambo ambayo hivi sasa hayapo tena.
Wananchi waliishi maisha ya hofu, amani katika Mkoa huu ilitoweka kulikuwa hakuna utulivu, mali ziliharibiwa na baadhi ya watu walipoteza maisha mambo ambayo hivi sasa hayapo kutokana na kuwepo na Viongozi imara na wenye msimamo.
Waziri Mhagama amesisitiza kuwa Wanawake ndiyo nguzo muhimu katika masuala ya maendeleo na ujenzi wa uchumi wa taifa hili.
Amesifu  Viongozi wa Mkoa wa Arusha wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Gambo kwa kuguswa  na maisha ya  Wananchi wa ngazi ya chini.
Amesisitiza  kwamba Serikali ya awamu ya tano itahakikisha Wananchi wote wananufaika na  matunda yanayopatikana  bila kujali Itikadi zao za Kisiasa.
Amesema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria  kufanya mageuzi na kutafsiri  kwa Vitendo Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 kwa lengo la kupunguza kwa kiasi kikubwa kiwango cha umaskini kwa kukuza uchumi wa wananchi kupitia mpango wa uwezeshaji wananchi  Kiuchumi.
Waziri Mhagama amesisitiza kuwa mikopo inayolewa na mradi huu maalum na Mkoa wa Arusha imelenga kuleta mabadiliko makubwa katika Jamii.
Amewambia Wanawake hao kutoka Kata zote 25 za Jiji la Arusha Mikopo hii inayotolewa na Serikali ya Mkoa itumike kufanya mageuzi ya Kiuchumi katika familia zenu.
Amewataka Wanawake hao kutumia Mikopo hiyo kwa nidhamu,Uaminifu na uadilifu wa hali ya juu  na kutadharisha kuwa mikopo hii isitumike akwa shughuli za anasa.
Hivyo amewataka Wanawake waliobahatika kupata mikopo hiyo   waonyeshe mabadiliko katika Jamii.Hata hivyo amesisitiza umuhimu wa Wanawake hao kujenga  tabia ya kurejesha mikopo hiyo haraka ili  makundi mengi yaweze kunufaika.
Waziri Mhagama amesisitiza kwamba Wanawake  ni Jeshi kubwa  katika Jamii linaloongoza mapambano ya maendeleo na Kiuchumi katika nchi.
Hata hivyo changamoto kubwa inayowakabili wanawake ni uwezo wa kujitengenezea ajira kwa njia ya biashara ndogondogo.Hivyo mradi huu ni Mkombozi mkuu kwa Wanawake wa Mkoa wa Arusha.
Mikopo hii haina dhamana wala riba hivyo  itumike ipasavya katika kuwakomboa wanawake wa Mkoa wa Arusha .Amesisitiza Waziri Mhagama.
Amesema utafiti unaonyesha kuwa ukosefu wa ajira hapa Tanzania ni asilimia 12.3 na kundi kubwa linalokabiliwa na kukosa ajira ni Wanawake.
Hata hivyo Waziri Mhagama ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma amesisitiza kwamba Mikopo hii  siyo Zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa huo Mrisho Gambo bali ni moja ya Mkakati  wa Serikali ya Mkoa huo  wa kuwakomboa Wanawake,Vijana na Walemavu Kiuchumi.
Serikali ya awamu ya tano inafahamu kuwa kazi iliyopo mbele ya Serikali bado ni kubwa kutokana na makundi mengi ngazi ya chini bado yanakabiliwa na changamoto  nyingi.
Hata hivyo Serikali imeanzisha mifuko 19 inayosimamiwa na Ofisi  ya Waziri Mkuu kwa ajili ya kutoa mikopo kwa ajili ya kuwawezesha wanawake, Vijana na makundi maalum wakiwemo walemavu.
Kwa upande wake Naibu Waziri katika  Ofisi hiyo Antony Mavunde amesema  ushindi wa  Chama cha Mapinduzi katika chauzi mbalimbali unatokana  mchango mkubwa unaotolewa na Jeshi kubwa la Wanawake.
Mavunde amesisitiza  kwamba Wanawake wanao mchango  mkubwa katika masuala ya maendeleo na ukuaji wa uchumi wa Taifa la Tanzania.
Aidha Naibu Waziri Mavunde amesisitiza kamba lengo la Serikali ya awamu ya tano ni kuyaweaeaha  makundi  mbalimbali kiuchumi bila kujali Itikadi zao za Kisiasa.
Mbunge wa Viti Malum CCM Mkoa wa Arusha Catherine  Magige amewataka Wanawake waliobahatika kupata mikopo hiyo waepuke kutumia  fedha hizo kwa ajili ya kununua Vitenge.
Magige amesema  akina mama hawana uwezo kiuchumi wa kukopa katika taasisi za fedha ambazo zinatoza riba kubwa  na dhama.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Meshack Gambo ameeleza kwamba  Serikali Mkoani humo itahakikisha Arusha inaendelea kuwa tulivu na Watu wanaisi kwa amani bila vurugu.
Serikali  ya Mkoa imejipanga kuendelea kuwezesha makundi mbalimbali ili makundi hayo yajikomboe kiuchumi.
Amesisitiza kuwa mikopo hii itakuwa imetengeza ajira nyingi kwa makundi hayo na watu wengi.hivyo fedha  iliyotolewa  leo kama mkopo itumike na wanawake hao kama mbegu kwa lengo la kuwabadilisha maisha yao.
Gambo ameeleza kwamba Mkoa wa Arusha kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ulitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni moja kwa makundi mbalimbali katika Mkoa  huo kwa lengo la kubadilisha maisha na ustawi wa Jamii.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Arusha ameeleza kuwa kutokana na Wananchi wengi hasa wa kada ya chini na wajasiriamali wadogo wadogo kushindwa kupata  mikopo katika taasisi za fedha kutokana  taasisi hizo kuw ana masharti magumu na riba kubwa  Mkoa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ulibuni mradi maalum kwa ajili ya kuwawezesha  wajasirimali Kiuchumi.
Amesema awali mradi huo ulikusanya fedha zaidi ya milioni 400.2. Fedha ambazo zilitumika kutoa mikopo kwa  Vijana waendesha boda boda 200 ambapo asilimia  75 ya mikopo hiyo imerejeshwa na Vijana hao.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Arusha amesisitiza kuwa Serikali Mkoani humo itaendelea kujenga mazingira rafiki na mazuri  kwa  ajili ya kuwawezesha wajasiriamli wadogo kuendesha biashara zao bila bugudha.
Gambo amesisitiza kuwa mikopo hii haingalii  mkopaji anatoka chama gani ama dini gani ama kabila gani bali ni kwa ajili ya Wajasiriamli wote wadogo.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Arusha amesisitiza kuwa Mikopo hii imelenga kuwakwamua Kiuchumi Wajasiliamali wadogo na kwamba mikopo hii haina riba  wala dhamana.
Gambo  amesisitiza kuwa suala la maendeleo na ujenzi wa uchumi wan chi halina  Itikadi za Kisiasa.hivyo amewataka Viongozi mbalimbali wa Vyama vya Siasa katika Mkoa huo kushirikiana na Serikali katika masuala mbalimbali ya Maendeleo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Dagarro amesisitiza kuwa Wanawake  ndio wajenzi wakuu wa uchumi na maendeleo ya Tanzania.
Aidha Mkuu wa Mkoa Gambo aliwachimba mkwara  wanasiasa katika Jiji hilo wanaodhani mradi huu hautafanikiwa na kueleza kuwa wao  walie tu.
Amesema alipotoa mkopo kwa vijana waendesha boda boda wanasiasa hao walisema mradi huo utakwama na hivi sasa mradi huo umeonyesha mafanikio makubwa  vijana hao wamerejesha mikopo kwa asilimia 75 na bado waliobakia wanaendelea kurejesha alisisitiza Gambo.
Gambo alisema wanasiasa hao hivi sasa wamekwama hawana hoja  ya kuongea mbele ya wananchi na amesisitiza kuwa  hakuna  maandamano wala vurugu za kisiasa  katika Jiji hilo wala Mkoa wa Arusha  kwa vile viongozi tumejipanga.
Dagarro pia amesema Wanawake ndiyo washiriki wakuu katika masuala ya uzaalishaji katika sekta ya Kilimo na Sekta nyingine.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya  amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha  elimu ya biashara kuanzia ngazi ya mtaa, Kata na tarafa kwa Wajasiriamali wadogo ili kuwawezesha kuendesha biashara zao kwa tija na ufanisi zaidi.
Mkuu huyo wa Wilaya ya Arusha amewahakikishia akina  mama hao kwamba  wataendesha biashara zao bila kubugudhiwa bali kwa amani na utlivu kwani Serikali haitaruhusu vurugu za kutimua timua wajasiriamali wadogo mitaani.
Kwa upande wake Mke wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mwalimu  Margreth Muro Gambo amewataka Wanawake hao kutumia mikopo waliyopata  kuwa chachu ya kuwaleta mageuzi kwa lengo la kuwakwamua kiuchimi.
Mwalimu Margreth Muro Gambo pia amesema mikopo hiyo itumike kujenga amani na utulivu katika familia.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama  Kinachosimamia  masuala ya Utalii Mkoani Arusha (TATO), Willy Chamburo amesema Mkoa wa Arusha ni Mkoa wa Utalii ambapo unapokea asilimia 80 ya Watalii wote wanaotembelea Tanzania.
Amesisitiza kuwa amani na utulivu vikiendelea kuwepo hali ya utalii itanedelea kukua.hivyo wajasiriamali  wadogo  hawa ni muhimu sana katika kukuza sekta ya Utalii Mkoani Arusha.
Kutokana na Kutambusa hilo Mwenyekiti huyo wa TATO alitoa Shilingi milioni 20 kama mchango kwa ajiili ya kuwapatia Wengine 100 mikopo.
Mbali na Mkopo huo pia Chamburo alitoa Vitanda 10 kwa ajili  Kituo cha Afya Murriet kwa ajili ya akina mama wanaojifungua.
Pia alitoa Vitanda 30 kwa ajili ya Kituo hicho kwa  ajiri ya akina mama wanaolazwa katika hospitali hiyo na Kampuni ya Tanzanite ilitoa  shilingi milioni nane(mil 8) kuunga mkono  juhudi za Chamburo.
Pia Kampuni nyingine ya Utalii ilitoa Gari aina ya Ambulance kwa ajili ya Kituo hicho cha Afya cha Murriet.
Dkt Phillemon Mollel  ambaye  ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya MONABAN akizungumza katika hafla hiyo alisema Mkoa wa Arusha umeanza kutekeleza kwa mafanikio  dhana ya Rasi Dkt John Pombe Joseph Magufuli ya hapa Kazi tu.
Dkt Mollell amesema Arusha kama Mkoa umejikita katika kufanikisha  maelekezo mbalimbali ya RaisDkt Magufuli yakiwemo maelekezo ya Dhana ya Viwanda.
Dkt Mollel ambaye ni mmoja wa Makampuni yake katika kuanzisha mradi huo maalum wa kuwawezesha wanawake Kiuchumi katika Mkoa wa Arusha.

Amesisitiza kuwa  hivi sasa Mkoa huo umejikita  na kujipanga kuhakikisha Wajasirimali wadogo wanawezeshwa Kiuchumi kwa kupatiwa Mikopo  kupitia mradi huo Maalum ulioanzishwa na Mkoa.
Dkt Mollel amesisitiza kwamba lengo la mradi huu kuanzishwa na Mkoa ni kuwainua Wanawake  wa Mkoa huo hususani katika Jiji la Arusha Kiuchumi na kuwaodoa katika matatizo ya kukopa  fedha kutoka  taasisi za fedha ambazo hutoza riba kubwa.
Pia lengo la mradi huu ni kuwasaidia wanawake na familia zao kuboresha maisha yao ili waondokane na Umaskini unaowakabili.amesisitiza Dkt Phillemon Mollel.
Mradi huu unatekelezwa na Mkoa kutokana na kuwepo na Sera Safi, AMani na Utulivu katika Jiji la Arusha n mkoa Mzima.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha (RAS) Richard Kwitega ambaye ndiye msimamizi Mkuu wa mradi huu amesisitiza kuwa nafasi ya akina mama katika uhai wa Mwandamu ndiyo tegemeo kubwa kuanzia  motto akiwa tumboni hadi makuzi yake yote.
Kwitega amesema Wanawake ndiyo wanaolea familia katika masuala mbalimbali ya Kijamii.hivyo ndiyo tegemeo kuu katika maisha ya Mwandamu.
Hivyo jamii kamwe haitaacha kuwaenzi Wanawake kutokana na umuhimu wao katika Jamii .Amesisitiza Richard Kwitega Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha.
RAS Kwitega amesisitza kuwa Wanawake ndio wanaoingarisha familia na taifa katika masuala mbalimbali  huku  akiwataja akina Mama Anna Abdallah,Anna Makinda na Getrude Mongela kuwa ni miongoni mwa Wanawake Viongozi walioingarisha Tanzania katika Mataifa ya nje
Wajasiriamali hao kila mmoja alipata mkopo wa shilingi laki mbili(200,000) ambazo kila mmoja aliingizwa katika akauti yake zilizoopo benki ya NMB Arusha.
Fedha hizo ni kati ya  shilingi milioni 400.2 ambazo ni mtaji  katika mradi huo maalum ulioanzishwa na Serikali ya Mkoa wa Arusha kwa  ajili ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo  wanaoendesha biashara ndogondogo katika Jiji la Arusha.
Kwitega amesisitiza kuanzishwa kwa mradi huu maalum na serikali ya Mkoa huo imelenga  kujaribu kutatua kero na matatizo yanayowakabili wananchi wa kada ya chini wanaoendesha biashara ndogondogo katika Mkoa huo.
RAS Kwitega  amesema mradi huu haueneshwi Kisiasa kama ambavyo baadhi ya wanasiasa katika Wilaya hivyo wanavyodhani bali ni kutekeleza  maelekezo ya JPM.
Katibu Tawala huyo wa Mkoa wa Arusha amesisitiza kuwa  Serikali ya Mkoa huo itatekeleza  maelekezo yote ya Rais DKT Magufuli ya kuhakikisha Wananchi katika kada zote wanaondokana na  kero  zinazo wakabili bila ubaguzi wa kiitikadi za kisiasa  kwa kutambua kuwa Serikali iliyopo madarakani ni kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wote wa Mkoa huo

Comments