Featured Post

MAMLAKA YA HIFADHI NGORONGORO NA TATO WAAZIMIA KUSHIRIKIANA KUKUZA UTALII NCHINI

Katibu Mtendaji wa TATO, Siriri Akko akichangia mada katika kikao kazi hicho juu ya maazimio ya kuondoa kero na changamoto wakutanazo watoa huduma za utalii nchini.


Katibu Mtendaji wa TATO, Siriri Akko akiainisha baadhi ya changamoto wanazokutana nazo wanachama wa TATO katika hifadhi ya Ngorongoro na kuomba uongozi wa NCAA kuwaondolea kero hizo ili kukuza utalii nchini na wanaomsikiliza kwa makini ni naibu mhifadhi wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Assangye Bangu nabaadhi ya  viongozi wa NCAA kutoka idara ya uhasibu na teknolojia ya mawasiliano 


naibu mhifadhi wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Assangye Bangu kushoto akizungumza na mwanachama wa chama cha mawakala wa utalii mara baada ya kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano katika hotel ya NEW ARUSHA.

Add caption

Baadhi ya wadau na wanachama wa cham cha mawakala wa utalii yaani Tanzania Association of Tour Operators wakimsikiliza kwa makini naibu mhifadhi wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Assangye Bangu juu ya suluhisho la changamoto zilizopo geti kuu la kuingia hifadhi ya Ngorongoro


Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) na Chama cha Mawakala wa Utalii(TATO), wamefikia makubaliano ya  kuondoa vikwazo baina yao na hivyo kushirikiana katika kukuza utalii hapa nchini.

Makubaliano hayo, yalifikiwa jana katika kikao  kazi kilichofanyika Arusha katika hotel ya New Arusha,   baina  viongozi NCAA,TATO na  Kampuni za Utalii  ambazo hivi karibuni zilitajwa kuwa huenda zingezuiwa kuingiza watalii katika hifadhi ya Ngorongoro.
Akizungumza katika kikao hicho, Naibu mhifadhi wa NCAA anayeshughulikia Huduma za Shirika  Asangye Bangu alisema,NCAA imejipanga kuboresha huduma kwa watalii na kuondoa changamoto zinazowakabili wenye makampuni ya Utalii.

"Kikao chetu kimekwenda vizuri, NCAA tutaendelea kuboresha mifumo ya malipo, kuboresha mawasiliano baina yetu na mawakala wa utalii lakini pia kutatua changamoto kadhaa, ikiwepo barabara ndani ya hifadhi"alisema

Alisema katika kukabiliana na kero ya barabara, NCAA inatarajiwa mwezi wa nane mwaka huu, kuanza ujenzi wa barabara ya kutoka geti la kuingia Ngorongoro hadi geti la kuingia Serengeti yenye urefu wa kilomita 83 kwa kuweka tabaka gumu juu.

"hii ni kero ya muda mrefu ya makampuni ya Utalii lakini sasa Shirika la umoja wa mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni(UNESCO)limetukubalia kuijenga barabara hii na ikikamilika tunaimani barabara itadumu kwa zaidi ya miaka 40"alisema

Awali Katibu Mtendaji wa TATO, Siriri Akko alisema, katika siku za karibuni kuliibuka taarifa za kuwachanganya baadhi ya wanachama wao juu ya kuzuiwa kuingia ngorongoro kupeleka watalii.
Hata hivyo, alisema baada ya kupata maelezo kutoka NCAA wamefikia makubaliano ambayo lengo lake ni kuboresha sekta ya utalii nchini na pia kuondoa changamoto zinazowakabili.
"kikao chetu kimekwenda vizuri na ile hofu ya kampuni kuzuiwa sasa haipo na tunaimani kampuni zote zitafuata sheria na taratibu za kufanya biashara ya utalii hapa nchini"alisema

Akizungumza katika kikao hicho,Mkurugenzi wa kampuni ya Utalii wa Shidolya, Lazaro Mafie alisema ni muhimu kuwepo na mawasiliano ya mara kwa mara baina ya NCAA na makampuni ya utalii ili kutatua kero.
Mafie alisema wao kama wamiliki wa makampuni ya Utalii, wateja wao ni watalii sawa na NCAA ambayo uwepo wao unategemea watalii hivyo ni lazima kuwepo na mawasiliano mazuri baina yao.
"kuna changamoto kadhaa ambazo tunakabiliana nazo lakini tunaimani sasa zitafanyiwa kazi ili kuboresha sekta ya utalii hapa nchini"alisema.

Comments