Featured Post

EXIM BENKI YATOA MSAADA WA VITANDA 500 NA MAGODORO KWENYE HOSPITALI ZA RUFAA KWENYE MIKOA 13 NCHINI




Mkuu wa Idara ya Masoko wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu kushoto akimkabidhi sehemu ya vitanda 40 magodoro 40 na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Clemence Marcel ikiwa mpango wao kupitia kampeni ya benki ya exim ya miaka 20 ya kujali jamii wa pili kulia ni Kaimu Mganga Mfawidhi wa
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Abdallah kushoto ni Meneja wa Benki ya Exim Mkoa wa Tanga, Emanuel Mwamkinga.



Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Dkt Clemence Marcel akiwa na Mkuu wa Idara ya Masoko wa Benki ya Exim Stanley Kafu wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi vitanda  na magodoro 40 kwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo.
Mkuu wa Idara ya Masoko wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu akizungumza wakati wa halfa hiyo  kulia ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Dkt Clemence Marcel kushoto ni Meneja wa Exim Benki Mkoa wa Tanga Emanuel Mwamkinga
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Dkt Clemence Marcel akizungumza katika halfa hiyo kulia ni Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga  Bombo Mohamed Abdallah kushoto ni Mkuu wa Idara ya Masoko ya Benki ya Exim Stanley Kafu



Muuguzi mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo Beatrice Rimoy akizungumza kuishukuru benki ya Exim kwa kuwapatia msaada huo wa vitanda na magodoro 40


Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Mohamed Abdallah akizungumza wakati wa halfa hiyo ya makabidhiano ya vitanda na magodoro 40 iliyofanyika katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo
 Sehemu ya vitanda na magodoro vilivyotolewa

 Sehemu ya watumishi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wakifuatilia matukio hayo
BENKI ya Exim Tanzania imetoa msaada wa vitanda 500 na magodoro kwa hospitali za rufaa kwenye mikoa 13 hapa nchini ikiwa ni sehemu ya kampeni yake yenye lengo la kusheherekea miaka 20 ya kuitumikia jamii.

Hayo yalibainishwa leo na Mkuu wa Idara ya Masoko wa Benki hiyo, Stanley Kafu wakati akikabidhi vitanda na magodoro 40 kwa ajili ya hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo inayolengo la kusaidia  upungufu wa vitanda katika hospitali nchini.

Alisema ili kukabiliana na hali hiyo ndio maana waliamua kutoa msaada ili kuweza kusaidia tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa katika kukabiliana na uhaba unaosumbua Taifa.

“Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma mwezi wa Agosti mwaka jana,kwa kuzindua kampeni ya mwaka mzima uuitwao ‘Miaka 20 ya kujali jamii”ambao benki hiyo itawekeza katika sekta ya Afya Tanzania…Sisi kama Benki ya Kitanzania iliyoanzishwa mwaka wa 1997 hivyo benki hiyo inafafanua mafanikio yake jinsi inavyoleta mabadiliko kwa wateja na jamii kwa ujumla “Alisema.

“Hospitali ya rufaa mkoa wa Tanga ni hospitali ya saba kupokea mchango huu, baada ya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mbeya mwezi uliopita, Hospitali ya Mount Meru mkoani Arusha mwezi Desemba, Hospitali ya rufaa Dodoma mwezi Novemba, Hospitali ya rufaa Ligula mkoani Mtwara mwezi Octoba,Hospitali ya Mnazi mmoja Unguja Visiwani Zanzibar mwezi Septemba na hospitali ya rufaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam mwezi wa nane mwaka huu”Alisema

Katika halfa hiyo tukio hilo la makabidhiano ya msaada huo yalifanyika kwenye ukumbi wa mikutano na mgeni rasmi alikuwa ni Afisa Matibabu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Clemence Marcel pamoja na Kaimu Mganga mkuu wa hospitali Dkt Mohamed Abdallah.

“Katika kipindi cha miaka 20 benki imetambua umuhimu wa jamii zinazozunguka eneo la biashara yetu na ndio maana shughuli za kijamii ni muhimu sana kwa kwa benki ya Exim…..Tunaamini kwamba tuna nafasi kubwa katika kuchangia mabadiliko chanya katika sekta mbalimbali kwa jamii zetu “Alisema

“Lakini pia benki iliamua kusheherekea miaka hiyo kwa kusaidia jamii kwa njia ya kampeni inayoitwa “Miaka 20 ya kujali Jamii” kuonyesha jinsi tunavyowashukuru kwani benki hiyo imekwisha kutoa vitanda na magodoro ya hospitali kwa hospitali nchini kote kila mwezi kwa mwaka mzima”Alisema

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Dkt Clemence Marcel aliipongeza Exim benki kwa juhudi zake za kusaidia kukabiliana na upungufu wa vitanda kwenye hospitali ambao umekuwa ukijitokeza mara kwa mara.

Alisema upungufu wa vitanda katika hospitali umekuwa ni changamoto kubwa hivyo kukabidhiwa vitanda 40 na magodoro utasaidia sana kupunguza vikwazo vya namna hiyo kwa jamii.

Benki ya Exim inatambuliwa kama Mwajiri bora wa kitanzania mwaka 2017 na taasisi ya The Banker ya Afrika mashariki na sasa inasheherekea miaka 20 ya mafanikio,ukuaji na kuwa kiongozi katika kuingia katika masoko mapya barani Afrika.

“Exim Benki iliyoanzishwa mwaka 1997 na imetanua soko lake kwa kufungua kampuni tanzu katika nchi za Comorro(2007),Djibouti(2010) na Uganda (2016) lakini pia benki hiyo inajuivunia kuwa benki ya kwanza kubwa ya kitanzania nay a kwanza kuingia katika masoko ya nje ya nchi.(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

Comments