Featured Post

DK MWAJELWA AWAPONGEZA WAKULIMA WA CHAI NA PARACHICHI MKOA WA NJOMBE

NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akisalimiana na sehemu ya wakulima wa chai alipowasili kwenye kijiji cha Lwangu Wilaya ya njombe mkoani Njombe kwa ziara ya kikazi hivi karibuni. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Ruth Msafiri. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs)
Sehemu ya wakulima wa chai wakimsikiliza Naibu Waziri wa Kilimo, Dk. Mary Mwanjelwa alipozungumza nao.

Sehemu ya wakulima wa chai wakikusanya zao hilo baada ya kutoka kuvuna wakati Naibu Waziri wa Kilimo, Dk. Mary Mwanjelwa alipofanya ziara na kuzungumza nao.


NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akiongea na wakulima wa chai alipotembelea kijiji cha Lwangu Mkoa wa Njombe hivi karibuni.  

Sehemu ya wakulima wa chai wakimpongeza Naibu Waziri wa Kilimo, Dk. Mary Mwanjelwa alipofanya nao mazungumzo wakati wa ziara  yake kwa wakulima hao. 

Naibu Waziri wa Kilimo, Dk. Mary Mwanjelwa akimwagiza Meneja Mkuu wa Njombe Outgrowers Services Company (NOSC), Fibert Kavia (kushoto) kuhakikisha risiti zao zinaonyesha kiasi cha fedha mkulima wa chai anachotakiwa kulipwa baada ya kupima bidhaa hiyo wakati kuuza zao hilo kwa kampuni hiyo. Wanaosikiliza (wa pili kushoto) ni Mkulima wa chai iliyopimwa, Juliana Casian na Karani wa NOSC, Flora Sanga. 
Naibu Waziri wa Kilimo, Dk. Mary Mwanjelwa (wa pili kushoto) akiangali kitalu cha mbegu za kupandikizwa za maparachichi alipofanya ziara na kuzungumza na wakulima wa zao hilo katika kijiji cha Nundu, Wilaya ya Njombe Mkoani Njombe. Kushoto ni Afisa Kilimo wa Wakulima wa zao hilo, Damasi Kasalala, Mbunge wa jimbo la Njombe, Mhe. Edward Mwalongo na ujumbe wa viongozi wa serikali.  

Naibu Waziri wa Kilimo, Dk. Mary Mwanjelwa akipata maelezo ya mche uliopandikizwa wa parachichi kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey Kirenga (kulia) na Afisa Kilimo, Damasi Kasalala alipofanya ziara na kuzungumza nao wakulima wa zao hilo. Kushoto ni Mbunge wa jimbo la Njombe, Mhe. Edward Mwalongo.

Wataalamu wa kuandaa mbegu za parachichi, Henry Mwepel (kulia), na Lugano Mwalusi wakifanya upandikizaji wa miche ya parachichi kutoka ule wa asili kuwa wa kisasa katika kitalu maalumu cha uzalishali wa zao.

NAIBU Waziri wa Kilimo, Dk Mary Mwanjelwa akilakiwa na  wakulima wa viazi mviringo (Irish potatoes) kwenye kijiji cha Lusitu, Wilaya ya Njombe mkoani Njombe, alipowatembelea na kuzungumza nao kujua changamoto zao na kutoa ushauri wake kukabiliana nazo. Pamoja naye ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Ruth Msafiri.

Wakulima wa viazi mviringo (Irish potatoes) kwenye kijiji cha Lusitu, Wilaya ya Njombe mkoani Njombe, wakimpokea kwa furaha Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Dk. Mary Mwanjelwa.


Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Dk. Mary Mwanjelwa akiwasabahi wakulima wa viazi mviringo (Irish potatoes) kwenye kijiji cha Lusitu, Wilaya ya Njombe mkoani Njombe alifanya ziara mkoani humo.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Dk. Mary Mwanjelwa (kulia) Mbunge wa jimbo la Njombe, Mhe. Edward Mwalongo (wa pili kulia) na Afisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Geoffrey Kirenga wakifuatilia jambo Mhe. Mwanjelwa alipozungumza na wakulima hao.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Dk. Mary Mwanjelwa (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa mradi wa ujenzi wa kituo cha kukusanya, kuchambua, kufungasha na kuuzia viazi mviringo kijiji cha Lusitu, namna bora ya uzalishaji wa viazi wakati Mhe. Mwanjelwa alipofanya ziara na kufanya nao mazungumzo. 

Comments