Featured Post

WATANZANIA TISA KUCHEZESHA NA KUSIMAMIA LIGI YA MABINGWA NA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

Mwamuzi Mfaume Ali Nassoro
 Waamuzi nane kutoka Tanzania wameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF kuchezesha mechi za Ligi ya Mabingwa Africa na Kombe la Shirikisho.

Waamuzi wanne wameteuliwa kuchezesha mchezo wa Ligi ya mabingwa kati ya Lydia Ludic Burundi Academic ya Burundi na Rayon Sports ya Rwanda.
Mwamuzi Mfaume Ali Nassoro atakuwa mwamuzi wa kati akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Frank John Komba wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa Soud Idd Lila na mwamuzi wa akiba Israel Omusingi Njunwa Mujuni huku kamishna wa mechi hiyo akitokea nchini Zimbabwe Gladmore Muzambi.
Mchezo huo utachezwa kati ya Februari 20 na 21, 2018 nchini Burundi.
Waamuzi wengine wanne wa Tanzania watachezesha mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya Masters Security Services FC ya Malawi dhidi ya Atletico Petroleos de Luanda ya Angola nutakaochezwa kati ya Febriari 20 na 21,2018 nchini Malawi.
Elly Ally Sasii atakuwa mwamuzi wa katikati kwenye mchezo huo akisaidiwa na Mwamuzi msaidizi namba moja Salim Mkono Mohamed na mwamuzi msaidizi namba mbili Ferdinand Chacha na mwamuzi wa akiba Alphonce Mwandembwa Emmanuel wakati kamishna wa mchezo huo atatokea Ethiopia Luleseged Gegashaw Asfaw.
Wakati huo huo Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF limemteua Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Ndugu Michael Richard Wambura kuwa Kamishna wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Africa kati ya Bidvest Wits ya Africa Kusini na Pamplemousses SC ya Mauritius utakaochezwa Februari 10, 2018 kwenye uwanja wa Johannesburg-Bidvest.
Wambura atasimamia mchezo huo utakaochezeshwa na waamuzi kutokea Seychelles.
Mwamuzi wa kati Nelson Emile Fred akisaidiwa na Hensley Danny Petrousse na James Fedrick Emile wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Allister Barra
Huu unakuwa ni muendelezo kwa CAF kuteua viongozi mbalimbali wa Tanzania kuwa makamishna wa mechi zinazoandaliwa na Shirikisho hilo.
Tayari Rais wa TFF Ndugu Wallace Karia licha ya kuteuliwa kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya maandalizi ya fainali za Africa kwa wachezaji wanaocheza ndani CHAN pia ameteuliwa mara mbili kuwa Kamishna wa mechi ya ufunguzi ya CHAN wenyeji Morocco walipocheza dhidi ya Mauritania Februari 13, 2018 na mchezo mwingine uliowakutanisha Namibia na Zambia uliochezwa Februari 22, 2018
Aidha mjumbe mwingine wa kamati ya utendaji Ahmed Iddi Mgoyi naye ameteuliwa na CAF kuwa kamishna wa mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya AFC Leopards ya Kenya dhidi ya Fosa Juniors ya Madagascar mchezo utakaochezwa kati ya Februari 9,10 na 11,2018 nchini Kenya.

Comments