Featured Post

ASILIMIA 62 YA MRADI WA DAWASA WA UBORESHAJI MIUNDOMBINU YA MAJI UMEKAMILIKA: WAZIRI KAMWELE


 Waziri wa Maji na Umwagilkiaji, Mhandisi Isack Kamwele, (katikati), Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka, (DAWASA), Mhandisi Romanus Mwang'ingo, (kulia), na Mkandarasi,   Mhandisi P.G. Rajani wa kampuni ya WAPCOS Limited ya India wakionyesha furaha wakati Mheshimiwa Waziri na ujumbe wake walipotembelea moja ya maeneo ya utekelezaji wa mradi wa uboreshaji miundombinu ya maji jijini Dar es Salaam na Pwani, kwenye ujenzi wa tenki la kuhifadhia na kusambaza maji la Makongo, Desemba 5, 2017.
 Waziri Mahandisi Kamwele, (kulia), Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mwang'ingo, (wakwanza kushoto) na wataalamu wengine,m wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa DAWASCO, Mhandisi Cyprian Luhemeja, wakati Mheshimiwa Waziri alipotembelea mradi wa ujenzi wa tenki Makongo juu.
 Waziri Mhandisi Kamwele, (Kushoto), akifurahia jambo na Meneja Uhusiano na Jamii wa DAWASA, Bi. Neli Msuya, wakati Waziri alipotembelea eneo la utandazaji mabomba huko Malamba Mawili.
Mhandisi Kamwele, akiongozana na wafanyakazi wanaofanya kazi ya kutandaza mabomba huko Malamba Mawili.

Comments