Featured Post

WCS WAIPIGA MSASA JUMUIYA YA HIFADHI YA WANYAMAPORI WAGA

 Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William aliwakata wanajumuiya ya hifadhi ya wanyamapori WAGA kuzitunza rasilimali za wanyama pori kwa faida ya sasa na vizazi vijavyo kama wao walivyotunziwa na wananchi waliokuwepo miaka ya huko nyuma .
Mratibu wa shughuli za uhifadhi kwa jamii katika shirika lisilo la kiserikali (WCS) Anna Kimambo alisema lengo la shirika hilo ni kuhakikisha jamii zinasimamia vilivyo rasilimali za wanyama pori,misiti na vyanzo vya maji ili baadae weweze kuona faida ya vitu wanavyo vitunza.


Na Fredy Mgunda, Mbalali

Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na uhifandhi shirikishi wa wanayama pori (WCS) limeipiga msasa jumuiya ya hifadhi ya wanyamapori WAGA kwa lengo la kuhakikisha kuwa wanawalinda wanyama pori na kunufaika na uwepo wa wanyama pori hao.
 
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William aliwakata wanajumuiya ya hifadhi ya wanyamapori WAGA kuyatumia vizuri mafunzo waliyopata kulinda rasilimali za wanyama pori.

“Nawaombeni tumieni vizuri mafunzo haya kwa kuwa yatawasidia katika swala zima la uhifadhi ambalo ndio jukumu lenu la kwanza kabla hamjaangalia nini mnapata kama faida kwa kufanya hivyo WAGA itakuja kuwa jumuiya kubwa sana” alisema William

William aliwaomba jumuiya hiyo kutojihusisha na ujangili kwa kuwa wanaelimu ya uhifadhi na kuhakikisha wanyama pori wanalindwa kwa faida za taifa.

“Kuna jumuiya nyingi zimekuwa na migogoro kutokana na baadhi ya wajumbe kujihusisha na ujangili na kusababisha wanyamapori wengi kukimbia katika maeneneo ya hifadhi na kuwapunguzia kipato kwa wanajumiya hivyo nendeni mkatoe elimu kwa wananchi wengine kwa kuwa nyinyi mshapata elimu hiyo” alisema William

Aidha William alisema kuwa jumuiya ya WAGA bado ni changa hivyo wanatakiwa kuheshimu utawala bora ili kufikia malengo ambayo wamejiwekea kwa kunufaika na pori ambalo serikali imewapatia kwa ajili ya kufanya maendeleo ya vijiji.

“Najua kuwa mmeenda kujifunza kwenye jumuiya nyingine na mmeona kuna jumuiya zinamigogoro mingi hadi serikali huwa inaingilia kati na kuna jumuiya ambazo zinaendeshwa kwa kufuata utawala bora hivyo nawaomba mjifunze kufanya kazi kwa kufuata utawala bora” alisema William

William alilipongeza Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na uhifandhi shirikishi wa wanayama pori (WCS) kwa mikakati wanayoifanya ya kuhaikisha jumiya ya WAGA inaendeshwa kisasa kwa manufaa ya taifa kwa kulinda wanyama pori ambao ndio hazina ya taifa katika kukuza pato la taifa.

Kwa upnde wake mratibu wa shughuli za uhifadhi kwa jamii katika shirika lisilo la kiserikali (WCS) Anna Kimambo alisema lengo la shirika hilo ni kuhakikisha jamii zinasimamia vilivyo rasilimali za wanyama pori,misiti na vyanzo vya maji ili baadae weweze kuona faida ya vitu wanavyo vitunza.

“Unajua kila siku nasema kuwa mtu akitunza rasilimali za wanyama pori nauhakika faida yake ni rahisi kuipata kutoka na kupata wawekezaji wengi ambao watakimbila eneo hilo kwa kuwa limehifadhiwa vizuri na litakuwa na wanyama pori wengi” Kimambo

Kimambo alisema kuwa WCS iliamua kuanza kuisaidia jumuiya hii ya WAGA kwa kutumia fedha za msaada kutoka USD ambazo zimetumika kutoka mwanzo mwa mchakato huu hadi hapa ulipofikia hivyo bila msaada wa USD wasingefika hapo walipofika.

“Kuunda jumuiya na kuisimamia hadi ilipofika hapa sio jambo dogo wangekuwa wananchi pekee yao wasingefanikiwa kutokana na mchakato huu kuhitaji fedha nyingi sana na kwa wananchi kingekuwa kitendawili” alisema Kimambo

Kimambo alisema kuwa WCS ilipita kijiji kimoja hadi kingine kutoa elimu ya uhifadhi wa wanyama pori ili wananchi wajue umuhimu wa uhifadhi wa wanyapori na ndio maana kukaundwa hii jumuiya ya WAGA inajumuisha vijiji vitano.
Lakini Kimambo alivitaja vijiji ambavyo vitanufaika na jumuiya ya hifadhi ya wanyamapori WAGA ni kijiji cha Nyakadete ambapo ndio makao makuu ya jumuiya hiyo,kijiji cha Nyamakuyu,kijiji cha Igomaa, Ihanzutwa na kijiji cha Mahoninga.

“Ukiangalia vijiji hivyo utagundua kuwa vimezunguka katika wilaya kuu tatu ambazo ni wilaya ya Mufindi,Iringa DC na wilaya ya Mbalali ambapo wilaya hizozipo katika mikoa miwili ya Iringa na Mbeya” alisema Kimambo

Naye afisa wanyamapori wilaya ya Mufindi Recho Nambo alisema kuwa katiba ya jumuiya ya WAGA imetengenezwa kwa mfumo ambao hautasababisha migogoro kama ilivyokuwa kwenye katiba za jumuiya nyingine.

“Kwa kweli katika jumuiya hii ya WAGA hatutegemei migogoro tena kwa kuwa tumetengeza katiba kwa ushirikiano wa wataalam wengi wenye weledi wa maswala ya katiba hivyo napenda kuwaambia kuwa jumuiya ya WAGA itakuwa ya mfano hapa nchini” Nambo

Comments