Featured Post

MAJI MAREFU ASIFU JUHUDI ZA SERIKALI YA JPM KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI

 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani Alimaarufu Proffesa Maji Marefu akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Mombo mashuka  kwa niaba ya Vituo vya Afya vyengine kwenye halfa iliyofanyika ukumbi wa Halmashauri Korogwe Vijijini kulia ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Dkt Frank Chiduo na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini.
  Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani Alimaarufu Proffesa Maji Marefu akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Mombo mashuka  kwa niaba ya Vituo vya Afya vyengine kwenye halfa iliyofanyika ukumbi wa Halmashauri Korogwe Vijijini kulia ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Dkt Frank Chiduo na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini
 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani Alimaarufu Proffesa Maji Marefu kulia akiteta jambo kabla ya kukabidhi vitanda hivyo kuhusu umuhimu wa vifaa hivyo kutunza ili kuweza kuwahudumia wananchi.
 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani Alimaarufu Proffesa Maji Marefu akiingia kwenye hospitali ya wilaya ya Korogwe Magunga kwa ajili ya kukabidhi vifaa tiba vilivyotolewa na Serikali kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini,John Nyarongo
 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani Alimaarufu Proffesa Maji Marefu kulia akiteta jambo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini,John Nyarongo
 Mganga Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Dkt Frank Chiduo akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea vifaa hivyo
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini,John Nyarongo naye akizungumza katika halfa hiyo
 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani Alimaarufu Proffesa Maji Marefu
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini akizungumza na waandishi wa habari
MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Nyong’ani alimaarufu Proffesa Maji Marefu alisifu juhudi za serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli kuhakikisha wanazipatia ufumbuzi changamoto za afya katika maeneo mbalimbali hapa nchini ili wananchi kupata huduma bora
Proffesa Maji Marefu aliyasema hayo wakati akikabidhi vifaa tiba kwa Halmashauri ya Korogwe Vijijini vilivyotolewa na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto kupitia Bohari ya Madawa MSD wamewapatia vitanda vya kulalia wagonjwa,magodoro na mashuka vikiwa na thamani zaidi ya sh.milioni 17.

Vifaa tiba hiyo kwa upande wa vitanda vya wagonjwa vitasambazwa kwa baadhi ya vituo vya Afya na Zahanati zilizopo wilayani humo ambavyo ni Magoma, Mombo, Bungu,Mazinde,Manka,Hale,Mashewa,Vugiri na Makumba

Kwa upande wa vitanda vya kuzalishia vitapelekwa kwenye zahanati za Mandera,Kwemazandu,Lwengera,Mkomazi  na Makumba ambavyo vitasaidia kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo awali.

“Niwaambieni tu serikali yenu chini ya Rais Dkt John Magufuli imejipanga vema kuhakikisha inatatua kwa vitendo changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo ya huduma za afya na ndio maana leo hii tunakabidhi vifaa hivi kwa lengo la kuboresha huduma hizo “Alisema.

Alisema vifaa hivyo vimefika wakati muafaka ambapo vitasaidia kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo ikiwemo mashuka,magodoro na vitanda vitakavyosaidia kuhakikisha huduma zinazotolewa vinakuwa bora.

“Ndugu zangu wananchi serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli imefanya mambo mengi makubwa likiwemo la kuhakikisha wanaboresha huduma za Afya katika maeneo mbalimbali nchini  hivyo tuendelea kumuombea mungu na kumuunga mkono katika juhudi hizo “Alisema.

Awali akizungumza katika makabidhiano hayo,Mganga Mkuu wa wilaya ya Korogwe (DMO) Dkt Frank Chiduo aliishukuru serikali kwa kuwapatia msaada huo ambao umekuwa chachu ya ya kupunguza changamoto za upungufu wa vifaa tiba kwenye wilaya hiyo kwa kuwapatia vifaa hivyo

Alisema halmashauri ya wilaya ina jumla ya hospitali moja ,Vituo vya Afya vitatu na Zahanati arobaini na mbili zote zikiwa zinamiliki wa na serikali .

“Lakini pia Halmashauri ina jumla ya vitanda 330 vya kulala wagonjwa pamoja na magodoro,shuka 624 kati ya shuka hizo 1320 zinahitajika ,vitanda 61 vya kujifungulia katika vituo vyote hivyo kukidhi mahitaji yaliyopo kwa sasa “Alisema.

“Pia kati ya magodoro yaliyopo 80 yemachakaa na yanahitaji kubadilishwa hivyo kuwa na upungufu wa shuka 690 na godoro 80 “Alisema.
 Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

Comments