- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
JAMII
kadhaa za vipepeo wana uwezo wa kujigeuza na kujifanya waonekane kama ni wa
jamii nyingine.
Jamii za
vipepeo wa aina hii ni Batesian na Mullerian ambao wanajibadilisha na kujifanya
ni wa jamii nyingine ili kupata faida kadhaa ikiwemo ulinzi, kwani jamii
wanazojifananisha nazo zinaogopwa kwa kiasi fulani na wadudu na ndege wanaoweza
kuwala.
Mathalan, wadudu
wengi na ndege hawapendi kuwala vipepeo wa jamii ya Common Rose na Crimson Rose
kwa sababu ya ladha yao mbaya.
Kwahiyo,
vipepeo wa jamii nyingine, hasa Common Mormon majike ambao hupatikana zaidi
huko India, hupenda kujigeuza kuonekana kama jamii hizo ili kukwepa kuliwa na
wadudu wengine au ndege.
Jamii ya
Mullerian wanapenda kujionyesha kama Aposematic kwa lengo lile lile la
kuwahadaa maadui zao.
Jamii
nyingine yenye sifa hii ya kujifananisha na jamii nyingine ni Heliconius
inayopatikana zaidi huko Marekani.
Baadhi ya
vipepeo wana michoro inayofanana na macho katika mabawa yao. Michoro hii ni
moja ya vitu ambavyo vipepeo wanavitumia kujifananisha na jamii nyingine.
Katika
jamii nyingine, hutumia sauti za mawasiliano kama njia ya kujifananisha na
jamii tofauti na za kwao.
Wengi
hutumia sauti wanazozitoa wakati wanapokuwa tayari kujamiiana.
Lakini
wataalam bado hawajaweza kuthibitisha moja kwa moja kazi kuu ya michoro hii
inayofanana na macho katika mabawa ya vipepeo.
Mabadiliko
kwa msimu
Jamii
nyingi za vipepeo katika maeneo ya Tropiki zinajibadilisha kulingana na msimu
ambapo mabadiliko yao yanatokana na mabadiliko ya misimu ya hali ya hewa.
Mara
nyingi mabadiliko haya huendana na misimu ya mvua, hivyo kuna mabadiliko wakati
wa kiangazi na wakati wa masika.
Hata
hivyo, ni jinsi gani vipepeo wanajibadilisha kulingana na msimu, ni jambo
ambalo halijaweza kubainika wazi.
Kwa mujibu
wa tafiti kwa kutumia kemikali, mabadiliko yanayotokea wakati wa kiangazi ni ya
ajabu na inadhaniwa kuwa mabadiliko hayo yanamwezesha kipepeo kuhimilia
mabadiliko ya hali ya hewa.
Baadhi ya
vipepeo hupata rangi nzito nyeusi wakati wa masika. Inaaminika rangi hii
huwasaidia kufyonza na kuhifadhi joto kutoka kwenye jua, kwani nafahamika kuwa
rangi nyeusi inahifadhi joto kwa wingi.
Vipepeo
jamii ya Bicyclus anynana ni moja ya jamii za vipepeo ambao huonyesha
mabadiliko ya msimu.
Jamii hii
ambayo hupatikana kwa wingi barani
Afrika wana mabadiliko makubwa mawili kulingana na msimu.
Wakati wa
masika, jamii hii huwa na alama za macho makubwa zinazong’aa lakini wakati wa
kiangazi wanakuwa na alama za macho madogo sana ambazo ni vigumu kuziona kwa urahisi.
Wakati mwingine alama hizo hupotea kabisa.
Lava wa
jamii hii wanaokua katika mazingira ya joto kali na unyevunyevu wa masika,
wanakua na kuwa na sifa za vipepeo wa msimu wa masika wakati wale wanaokua
wakati wa kipindi cha kiangazi wanakuwa na sifa za vipepeo wa msimu wa kiangazi
pale wanapopevuka.
Mabadiliko
haya yanayohusu alama za macho yanawasaidia sana vipepeo hawa kuendesha maisha
yao kirahisi kulingana na msimu. Mathalan, wakati wa msimu wa kiangazi, vipepeo
hawa wanaishi katika majani makavu ambayo hayahitaji sana kuwa na alama hizo.
Kwa
kutokuwa na alama hizi wakati wa kiangazi, wanaweza kujificha kwa urahisi
katika majani makavu.
Hii
inawasaidia kujilinda dhidi ya maadui. Wakati wa masika vipepeo hawa ambao
aghalabu huwa na rangi ya kahawia, wanakuwa hawana namna nzuri ya kujificha kwa
kutumia rangi zao kwa sababu majani wakati huu yanakuwa na rangi ya kijani.
Kwahiyo,
alama za macho zinazotokea wakati huu huongeza rangi zao na kuwawezesha
kuendelea kujichanganya na mazingira bila kugundulika kwa wepesi.
Tabia
Chakula
kikuu cha kipepeo ni nekta kutoka katika maua. Baadhi ya jamii pia hula poleni
kutoka katika maua pia.
Wengine
hula majimaji kutoka katika magamba ya miti, matunda yanayooza, vinyesi na
takataka nyingine.
Kutokana
na hali hii ya kujitafutia chakula kutoka kwenye maua, kipepeo anafanya jambo
moja kubwa la kusaidia kusafirisha poleni kutoka ua moja hadi jingine hivyo
kusaidia kazi ya uchavushaji (uzalishaji) ingawa vipepeo hawabebi poleni nyingi
kama walivyo wadudu wengine hususan nyuki, lakini wana sifa ya uwezo wa
kusafirisha poleni katika masafa marefu kuliko wadudu wengine.
Wanapopevuka,
vipepeo hula chakula katika hali ya majimaji tu ambayo huyafyonza kupitia
mirija inayojulikana kitaalam kama Proboscis.
Kama
ilivyoelezwa, vipepeo wanategemea zaidi nekta lakini pia hufyonza majimaji
mengine kutoka sehemu yoyote wanayoweza kuyapata.
Kupitia
majimaji hayo, vipepeo hujipatia maji na sukari ambayo huwaongezea nguvu na
madini kama Sodium na mengineyo na kuwasaidia sana kuzaana.
Jamii
kadhaa za vipepeo wanahitaji
Sodium kwa
wingi kwa ajili ya kuzaana. Jamii nyingine huhitaji sodium nyingi kuliko ile
wanayoweza kuipata kwenye nekta.
Ili
kutafuta sodium hii ya ziada, vipepeo wanavutiwa na vitu vyenye chumvichumvi na
matokeo yake wanajikuta wakati mwingine wakitua katika miili ya binadamu
inayokuwa na chumvi kutokana na jasho.
Pamoja na
kutembelea sehemu zenye majimaji, lakini inafahamika pia vipepeo hujipatia
chakula hasa madini katika vinyesi vya wanyama, matunda yanayooza na mizoga lakini
katika jamii nyingi za vipepeo ni madume tu ndio wanaokuwa na tabia ya
kujipatia chakula kutoka kwenye vinyesi.
Tafiti
zinaonyesha kuwa madume hutumia madini haya wanayoyapata kutoka kwenye vinyesi
na vitu vingine kama zawadi kwa wapenzi wao wakati wa kujamiiana.
Hii ndiyo
maana majike hawajihangaishi katika vinyesi na mizoga, wanajua tu kuwa
watajipatia madini haya kutoka kwa wapenzi wao.
Imeandaliwa na www.maendeleovijijini.blogspot.com.
Simu: +255 656331974.
Comments
Post a Comment