Featured Post

TFF YAMSIMAMISHA MCHEZAJI JOHN BARAKA WA AREA C


Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.
 
Katika taarifa hizo imebainika kuwa mchezaji wako John Baraka jezi namba 2 alioneshwa kadi nyekundu baada ya mchezo kumalizika kwa kumpiga ngumi mwamuzi ngumi ya mgongoni.

Alifanya kitendo hicho kwenye mechi namba 1 ya Kundi D la Ligi Daraja la Pili kati ya timu yako na Nyanza FC iliyofanyika Oktoba 1 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyerere uliopo Mbulu mkoani Pwani.

Kwa vile suala lake ni la kinidhamu, na kwa kutumia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza, Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imemsimamisha kucheza mechi za SDL hadi suala lake litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Mchezaji wako atafahamishwa siku ambayo kikao cha Kamati ya Nidhamu kitafanyika kusikiliza shauri dhidi yake ambapo pia atapata fursa ya kuwasilisha utetezi wake kama upo.

Comments