Featured Post

NAGANA (TRYPANOSOMIASIS) UGONJWA HATARI UNAOSHAMBULIA MIFUGO PAMOJA NA BINADAMU

Ng'ombe anayeumwa Nagana.

NAGANA au kitalaam Trypanosomiasis ni ugonjwa ambao hushambulia karibu mifugo yote na pia binadamu. Kwa binadamu ugonjwa huu hujulikana kama malale.

Ugonjwa huu husababishwa na vimelea vya protozoa vijulikanavyo kama Trypanosoma evansi na husambazwa na mbung'o au ndorobo (glossina spp).
Mbung'o akimuuma mtu.

Vijidudu hivi vikimuingia mnyama vinafyonza kiasi kingi cha sukari kwenye mwili wa  mnyama na kuharibu chembe nyekundu za damu na kusababisha upungufu mkubwa wa damu kwa mnyama husika.

DALILI
-Ugonjwa huu kwa ng'ombe unaweza usiwe hatari, wa kawaida au hata kuwa sugu na kuleta madhara makubwa ikiwemo kifo.
-Joto la mnyama hupanda hadi kufikia nyuzijoto 39C – 41C
-Mnyama hupata tabu kuona huku akitoa machozi mengi kama anayelia
-Uzalishaji wa maziwa hupungua ghafla kwa kiasi kikubwa
-Mnyama hupumua kwa tabu kwa kutumia nguvu
-Mnyama huonyesha kuchanganyikiwa akili, anaweza kutembea kwa mduara, kupiga pika kichwa kwenye mabanda au chochote na mnyama  huweza kupoteza fahamu
-Baadhi ya wanyama wajawazito huweza kutoa mimba, hii ni kwenye ile hali ya ugonjwa sugu ambao hushambulia pole pole
-Kuvimba kwa matezi
-Manyoya ya ng'ombe mgongoni wakati wa asubuhi yana kuwa yanang'aa fulani jua likiwaka, ila inahitaji uonyeshwe na wataalam kwanza.

UCHUNGUZI
Maafisa ugani wa mifugo watachukua sampuli za damu kutoka kwenye mkia au sikio la mnyama na vijidudu kuonekana kwa darubini ya umeme mkali kabla ya damu kukauka, pia njia ya kimaabara ya GIEMSA itasaidia kwa uchunguzi zaidi wa kimaabara wadudu wanaweza kupandikizwa kwenye sungura, panya na simbilisi/pimbi na baadae njia ya PCR, ELISA kutumika kuangalia vichochezi vya mwili.

TIBA
Kwa mifugo kama ng'ombe, mbuzi, kondoo, jamii ya farasi, mbwa na paka dawa kama diminaphen, diminakel hutumika kutibu ugonjwa huu, kwa upande wa binadamu sifahamu dawa gani inatumika.

KINGA
- Kuna njia ya kitaalam ijulikanayo kama sterile male technique, ambapo madume ya mbung'o hupigwa na mionzi ya gama na kushindwa kuzalisha yanapo panda, hii husaidia sana kwa sababu majike ya mbung'o hupandwa mara moja tu katika maisha yao wakati madume haya tasa huendelea kupanda majike tofauti tofauti.
- Dawa zinazomika kutibu ugonjwa huu zinaweza kukinga wanyama kama watapigwa kila baada ya miezi mitatu na mara 4 kwa mwaka.

- Ng'ombe wanaojulikana kama N'DAMA wanaopatikana Afrika Magharibi wanastahimili sana ugonjwa huu.

Comments