- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na wananchi wa eneo la
Lizaboni wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, na kuwataka kuendelea kutoa
ushirikiano kwa Jeshi hilo na kutii sheria za nchi pamoja na kuwafichua
wahalifu waliopo kwenye jamii, IGP Sirro, yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi
ya siku moja. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, akimsikiliza Kamanda wa Polisi
mkoa wa Ruvuma (SACP) Gemini Mushy, alipowasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi
ya siku moja yenye lengo la kuzungumza na maofisa na askari kuona changamoto
zao ikiwa pamoja na kuwakumbusha wajibu wao wa kutenda haki na kutoa huduma
bora kwa wananchi. Picha na Jeshi la Polisi.
Askari
wa kikosi maalumu cha kupambana na uhalifu na wahalifu katika mkoa wa Ruvuma,
wakimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, na kuwataka
kufanyakazi kwa kuzingatia sheria na taratibu pamoja na kutimiza wajibu wao wa
kutenda haki wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi. Picha na Jeshi la
Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro (watatu kulia kwenye meza kuu) na
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Binilith Mahenge,
wakiwa kwenye kikao cha pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama
ya mkoa huo, IGP Sirro, yupo mkoani humo kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku
moja yenye lengo la kuzungumza na Maofisa na askari na kuona changamoto zao
ikiwa pamoja na kuwakumbusha wajibu wao wa kutenda haki na kutoa huduma bora
kwa wananchi. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, akiwasalimia wanafunzi wanaosoma
shule ya msingi Wilayani Songea, aliokutananao uwanja wa ndege mkoa wa Ruvuma,
muda mfupi baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku moja yenye
lengo la kuzungumza na Maofisa na askari na kuona changamoto zao ikiwa pamoja
na kuwakumbusha wajibu wao wa kutenda haki na kutoa huduma bora kwa wananchi. Picha
na Jeshi la Polisi.
Comments
Post a Comment