Featured Post

DKT MWINUKA: NISHATI YA UMEME NI KIUNGO MUHIMU KUCHOCHEA UWEKEZAJI WA VIWANDA

NISHATI ya  umeme imeelezwa kuwa ni kiungo muhimu katika kuchochea uwekezaji wa viwanda hapa nchini ambao utasaidia kuinua kwa kasi uchumi ikiwemo maendeleo kwa watanzania.

Hayo yalibainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Dkt Tito Mwinuka hivi karibuni wakati akizungumza katika baraza kuu la 47 la wafanyakazi wa Tanesco  mjini hapa ambapo alisema kwa kutambua umuhimu huo wataihakikishia serikali malengo yao ya viwanda yanatimia.
Alisema kutokana na hali hiyo wataendelea kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana katika maeneo mbalimbali hapa nchini bila kuwepo kwa vikwazo vya namna yoyote ile ili azma hiyo iweza kutimia kwa vitendo na hivyo kuchochea kasi ya uchumi.
“Kama mnavyojua serikali ya awamu ya tano imeazimia kukuza uchumi nchi kufikia ule wa kati wa viwanda hivyo kufikia azma hiyo nishati ya umeme ni kiungo muhimu katika kuchochea uwekezaji wa viwanda ambao utasaidia harakati za maendeleo “Alisema
“Hivyo napenda kuihakikishia serikali kwamba tunatambua wajibu tulio nao katika kutimiza malengo hayo kwa kuongeza uwajibikaji na ufanisi kazini ambao ndio utakuwa dira ya kufikia mafanikio “Alisema.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema tokea kuanzishwa kwa baraza hilo limekuwa ni sehemu muhimu kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali kwa maslahi ya wafanyakazi ambao wamewaamini kuwawakilisha.
“Baraza hili limesaidia shirika kujua changamoto na kero
zinazowakabili mahala pa kazi na kwa pamoja ufumbuzi wake na
changamoto hizo zimepatiwa ufumbuzi kwa faida ya wafanyakazi na shirika kwa ujumla “Alisema.
Alisema serikali ya awamu ya tano imeazimia kukuza uchumi nchi kufikia ule wa kati wa viwanda hivyo ili kufikia azma hiyo nishati ya umeme nikiungo muhimu katika kuchochea uwekezaji wa viwanda ambao utasaidia harakati za maendeleo.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

Comments