Featured Post

WAZIRI UMMY SERIKALI IPO TAYARI KUGHARAMIA MATIBABU YA MBUNGE LISSU MAHALI POPOTE DUNIANI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga wakati akitangaza kuwa serikali ipo tayari kumpeleka kwenye matibabu mahali popote duniani mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lisu.

SERIKALI imesema kuwa ipo tayari kuingia kugharama zozote ili kumpeleka kwenye matibabu mahali popote duniani Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lissu iwapo watapokea maombi kutoka kwa ndugu na familia yatakaothibitishwa na daktari kuwa anahitaji huduma ya madaktari wa bingwa zaidi.

Akitaka apelekwe Marekani,Ujerumani na mahali mengine ikiwemo India tunaweza kumpelekea iwapo watapeleka maombi serikali kutaka ifanyie hivyo ili kuweza kuhakikisha anapata matibabu.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Tanga ambapo alisema wakipita maombi watatekeleza suala hilo haraka iwezekanavyo.

"Serikali haitakataa wala kushindwa kumuhudumia Tindu Lissu yeye ni Mtanzania kama wanavyohudumiwa wengine hivyo wao wapo tayari kuhakikisha anapata matibabu bora nje ya nchi "Alisema
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

Comments