Featured Post

MBUNGE ROSE TWEVE ASEMA, WATENDAJI FANYENI KAZI ACHENI MAJUNGU


Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Rose Tweve akizungumza na madiwani na wananchi wa halmashauri ya Mafinga Mjini wakati wa Baraza la Madiwani.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga akizungumza wakati wa baraza la madiwani lilofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo
Baadhi ya madiwani,viongozi pamoja na wananchi waliohudhuria baraza la madiwani lilofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Mafinga Mjini.

Na Fredy Mgunda, Mafinga

Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Rose Tweve amewata watendaji wa halmashauri ya Mafinga Mjini kufanya kazi kwa kujituma na kuwa tumikia wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini ambalo linaongozwa na mbunge Cosato Chumi.

Akizungumza wakati wa baraza la madiwani wa halmashauri ya Mafinga Mjini alisema kuwa watendaji wengi wamekuwa wakilalamikiwa kutokana na kufanya kazi chini ya kiwango na kuwapelekea wananchi kuwa na changamoto ambazo hazina sababu.

"Hivi watendaji kitu gani kinachosababisha msifanye kazi kwa weledi kama ambavyo mlivyokuwa mnaomba kazi,jamani serikali ya awamu ya tano haitaki mfanye kazi kwa mazoea kama zamani saizi mnatakiwa kufanya kazi kutokana na kasi ya kimaendeleo ya serikali ya awamu ya tano"alisema Tweve

Tweve alisema kuwa watendaji wanaohusika na sekta ya maji katika halmashauri ya Mafinga Mjini wamekuwa hawafanyi kazi kwa weledi kwani tatizo kuwabambikia bili wananchi limekuwa Sugu na kuongeza malalamiko mengi huko mitaani hivyo lazima mbadilike maana swala la bili limekuwa kero sana hapa Mafinga Mjini lazima mlitafutie ufumbuzi.

"Toka nimerudi nimekuwa nikipokea malalamiko mengi yanayohusu bili za maji naombeni tembeleeni nyumba kwa nyumba kuandika bili sahihi na sio kutoa bili kwa kukisia hii inaalibu sura nzima ya viongozi wa halmashauri ya Mafinga Mjini, narudia tena watendaji fanyeni kazi kwa kujituma acheni mazoea kazini"alisema Tweve

Aidha Tweve alimuomba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanafanya kazi za wananchi na sio kukaa tu ofisini kitu kinachosababisha kuongezeka kwa matatizo kwa wananchi, hivyo mtalazimika kuwafuata wananchi kujua changamoto zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga alisema kuwa ahakikisha watendaji wote wanaenda kufanya kazi kwa wananchi na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kama ilivyokuwa miaka ya huko nyuma na kuendelea kutekeleza Sera za chama cha mapinduzi CCM na kuendena na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John pombe Magufuli na kuwaletea maendeleo wananchi.

"Watendaji wangu mmekisikia alichosema mbunge Rose Tweve kuhusu wajibu kwa kweli hii ni aibu kubwa inatupaswa kujilekebisha ili kuendelea kutekeleza Sera za serikali ya awamu ya tano la sivyo nitaanza kuwatumbua mmoja baada ya mmoja ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa halmashauri ya Mafinga Mjini"alisema Makoga

Lakini Makoga aliwasifu wabunge Wawili ambao ni mbunge Cosato Chumi na Rose Tweve kwa kufanya kazi kwa nguvu na kuleta maendeleo ya wananchi wa wilaya ya Mufindi kwa ujumla maana kila siku tunapata mambo mapya ya kimaendeleo kupitia migongo yao na kuwaomba waendelee kutafuta njia nyingine za kuiletea maendeleo Mufindi.

"Miaka yote tungekuwa na wabunge kama hawa wawili leo hii Mufindi ingekuwa mbali sana kimaendeleo kutokana na Juhudi zao tunaziona maana saizi kila secta wameigusa kwa kuleta maendeleo au mikakati ya kutatua changamoto za maeneo husika" alisema Makoga

Nao baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo wasema kuwa bado wazitafutia ufumbuzi changamoto za Mji wa Mafinga licha ya kuwa na ufinyu wa bajeti za kimaendeleo kwenye miradi waliyoiomba hivyo wakipewa bajeti na kuajiri baadhi ya watumishi kila kitu kitaenda vizuri na changamoto za wananchi zitatuliwa kwa wakati.

Comments