Featured Post

TANGA UWASA INAHITAJI BILIONI 15 KUTEKELEZA MPANGO WA KUSAFISHA MAJITAKA


Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga kuhusu maadhimisho ya wiki ya Maji
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorra Killo akizungumza jambo wakati wa kikao hicho leo

 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga kuhusu maadhimisho ya wiki ya Maji
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa kulia akiteta jambo na Meneja Rasilimali watu na Utawala wa Mamlaka hiyo,Haika Ndalama.
 Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa ambaye hayupo pichani.
  Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa ambaye hayupo pichani katikati mwenye hijabu ni Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania

 Watumishi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa wakiandaa baadhi ya dondooo kuhusiana na wiku ya maji

 Mwandishi wa Gazeti la Daily News Mkoani Tanga Amina Kingazi akiuliza swali kwenye mkutano huo kulia ni Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Mkoani Tanga,Raisa Saidi.
 Mwandishi wa Azam TV Mkoani Tanga,Mariam Shedaffa akifuatilia kwa umakini taarifa mbalimbali za mamlaka ya Maji Safi na Usafiri wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)

 Waandishi wa Habari Mkoani Tanga Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania wa pili kulia wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwakilishwa kwenye semina hiyo
Mwandishi wa Gazeti la Mtanzania,Amina Omari akuliza swali kwenye mkutano huo
MAMLAKA ya Majisafi na Majitaka katika Jiji la Tanga (Tanga-Uwasa), linahitaji kiasi cha shilingi bilioni 15 hadi 20 kwa ajili ya kutekeleza mpango wa kusafisha majitaka yaweze kutumika kwa shughulinyingine za kibinadamu ikiwemo kilimo cha umwagiliaji.
 
Akizungumza katika semina kwa wanahabari Jijini hapa Mkurugenzi wa Tanga-Uwasa Injinia Joshua Mgeyekwa, alisema kutokana na kuzaliza kiasi cha mita za ujazo zipatazo 2,700, wameonelea wayasafishe kwa kujenga mfumo utakaosaidia maji hayo kutumika tena.

Mgeyekwa alisema tayari wametenga eneo la Utofu kama sehemu
itayokusanya maji taka ambayo kwa sasa kiasi cha asilimia 10 cha wateja wao maji wanayoyazalisha kupelekwa baharini hivyo mfumo huo utasaidia suala zima la uchafuzi wa mazingira.

“Tupo na mpango wa kuyatumia maji taka kwa shughuli nyingine kama kilimo cha mbogamboga, unaimani kwa kufanya hivyo tutaongeza kipato cha mtu mmoja moja…Lakini ili mpango huu uweze kutimia tunahitaji kiasi cha shilingi bilioni 15 hadi 20 kutekelezwa,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa mfumo wa kutumia majitaka kwa shughuli nyingine za kibinadamu umekuwa ukitumika katika nchi zilizoendelea kama China, Israel na kwingineko ambako teklonojia hiyo imeanza.

Katika hatua nyingine Mamlaka hiyo imeanza mpango wa kufunga mita za watumiaji maji wa malipo ya kabla zinazojulikana kwa jina la ‘Lipa Maji Kadiri Unavyotumia’ (LIMAKU) ambazo tayari wamezifunga katika baadhi ya maeneo yakiwemo vikosi vya jeshi hapa nchini.

Mkurugenzi huyo alisema hadi sasa wamefunga katika vikosi vya jeshi vilipo mkoani hapa pamoja na shule 20 za msingi zilizopo katika Jiji la Tanga na maendeleo yake yanaenda vizuri.

“Tumeagiza mita nyingine za Limaku zipatazo 300 hizi pia tutazifunga katika taasisi za serikali na watu wengine hasa wateja wetu wenye madeni makubwa,” alisema Mgeyekwa.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

Comments