Featured Post

MKUU WA MKOA WA TANGA, MARTIN SHIGELLA AWAPIGA MSASA MAKATIBU TAWALA


Tanga, MKUU wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella, amesema Utafiti mpya wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi kwa kutumia mfumo wa (CD4T-cell count) utasaidia kupunguza maambukizi ya Ukimwi.
Amesema Utafiti huo utaangazia pia kuwepo kwa Viashria vya Usugu wa dawa, kiwango cha maambukizo ya Kaswende na homa ya Ini kwa watu wenye umri wa miaka 15 na zaidi.
Amesema Tafiti tatu zilizotangulia zimekuwa zikiwahusiha wananchi wenye umri wa miaka 15 hadi 49 tofauti na utafiti wa mwaka 2016/ 2017 ambao ni wa  kipekee ambapo kwa mara ya kwanza wananchi wa rika zote katika kaya zilizochaguliwa watahusihwa.
Kwa upande wake, Meneja Takwimu Mkoa wa Tanga, Tonny Mwanjoto, aliwataka Makatibu Tawala kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi pamoja na wanafunzi shuleni kutokomeza maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Alisema kufanya hivyo itasaidia  juhudi za Serikali kuhakikisha maambukizi ya VVU yanapungua ikiwa na pamoja na kuyatokomeza moja kwa moja.




Wajumbe wa mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi 2016 /2017 wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa kwa Makatibu Tawala kutoka Wilaya za Tanga na Wawakilishi wa TACAIDS pamoja na Wadau wa Maendeleo uliofanyika leo  ukumbi wa mikutano jengo la Mkuu wa Mkoa.



Meneja Takwimu Mkoa wa Tanga, Tonny Mwanjoto akizungumza na waandishi wa habari wa Tanga mara baada ya kuisha kwa mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashria na Matokeo ya Ukimwi 2016/ 2017.

Comments