- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Dk. Karl Peters (kati) akiwa na wenzake Dk. Karl Juhlke na Joachim Graf.
Na
Daniel Mbega
MIKATABA ya ulaghai! Ndivyo inavyoitwa. Naam, ni ile
mikataba iliyofanywa kwa hila na Mjerumani Dk. Karl Peters dhidi ya
watawala wa Kiafrika ambayo ndiyo ilikuwa mwanzo wa kuitishwa kwa Mkutano wa Kuligawa
Bara la Afrika mwaka 1884-1885 kule Berlin na kuanza kwa ukoloni barani humu.
MaendeleoVijijini inafahamu kwamba, mkutano huo ambao pia unafahamika kama
Congo Conference ulifanyika siku ya Jumamosi, Novemba 15, 1884 katika makazi
rasmi ya Chancellor Otto von Bismarck huko Wilhelmstrasse.
Mataifa 14 yaliyohusika na mkutano huo muhimu yalikuwa Muungano wa
Austria-Hungary, Ubelgiji, Denmark, Ufaransa, Dola ya Ujerumani yenyewe,
Italia, Uholanzi, Dola ya Ottoman (Uturuki ya sasa), Ureno, Russia, Hispania,
Muungano wa Sweden-Norway, Uingereza na Marekani.
Bismarck alikubali kuwa mwenyekiti. Mwakilishi wa Uingereza
alikuwa Sir Edward Malet (Balozi wa Uingereza katika Dola ya Ujerumani). Henry Morton Stanley
alihudhuria kama mwakilishi wa Marekani.
Akitumia ‘ujinga’ wa watawala wetu wa jadi ambao hawakujua
kusoma wala kuandika, achilia mbali kuijua lugha ya Kijerumani, Karl Peters
alitumia hila na kuwasainisha mikataba ya kilaghai ambapo bila wenyewe kuelewa,
walijikuta wakimkabidhi, kwa niaba ya Ujerumani, himaya zao zote na wao wakawa
watawaliwa.
MaendeleoVijijini inatambua kwamba, mkataba wa ulaghai ambao umekuwa
ukipigiwa mfano zaidi nchini Tanzania ni ule wa Karl Peters na Chifu Mangungo
wa Usagara huko Msowero, Wilaya ya Kilosa katika Mkoa wa Morogoro.
Vizawadi vidogo vidogo na hila nyingi, huku akitumia
watumishi wake Waafrika ‘kutafsiri’ Kijerumani – ambacho pia hawakukijua –
viliweza kumfanya Karl Peters amrubuni Chifu Mangungo aisalimishe himaya yake
yote kwa Wajerumani bila kutambua.
Karl Peters, akiwa na miaka 28 tu wakati huo, na rafiki zake
Dk. Karl Juhlke, Pfeil na August Otto waliondoka Ujerumani mwezi Septemba 1884.
Walisafiri wakijifanya mafundi makenika huku wakitumia majina ya bandia hadi
walipoingia Zanzibar ambako waliwasili Novemba 4, 1884. Baadaye wakavuka kuingia
bara. Waliondoka Sadani mnamo Novemba 10 wakiwa na wapagazi 36.
Wakasafiri hadi Uzigua (ambako walimsainisha mkataba wa
kwanza kabisa wa kilaghai Chifu Mbwela wa Wazigua) wakipitia Mto Wami hadi
kuingia Uluguru, ambako kote walifanya mikataba ya ulaghai (bogus treaties)
katika kila walikopitia. Chifu Mangungo wa Msowero katika Usagara mara nyingi
ndiye anayetajwa kwenye mikataba hiyo ya kilaghai.
Mkataba wa ulaghai baina ya Karl Peters na Mangungo, ambao
MaendeleoVijijini imeuona, unasomeka hivi kwa Kiingereza:
Mangungo,
Sultan of Msovero in Mwenyisagara, and Dr.
Karl Peters. Mangungo simultaneously for all his people and Dr. Peters for alt
his present and future associates hereby concluded a treaty of Eternal
Friendship.
Mangungo
offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters,
as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive
and universal utilization for German colonization.
Dr. Karl
Peters, in the name of the Society for German Colonization declares his
willingness to take over the territory of the Sultan Mangungo with all rights
for German Colonization subject to any existing suzerainty of Mwenyi Sagara.
In
pursuance thereof, Sultan Mangungo hereby cedes all the territory of Msovero,
belonging to him by inheritance or otherwise for all time, to Dr. Karl Peters,
making over to him at the same time all his rights.
Dr. Karl
Peters in the name of the Society for German Colonization undertakes to give
special...attention to Msovero when colonizing Usagara.
This
treaty has been communicated to the Sultan Mangungo by the interpreter Ramzan
in a clear manner and has been signed by both sides, with the observation of
the formalities valid in Usagara the Sultan on direct enquiry having declared
that he was not in anyway dependent upon the Sultan of Zanzibar, and that he
did not even know the existence of the latter.
Sgd. Dr.
KARL PETERS
Sgd. MANGUNGO
Sgd. MANGUNGO
This
contract has been executed legally and made valid for all time before a great
number of witnesses, we testify herewith:
Kwagakinga
(mark);
Sultan
Mangungo’s son of Golola (mark);
Sultan
Mangungo’s second son of Draman (mark);
Graf
Pfeil August Otto;
Mark of
the intepreter Ramazan etc.
Dr. Karl
Juhlke.
Msovero
Usagara November 29, 1884.
Hii ni tafsiri isiyo rasmi ya MaendeleoVijijini:
Mangungo,
Sultan wa Msovero katika Mwenyisagara, na Dk. Karl Peters. Mangungo sambamba na
watu wake wote na Dk. Peters kwa niaba yake na washirika wake wengine wajao kwa
pamoja wanaweka mkataba wa Urafiki wa Kudumu.
Mangungo
amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl
Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani (Society for German
Colonization), kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja koloni la Kijerumani.
Dk. Karl
Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira
yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni
la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.
Katika
kutekeleza hilo, Sultan Mangungo anakabidhi himaya yote ya Msovero, inayomilikiwa
nay eye mwenyewe kwa urithi au kwa namna yoyote ile kwa nyakati zote, kwa Dk.
Karl Peters, na wakati huo huo kumkabidhi haki zake zote.
Dk. Karl
Peters kwa niaba ya Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani anakusudia kuweka mkazo
maalum kwa eneo la Msovero wakati wa kuitawala Usagara.
Mkataba
huu umewasilishwa kwa Sultan Mangungo na mkalimani Ramzan katika dhana ya wazi
kabisa na umesainiwa na pande zote, kwa kuzingatia taratibu zilizopo katika Usagara,
Sultan baada ya kuhojiwa moja kwa moja alikiri kwamba hakuwa na ushirika ama
kutegemea kwa namna yoyote Sultan wa Zanzibar, na kwamba hakuwa hata akimfahamu.
Imesainiwa.
Dk. KARL PETERS
Imesainiwa. MANGUNGO
Imesainiwa. MANGUNGO
Mkataba
huu umefanyika kihalali kabisa na umehuishwa kwa nyakati zote mbele za
mashahidi wengi, ambao tunakiri hapa:
Kwagakinga
(dole gumba);
Golola mtoto
wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Draman mtoto
wa pili wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Graf
Pfeil August Otto.
Dole
gumba la mkalimani Ramazan etc.
Dk. Karl
Juhlke.
Msovero
Usagara Novemba 29, 1884.
Hii ndiyo ilikuwa aina ya mikataba ambayo Karl Peters
aliisaini na watawala wa jadi. Ni ukweli ulio wazi kwamba Chifu Mangungo, na
kwa kiongozi yeyote wa Kiafrika kwa maana hiyo, angeweza kuingia mkenge na
kuiachia ardhi yake na mamlaka yake kwa mgeni laghai kama Karl Peters.
Ni dhahiri kwamba Mangungo hakujua kusoma wala kuandika Kijerumani.
Inaonekana pia kupitia kwenye maelezo ya mkataba kwamba mkalimani mwenyewe
hakujua kusoma wala kuandika kabisa. Kwa gharama yoyote ile, ikumbukwe kwamba Ramazan
alikuwa ameajiriwa na Karl Peters na alitakiwa kufuata maelekezo yake.
Karl Peters aliwasili Ujerumani Februari 7, 1885 akiwa na
lundo la mikataba. Peters alitumia mikataba hiyo kupata kibali maalum - Schutzbrief
– ili kutambuliwa kwa madai yake Februari 27, 1885.
Kwa maneno mengine, Otto von Bismarck, Chancellor mkuu wa
Ujerumani wakati huo, alikuwa amebadili sera yake ya awali dhidi ya Ujerumani
katika kutafuta makoloni.
Imeandaliwa na MaendeleoVijijini
Comments
Post a Comment