Featured Post

ZAIDI YA SHILINGI MILIONI NNE ZAPATIKANA KWENYE HARAMBEE ILIFANYWA NA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE

 Mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi akiwa kwenye harambee ya uchangiaji wa vifaa vya ujenzi wa zahanati ya ushirika wa Rungwa iliyopo katika wilya ya Ileje.

 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Haji Mnasi  alihesabu kiasia cha shilingi milioni nne na zaidi kwa lengo la ufanikishaji wa upatikanajiwa vifaa vya kumalizia ujenzi wa zahanati ya ushirika wa Rungwa.

Na Fredy Mgunda
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Haji Mnasi afanikisha azima ya ujenzi wa zahanati bora katika ushirika wa rungwa kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa wilaya ya Ileje.


Akizungumuza wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa zahanati hiyo  mkurugenzi Mnasi alisema kuwa wameamua kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha hutuma za afya kwa wananchi ili wafanye kazi kwa kujituma.

“Kauli mbiu ya Rais wetu ni hapa kazi tu sasa ukiwa na jamii ambayo dhohofu huwezi kufikia malengo ya hapa kazi hivyo nimefanya harambee hii kumuunga mkono Rais kwa kuboresha huduma za afya katika wilaya yetu ya Ileje na kuwafanya wananchi kufanya kazi kwa kujituma huku wakiwa na afya njema na kuendelea kulijenga taifa kwa kufanya kazi kwa kujituma”.alisema Mnasi

Mnasi alisema wananchi wanatakiwa kujitoalea kwa hali na mali kufanikisha ujenzi wa zahati hiyo unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa jamii.

“Leo hii tumefanya harambee ya kuchangia kupatikana kwa vifaa vya kumalizia ujenzi wa zahanati unaogharimu kiasi cha shilingi milioni sita na nashukuru mungu nimefanikiwa zaidi  kupata shilingi milionii nne  hivyo lengo limetimia kilicho baki ni utekelezaji tu labda niwaombe kuzitumia pesa hizi vizuri kununua vifaa ya ujenzi ili wananchi waanze kupata huduma bora”. Alisema Mnasi

Aidha Mnasi alizitaka taasisi nyingine kuiga mfano wa ushirika wa Rungwa kwa ujenzi wa zahanati hiyo ambayo itarahisisha uwepo wa huduma bora kwa jamii husika.

“Tuna taasisi nyingi sana katika wilaya yetu hivyo naziomba nazo zijitahidi kuwa na malengo ya ujenzi wa zahanati ili kuendeleza kutoa huduma bora kwa jamii na kuifanya jamii kuwa huru kufanya kazi kwa nguvu huku wakiwa na afya bora”.alisema Mnasi

Nao baadhi ya waumini wa ushirika wa Rungwa walimushukuru Mkurugenzi huyo kwa kuendelea kujituma kufanya kazi kwa wananchi wa chini na kuwaboresha huduma za afya.

“Tulikuwa tunahitaji zaidi ya milioni sita lakini uwepo wa mkurugenzi Mnasi katika harambee ya leo kumesaidia kupata pesa nyingi ambazo zimefanisha azma ya umaliziaji wa ujenzi wa zahanati yetu”.walisema washirika

Comments