Featured Post

UNDP WAKUTANA NA WANAFUNZI WA SHULE YA WASICHANA ,WERUWERU MKOANI KILIMANJARO KUJADILI MALENGO MAPYA YA MAENDELEO ENDELEVU.

Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Alavaro Rodriguez (katikati) akiwa ameongozana na Mkurugenzi anayesimamia Mashirika ya Umoja wa Mataifa ,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ,Balozi Celestine Mushi (kushoto) na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru ya mkoani Kilimanjaro,Rosalia Flavian wakiingia katika ukumbi wa shule hiyo kwa ajili  kongamano.

Wanafunzi wa kidato cha Tano na Sita pamoja na wageni wakiimba wimbo kabla ya kuanza kwa kongamano hilo lililolenga kuzungumzia juu ya Malengo ya Maendeleo endelevu .
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru ,Rosalia Flavian akizungumza wakati wa Kongamano hilo.
Baadhi ya Walimu katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Weruweru wakifuatilia maelezo ya awali yaliyotolewa na Mkuu wa Shule hiyo.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Weruweru akiteta jambo na  Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Alavaro Rodriguez.
 Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Alavaro Rodriguez akizunguza katika Kongamano hilo.
Baadhi ya wanafunzi katka shule ya Sekondari ya Wasichana  ,Weruweru wakiwa katika kongamano hilo.
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania ,Hoyce Temu akizungumza katika kongmano hilo.
  Mkurugenzi anayesimamia Mashirika ya Umoja wa Mataifa ,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ,Balozi Celestine Mushi akitoa mada kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru juu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu .
Baadhi ya Wananfunzi wa Shule ya Sekondari ,Weruweru wakiwa wameshikilia vibao vinavyoonesha baadhi ya malengo mapya ya maendeleo endelevu wakati Balozi Mushi akiwasilisha mada .
Balozi Mushi akionesha Malengo mapya 17 ya  Maendeleo Endelevu kwa wananfunzi wa Shule ya sekondari Weruweru wakati akiwasilisha mada.
Balozi Mushi akitoa zawadi ya Pesa kwa wanafunzi wawili wa kidato cha Tano na Sita katika shule ya sekondari ya Wasichana ya Weruweru baada ya kuuliza na kujibu vyema maswali . 
Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Alavaro Rodriguezakiwa katika picha ya pamoja na walimu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru pamoja na wafanyakazi wengine wa Serikali.
Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Alavaro Rodriguez akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini. 

Comments