Featured Post

WAANDISHI WA HABARI WAPATA SEMINA KUHUSU MAHINDI YA GMO NA MATUMIZI YA BIOTEKNOLOJIA KATIKA KILIMO

 Mshauri mstaafu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAM), Dk.Nicholas Nyange, akitoa mada kwa waandishi wa habari kuhusu matumizi ya Bioteknolojia katika matumizi ya kilimo walipotembelea kituo cha utafiti wa kilimo cha Makutupora mkoani Dodoma.
 Mshauri mstaafu wa mradi wa kuzalisha mahindi yanayostahimili ukame kupitia mradi wa Wema, Dk. Alois Kullaya akitoa mada kuhusu mahindi hayo yanayotokana na teknolojia uhandisi jeni (GMO) kuhusu mafanikio ya mradi huo na changamoto zake.
 Wanahabari wakiwa nje ya lango kuu la kuingia katika shamba la majaribio la mahindi yaliyotokana na teknolojia ya GMO la Makutupora mkoani Dodoma wakisubiri taratibu za kuingia kwenye shamba hilo.
 Mtafiti Ismail Ngolinda wa Kituo hicho (kushoto), akitoa maelekezo kwa wanahabari kabla ya kuingia katika shamba hilo la majaribio.(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
  Mtafiti Ismail Ngolinda akiwaonesha wanahabari mahindi yaliyooteshwa kutokana na teknolojia hiyo ya GMO.
Wanahabari kutoka mikoa 7 wakiwa katika picha ya pamoja na watafiti wa kilimo mbele ya shamba hilo.

Comments