Featured Post

SKIPPERS HAVEN: HOTELI ILIYOSHEHENI MICHEZO LULUKI YA BAHARINI

 Na Jumia Travel Tanzania

Unaweza usiamini kwamba ile michezo ya baharini unayoiona kupitia kwenye runinga, wazungu wakiicheza unaweza ukaifanya ukiwa hapahapa nchini Tanzania. Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ingependa kukujuza kuwa hoteli ya Skipper’s Haven iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam, inayo michezo kadhaa ya baharini ambayo itakustaajabisha.

Hoteli hii ya kifahari na ya kuvutia inapatikana katika peninsula ndogo huku ikiwa na ufukwe binafsi na kukupatia fursa ya kufurahia michezo mbalimbali ya baharini kama ifuatavyo: 
Uvuvi kwenye kina kirefu
Skipper’s Haven ni hoteli pekee katika fukwe za Kusini, iliyopo umbali wa kilometa 40 Kusini mwa Dar es Salaam, yenye vifaa vya kutosha kwa ajili ya uvuvi wa kwenye kina kirefu. Ina wataalamu wenye uzoefu wa muda mrefu na ufukwe unaopendekezwa kuwa bora kwa shughuli hizo katika ukanda wa Afrika ya Mashariki.  


 Kupiga mbizi
Ni ndoto ya kila mpiga mbizi kupata fursa ya kuzamia kwenye kina kirefu cha bahari ya Hindi kujionea utajiri wa viumbe vilivyomo ndani yake. Fukwe za pwani ya Afrika ya Mashariki zinazo aina mbalimbali za samaki na miamba ya kuvutia. Hoteli hii ina vifaa vya kisasa pamoja na wataalamu wa kukusaidia kulifanikisha hilo. Samaki kama vile kobe wa baharini, dolfini na aina kadhaa za nyangumi wanaweza kuonekana kwa urahisi.  
Kusafiri kwenye Jahazi
Mojawapo ya vitu utakavyovikumbuka ukiwa hapa ni pamoja na kusafiri kwenye Jahazi siku nzima ukiwa baharini. Wataalamu waliobobea watakuzungusha sehemu mbalimbali baharini ukiwa kwenye chombo hicho na kufurahia mawimbi ya bahari ya Hindi. 

Michezo ya kwenye maji
Skipper’s Haven inakupatia uzoefu wa aina yake kwa michezo mbalimbali ya kwenye bahari. Michezo kama vile kuelea kwenye puto la plastiki au kuvutwa kwa kutumia boti pamoja na kuelea juu ya maji kwa kutumia kifaa maalumu. Mtu mwenye uzoefu wa yoyote anaweza kushiriki kwani kutakuwa na wataalamu watakaokuwa wanatoa muongozo ili uweze kujifunza na kufurahia.
Kujionea ndege wa aina mbalimbali
Mbali na michezo ya baharini, Skipper’s Haven ni mojawapo ya hoteli zilizojengwa kwa kuzingatia ustawi wa mimea na wanyama kwani hakuna miti iliyokatwa wakati inajengwa. Ukiwa hapa utapata fursa ya kujionea aina tofauti za ndege wakirandaranda na kuruka karibu na eneo hili. Hivyo, kwa wanaopenda kuona ndege wa mwituni ni vizuri kujaribu kutembelea. 

Hoteli hii pamoja na zingine kama vile Jangwani Sea Breeze Resort na Golden Tulip Hotel za jijini Dar es Salaam; Mermaids Cove Beach Resort & Spa, Paradise Beach Resort na Golden Tulip Zanzibar Boutique Hotel za visiwani Zanzibar; Nashera Hotel ya Morogoro na Kwetu Hotel inayopatikana mkoani Tanga zinapatikana kupitia mtandao wa Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ambapo kila siku ya Jumatano hutoa punguzo kubwa la bei kwa wateja, zoezi ambalo hudumu mpaka Ijumaa ya kila wiki.

Comments