Featured Post

SHINDANO LA KUMSAKA MLIMBWENDE WA MISS KIBOSHO 2017 JIJINI MWANZA LAFANA

Shindano la kumsaka mlimbwende wa MISS KIBOSHO 2017 Jijini Mwanza limeanza jana katika viunga vya Kibosho Luxury Bar iliyopo Kiseke Ilemela Jijini Mwanza ambapo wanyange 10 wanawania nafasi hiyo.


Wanyange hao kama wanavyoonekana pichani ni Caren Nestory, Dorice Ezra, Jullieth Michael, Elizabeth Faustine, Christina Lucas, Nasra Ramadhan, Jacline Moses, Denzry Michael, Kephlin Jacob na Aida Gazar.

Shindano hilo limeandaliwa na Raj Entertainment kwa udhamini wa Kibosho Luxury Bar, Wema Salon na Ngenda Salon huku likiwa limelenga kukuza sanaa ya ulimbwende kuanzia za mitaa hadi kitaifa.

Baada ya usiku ya kuamkia leo wanyange hao kuchuana vikali, fainali itafanyika leo kuanzia majira ya saa moja jioni katika viunga hivyo vya Kibosho Luxury Bar Kiseke Jijini Mwanza kwa kiingilio cha shilingi 5,000 tu.
Binagi Media Group
Wanyange wa shindano la Miss Kibosho 2017 wakionesha makeke yao jukwaani
Washereheshaji wakimtambulisha Matron wa Miss Kibosho 2017, Fania Hassan (katikati) ambaye alikuwa Miss Utalii nchini mwaka 2006.
Kila mlimbwende alionesha makeke ya hali ya juu hadi kuwapa wakati mgumu majaji. Kumbuka majaji ni Leonald Kaduguda (kushoto), Mama Ngenda Lutalo (katikati) na Mwl.Tatu Ngelengela (kulia).
Umakini katika kufuatilia kinyang'anyiro cha Miss Kibosho 2017
Majaji wakiahilisha shindano la Miss Kibosho 2017 usiku wa kuamkia leo. Kushoto ni Leonald Kaduguda, Mama Ngenda Lutalo (kulia) na Mwl.Tatu Ngelengela (katikati). Fainali itafanyika leo jioni kuanzia majira ya saa moja kamili.

Comments