Featured Post

MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOSHI WATOA ZAWADI KWA WAGONJWA HOSPTALI YA RUFAA YA MKOA WA KILIMANJARO, MAWENZI

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakiwasili katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro,Maawenzi wakiwa  wamebeba zawadi mbalimbali kwa ajili ya kutoa kwa wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo

Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro,Mawenzi ,Boniface Lyimo akizungumza mara baada ya kuwapokea Madiwani hao na kutoa maelekezo ya namna ya kutoa zawadi hizo kwa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo
Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,wakielekea katika wodi walimolazwa wagonjwa kwa ajili ya kutoa zawadi.
Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema na Diwani wa kata ya Kiusa,Stephen Ngasa akikabidhi zawadi ya sabuni ya unga kwa wagonjwa waliolazwa katika Hopstali ya Mawenzi.
Diwani wa kata ya Mawenzi,Hawa Mushi akitoa zawadi kwa mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo.
Diwani wa kata Pasua ,Charles Mkalakala akikabidhi zawadi kwa mmoja wa wagonjwa katika Hospitali hiyo.
Madiwani wakiongojea kuingia katika wodi nyingine kwa ajili ya kutoa zawadi kwa wagonjwa katika hospitali hiyo.
Madiwani wakitoa zawadi katika wodi ya wanawake Hospitali ya Mawenzi
Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema,Stephen Ngasa akizungumza na baadhi ya viongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro,awenzi mara baada ya kuhitimisha zoezi la kutoa zawadi kwa wagonjwa pamoja na kusafisha mazingira katika Hospitali hiyo.
Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema, Stephen Ngasa akiagana na katibu wa Hosptali ya Mawenzi, Boniface Lyimo mara baada ya kuhitimisha zoezi la kutoa zawadi na kusafisha mazingira ya hosptali hiyo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

Comments