Featured Post

KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA MAKAO MAKUU YA TTSA, TAWA NA TAFORI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizaya hiyo, Meja Generali Gaudence Milanzi (kushoto) wakiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipowasili katika ofisi za Wakala ya Miti za Mbegu Tanzania (TTSA) mjini Morogoro jana kwa ajili ya kuona kazi na miradi ya wakala huyo. Kushoto ni wajumbe wa kamati hiyo, Silafi Maufi ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa na Godwin Molel (wa pili kushoto), Mbunge wa jimbo la Siha.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhandisi Atashasta Nditiye (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi Endelevu ya Rasilimali za Misitu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Mohammed Kilongo alipowasili na kamati yake katika ofisi za Wakala wa Miti za Mbegu Tanzania mkoani Morogoro jana. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Wizara ya Maliasili na Utalii, Marry Faini na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa (wa pili kulia).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika ofisi za makao makuu ya Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA). Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhandisi Atashasta Nditiye.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA), Edigar Masunga (wa pili kulia) akiwasilisha taarifa ya wakala huyo kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi ya Maliasili na Utalii mkoani Morogoro jana. Alisema wakala huyo huzalisha aina 195 za mbegu, kati ya hizo asilimia 60 ni miti ya kienyeji na asilimia 40 ni miti ya kigeni. Kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe na kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhandisi Atashasta Nditiye.
Katibu Mkuu wa Wizaya ya Maliasili na Utalii, Meja Generali Gaudence Milanzi (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA), Edigar Masunga kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii mkoani Morogoro jana. Meja Generali Milanzi alisema Ujangili nchini kwa sasa umepungua kutokana na kasi ya udhibiti wa vitendo hivyo inayofanywa na askari wa wanyamapori kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama. Alisema nyara nyingi zinazokamatwa kwas sasa ni zile za zamani na kwamba uamuzi wa China kuzuia biashara ya meno ya tembo utasaidia kupunguza zaidi ujangili nchini.
Mtaalam wa Baiolojia ya mbegu wa Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania, Fandey Mashimba (kulia) akitoa ufafanuzi wa namna ya uaandaaji wa mbegu na miche ya miti kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipotembelea wakala huyo jana Mkoani Morogoro kwa ajili ya kuona shughuli na miradi ya wakala huyo. Kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe.
Meneja wa Kanda ya Mashariki na Kati wa Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania, Frida Mngulwi (kulia) akitoa maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii namna mashine za kuandaa mbegu za miti zinavyofanya kazi. Wa pili kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe.
 Wajumbe wa Kamati ya Bunge, Ardhi, Maliasili na Utalii wakikagua vitalu vya miche ya miti vya wakala wa mbegu za miti Tanzania (TTSA) walipotembelea makao makuu ya wakala huyo mkoani Morogoro jana.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA), Edigar Masunga (mbele kushoto) akiongoza wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kukaga shamba la miti la wakala huyo mkoani Morogoro jana. 
Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi Endelevu ya Rasilimali za Misitu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Mohammed Kilongo (kulia) akifafanua jambo kwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kulia) wakati wa kukagua shamba la miti la Wakala wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA) mkoani Morogoro jana.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI), Laurence Mbwambo (kushoto) akitoa maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii namna taasisi hiyo ilivyojipanga kuendesha tafiti zake na kuhifadhi taarifa za utafiti kwa njia ya mtandao.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akisistiza jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipotembelea ofisi za Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) mkoani Morogoro jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wanne kushoto) akitoa maelezo ya mtandao (kulia) wa kugundua matukio ya moto kwenye maeneo ya misitu nchini unavyofanya kazi kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii. Mtambo huo upo chini ya usimamizi na utafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Martin Laibooki akiwasilisha taarifa ya mamlaka hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembelea makao makuu ya mamlaka hiyo mkoani Morogoro jana. Katika taarifa yake ameeleza kuwa katika kipindi cha mwezi Julai hadi Agosti 2016 mamlaka hiyo ilitoa jumla ya shilingi bilioni 2.2 kama faida ya mgao wa mapato ya utalii kwa Halmashauri za Wilaya, vijiji pamoja na Jumuiya za Uhifadhi wa Wanyamapori nchini (WMAs). Hata hivyo alisema changamoto kubwa ya mamlaka hiyo kwenye uhifadhi kwa sasa ni uvamizi wa mifugo ndani ya maeneo ya hifadhi.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utali, Dkt. Aloyce Nzuki (kulia) akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki wa Wizara hiyo, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa wakati kamati ya bunge, Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembelea makao makuu ya TAFORI NA TAWA mkoani Morogoro jana.
Picha ya pamoja ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania na Taasisi ya Utafiri wa Misitu Tanzania (TAFORI).
Mtaalamu wa maabara wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) akieleza namna tafiti za misitu zinavyofanywa kwenye maabara ya taasisi hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii.
Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA) wakiwa kwenye mkutano wa kamati hiyo ya bunge.
(PICHA ZOTE NA HAMZA TEMBA - WMU)

Comments