- Get link
- Other Apps
Featured Post
KUKAMATWA MENO 50 YA TEMBO + ZIARA YA MAGUFULI MALIASILI = KUTUMBULIWA KWA DCI DIWANI ATHUMANI MSUYA
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
JUMAMOSI, Oktoba 29, 2016, Dk. John Magufuli alitimiza
miaka 57 ya kuzaliwa kwake, lakini badala ya kukaa nyumbani kula keki, Rais
huyo wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya mambo makubwa
mawili yaliyoacha simulizi.
Kwanza alizuru ghafla katika Wizara ya Maliasili na Utalii
katika kilichoelezwa kwamba alikuwa anafuatilia utekelezaji wa operesheni ya
kukabiliana na ujangilii inayofanywa na Kikosi Kazi cha wizara hiyo.
Lakini pili, mara baada ya ziara hiyo,
ikatolewa taarifa ya kutenguliwa kwa uteuzi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa
ya Jinai – DCI, Kamishna wa Polisi Diwani Athumani Msuya, aliyeishikilia nafasi
hiyo kwa muda wa mwaka mmoja, miezi mitano na siku 26 tangu alipoteuliwa Mei 3,
2015.
CP Diwani Athumani Msuya aliteuliwa Rais Jakaya
Mrisho Kikwete (sasa mstaafu) kushika nafasi hiyo iliyoachwa wazi na CP Robert
Manumba aliyestaafu kwa mujibu wa sheria.
Kabla ya uteuzi huo CP Diwani alikuwa Kaimu
Kamishna wa Kamisheni ya Intelijensia ya Jinai, ambayo wakati huo ilijazwa na Naibu
Kamishna wa Polisi (DCP) Valentino Mlowola (sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa - Takukuru).
Siyo jambo la ajabu hata kidogo katika
serikali hii kuamka asubuhi na kusikia watu wawili ama watatu ‘wametumbuliwa’
kwa siku moja, hasa kutokana na utendaji kazi wa Rais Magufuli, ambaye
inaonekana wazi kwamba, ule utaratibu wa zamani wa ‘kuleana’ wakati makosa
yanapofanyika, au kusubiri kuundwa kwa ‘tume’ zisizokuwa na matokeo halisi,
umekuwa ukimkera na ndiyo maana ameamua kuchukua hatua mara anaporidhika kwamba
ofisa amekiuka viapo vya utumishi wa umma.
Hakuna sababu zilizotolewa, na hakuna
ulazima wa kuhoji, lakini daima jibu la hesabu linaweza kuwa sahihi kwa kadiri
mtu anavyoitafsiri hesabu yenyewe. 1 + 1 =
2, lakini yaweza pia kuwa 11. Hivyo basi, kutenguliwa kwa uteuzi wa DCI Diwani
Athumani kuna kila dalili kwamba kunaendana na kukamatwa kwa meno ya tembo 50,
tukio lililotokea Oktoba 30, 2016, yaani siku moja kabla ya Rais Magufuli
kufanya ziara ya kushtukiza Maliasili.
Kikosi Kazi
cha Idara ya Wanyamapori kina wajibu wa kukamata wahusika, lakini ni Jeshi la
Polisi ndilo lenye mamlaka kwa mujibu wa sheria kuandaa mashtaka dhidi ya
wahusika, kazi ambayo inafanywa chini ya Idara ya DCI.
Vyanzo vya
habari kutoka ndani ya Jeshi la Polisi pamoja na Idara ya Wanyapori, vinaeleza
kwamba uhusiano wa matukio hayo ni mkubwa hasa kutokana na ukweli kwamba kesi
nyingi za ujangili nchini zimekuwa zikizimika ama wakati mwingine baadhi ya
wahusika wakiangaliwa bila kuguswa kwa sababu ambazo hazijulikani.
Wanasema, iwe ni kwa kuwajibishwa kwa kushindwa kuwajibika au la, lakini kuna dalili ambazo zinaonyesha uhusiano wa 'kutumbuliwa' kwa CP Diwani.
Wanasema, iwe ni kwa kuwajibishwa kwa kushindwa kuwajibika au la, lakini kuna dalili ambazo zinaonyesha uhusiano wa 'kutumbuliwa' kwa CP Diwani.
Na hii
inajidhihirisha baada ya kukamatwa kwa wahusika wa meno hayo ya tembo pamoja na
tukio jingine lililotokea siku tatu baadaye baada ya Kikosi Kazi cha Idara ya
Wanyamapori, ambacho kinawahusisha maofisa kutoka idara mbalimbali za serikali,
kukamata jumla ya bunduki 11 nyumbani kwa mbbunge mmoja wa Chama cha Mapinduzi
ambazo inadhaniwa kwamba zimekuwa zikitumika katika vitendo vya ujangili.
Wakati alipozuru Maliasili, Dk. Magufuli alionyeshwa magari
yaliyokamatwa yakiwa yamebeba pembe hizo na watuhumiwa nane wanaodaiwa
kujihusisha na mtandao wa biashara haramu ya pembe za ndovu.
Na kwa dhati kabisa, akawapongeza askari wote waliopo katika
Kikosi Kazi cha kudhibiti na kupambana na biashara haramu ya pembe za ndovu
pamoja na raia wema wote wanaotoa ushirikiano katika operesheni hiyo na akawahakikishia
kuwa anatambua kazi kubwa wanayoifanya na anawaunga mkono.
“Nawapongeza sana kwa kazi nzuri mnayoifanya na
ninawahakikishia kuwa ninawaunga mkono, chapeni kazi, wakamateni wote
wanaojihusisha na biashara hii haramu, hakuna wa kumbakiza, awe mkubwa au nani,
kamateni, wala msijali cheo chake, umri wake, dini yake, kabila lake, umaarufu
wake, sheria ni msumeno, watafuteni wote mpaka watu wakiona tembo wawe wanakimbia
wenyewe ili tuokoe wanyama wetu ambao wanaendelea kutekelezwa.
“Hapa mmekamata pembe 50 maana yake tembo 25 wameuawa,
haiwezekani maliasili yetu ikawa inapotea hovyo hovyo kwa sababu ya watu
wachache wenye tamaa ya kutaka utajiri wa haraka haraka,” akasisitiza Rais Magufuli.
Huu ndio mtazamo wangu.
Comments
duh ! stori nzuri lakini edit hyo tarehe juu kabisa mbona tarehe 29 Novemba 2016 bado,na rais alizaliwa oktoba 29 siyo Novemba
ReplyDelete