Featured Post

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO AKABIDHIWA RIPOTI YA UKAGUZI WA MANUNUZI YA UMMA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2015/2016

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akikabidhiwa Ripoti ya ukaguzi kwenye Manunuzi ya Umma kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Balozi DKT. Matern Lumbanga. Makabidhiano yaliyofanyika Wizarani jijini Dar es Salaam, Septemba 30, 2016.
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango baada ya kupokea Ripoti ya Ukaguzi wa Manunuzi ya Umma kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Waziri Mpango aliwataka kufanya kazi kwa bidii ili kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025 kwa kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Balozi DKT. Matern Lumbanga (kushoto kwa waziri wa Fedha na Mipango aliyekaa katikati), akifafanua jambo kabla ya kukabidhi Ripoti ya ukaguzi kwenye Manunuzi ya Umma kwa mwaka wa Fedha 2015/2016.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Balozi DKT. Matern Lumbanga (kushoto), akifafanua jambo kabla ya kukabidhi Ripoti ya ukaguzi kwenye Manunuzi ya Umma kwa mwaka wa Fedha 2015/2016. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA-Dkt. Laurent Shirima.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akizungumza baada ya akukabidhiwa nakala za  Ripoti ya ukaguzi kwenye Manunuzi ya Umma kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Balozi DKT. Matern Lumbanga (Kulia). Makabidhiano yamefanyika Wizarani Jijini Dar es Salaam, Septemba 30, 2016.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Balozi DKT. Matern Lumbanga (kushoto), akitoa taarifa aya ripoti hiyo mbele ya waandishi wa Habari (Hawapo Pichani) kwenye makao Makuu ya Mamlaka hayo, Jijini Dar es salaam, Septemba 30, 2016. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Dkt. Laurent Shirima na kushoto kwake ni Wajumbe wa Bodi hiyo Dkt. Leonard Chamriho ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Uchukuzi) na Dkt. Edmund Mndolwa.
(Picha zote na Wizara ya Fedha na Mipango)

Comments