Featured Post

KOROSHO KUUZWA SHS1,300 KWA KILO MSIMU UJAO

By Muyonga Jumanne, Mwananchi
Dar es Salaam. Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imetangaza mwongozo wa bei dira msimu mpya wa korosho wa mwaka 2016/17 kuwa ni Sh1,300 kwa kilo moja daraja la kwanza na Sh1,040 kwa daraja la pili.
Msimu huo unatarajiwa kuanza Septemba Moja kwa kuwa Tanzania ni nchi pekee inayoanza kuvuna korosho tofauti na nchi nyingine duniani.
Mwenyeketi wa wakurugenzi wa bodi hiyo, Mudhihir Mudhihir amesema bei hizo siyo bei halisi bali halisi itapatikana kwenye mnada.
Aliwataka wanunuzi wa korosho kukata leseni kuepuka changamoto zinazojitokeza.

CHANZO: MWANANCHI

Comments