Featured Post

KAMPUNI YA MABIBO YAWAANDALIA BONANZA WASHIRIKI MISS KINONDONI 2016 ILI KUWAWEKA FITI

 Wanyange wa Lete Raha Miss Kinondoni 2016 wakionesha moja ya shoo katika Bonanza walioandaliwa na Mdhamini wao Mkuu Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd lililofanyika ufukwe wa Jangwani Sea Breeze Mbezi jijini Dar es Salaam jana lenye lengo la kuwaweka fiti kabla ya shindano lao litakalofanyikaa Septemba mbili Hoteli ya Denfrances Sinza jijini Dar es Salaam.
 Wanyange hao wakiwa na waandaaji wa shindano hilo litakalofanyika Septemba 2, 2016 Hoteli ya Denfrances iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.
 Warembo hao wakiwa wameshika chupa za Windhoek kinywaji kinachosambazwa na kuuzwa Mdhamini wao Mkuu Kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd.
 Wanyange hao wakitosti kinywaji hicho
 Mratibu wa Shindano hilo, Rahmat George ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Rahmat Entertainment iliyoandaa shindano hilo, akizungumza na wanahabari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya shindano hilo.
 Mwakilishi wa Kampuni ya Mabibo, Abdallah Ngoma, akizungumzia udhamini shindano hilo na shabaha ya kuandaa bonanza hilo.
 Mshauri wa shindano hilo, Boy George, akizungumza na wanahabari.
 Burudani zikiendelea katika bonanza hilo.
 Wanyange hao wakishiriki kucheza mpira wa mkono kwenye bonanza hilo.
 Wadau wa Windhoek wakicheza soka la ufukweni katika 
bonanza hilo.
 Soka la ufukweni likiendelea.

Mchezo wa kuogelea ukiendelea ndani ya kiota cha Jangwani  Sea Breeze huko Mbezi jijini Dar es Salaam.

Na Dotto Mwaibale

MDHAMINI Mkuu wa Lete Raha Miss Kinondoni 2016 Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd imewaandalia Bonanza wanyange wa shindano hilo ili kuwaweka fiti kuelekea shindano lenyewe litakalofanyika Septemba 2 Ukumbi wa Denfrances uliopo Sinza.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwakilishi wa 
Kampuni hiyo, Abdallah Ngoma alisema wameamua
kuwa andalia bonaza hilo ili kuwafanya wawe fiti kabla
ya kuingia kwenye shindano lenyewe Sptemba 2.

" Katika bonaza hilo warembo hao wameweza kushiriki
mpira wa miguu, mikono na  kucheza" alisema Ngoma.

Mratibu wa shindano hilo Rahmat George alisema maandalizi
 yote yamekwisha kamilika ambapo warembo 20 watapanda
jukwaani kuwania nafasi ya Miss Kinondoni 2016.

Alisema kama kawaida warembo hao watapanda jukwaani 
wakiwa katika vazi la ufukweni, ubunifu na kujibu maswali wata
kayoulizwa na majaji.

George ametumia nafasi hiyo kuwaomba wadau wa 
mashindano hayo kufika kupata burudani safi itakayotolewa na mwanamuziki 
nguri Christian Bela na kikosi cha promosheni cha kampuni ya
Mabibo.

Comments