Featured Post

WAZAZI WATAKIWA KUWA MAKINI NA MARAFIKI WA WATOTO WAO

Mkurugenzi wa Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone, Usia Nkhoma Ledama (kushoto) akizungumza na mmoja wa wazazi Bw. Ally Msoya alipowasili kwenye mahafali ya nne ya shule hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Tower jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Modewjiblog)

Kutokana na baadhi ya watoto kuwa na tabia ambazo hazipendezi watu bila ya kufahamu chanzo chake, imeelezwa kuwa ni vyema wazazi wakajenga mazoea ya kuwafahamu watu ambao wanakuwa karibu na watoto wao ili kuchukua hatua mapema.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone, Usia Nkhoma Ledama wakati wa mahali ya nne ya shule hiyo ambapo watoto wa ngazi mbalimbali za madarasa walihitimu.

Usia alisema kuwa wazazi wengi wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kujishughulisha na kazi zao bila kuwa na muda wa kukutana na watoto wao na hivyo kuwa ngumu kutambua chanzo cha tabia ambazo zinaibuka kwa watoto wao kutokana na wao kutowafatilia watu ambao wanakuwa karibu na watoto.

"Tunafahamu wazazi wengi mnakuwa busy na kazi zao na hivyo mtoto akitoka shule anakuwa na dada au kuangalia tv lakini akiwa katika michezo na watoto wenzake mnakuwa hamjui ni vitu vya aina gani wanafanya,

"Nadhani ni vyema sasa kuhakikisha mnawafahamu marafiki wa watoto wenu, marafiki zao wa shuleni na marafiki zao wa nyumbani, huwezi kujua wanafanya nini kama huwafahamu tabia watoto wanaocheza nao lakini kama ukiwajua unakuwa unafahamu rafiki anayefaa ni yupi," alisema Usia.

Aidha aliwatoa hofu wazazi kuwa shuleni hapo wanawafundisha watoto tabia njema na wanawafahamu vyema wanafunzi wao hivyo kazi kubakia kwa wazazi kuhakikisha wanakuwa makini na watoto wanapokuwa nyumbani.

Kwa upande wa mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Eda Sanga aliwapongeza wanafunzi ambao wamehitimu masomo na wazazi kwa moyo wao wa kujitoa kuwasomesha watoto wao lakini pia kuwataka kuwasimamia vyema watoto wao ili waweze kufika mbali kielimu.

"Elimu ni muhimu sana kwa watoto wenu wanatakiwa kusoma ili kufika mbali kimaisha niwasihi kuwasimia vyema watoto ili wanapokuwa shuleni wafanye vizuri na wanaporudi nyumbani pia wafanye vizuri," alisema Eda.
Watoto ya O'Jays Kiddies Zone wakitoa burudani kwa wazazi kwenye mahafali ya nne ya shule hiyo.
Mhitimu wa darasa la Laurey, Thomas Mboya akiongoza watoto wenzake kwenye burudani maalum wakati wa mahafali ya nne ya shule hiyo.
 
Mwanafunzi wa Lilies Class, Iptihaj Kinyaga akiongoza darasa la wanafunzi wenzake kutoa burudani kwa wazazi kwenye mahafali hayo.
Wahitimu wa Laurel Class wakitoa burudani ya kuagana na wanafunzi wenzao katika mahafali ya nne ya shule hiyo.
Pichani juu na chini ni sehemu ya wazazi waliohudhuria mahafali hayo.
Bwana na Bibi Lugoe wazazi wa mhitimu Abigail Lugoe wakiwa meza kuu.
Wazazi wa Watoto ya O'Jays Kiddies Zone wakitazama burudani na vipaji mbalimbali vilivyokuzwa shuleni hapo kutoka kwa watoto wao.
  
Lantana Class wakitoa burudani kwenye mahafali ya kaka na dada zao
Mkurugenzi wa Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone, Usia Nkhoma Ledama akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mama Eda Sanga kutoa risala kwenye mahafali ya nne ya shule hiyo yaliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Msasani Towers jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Eda Sanga akitoa nasaha kwa wazazi na walezi waliohudhuria mahafali ya nne ya darasa la Laurel Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone yaliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Towers jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wazazi na walezi wakisikiliza nasaha za mgeni rasmi.
Wazazi maalum wa mtoto Abigail Lugoe, Bwana na Bibi Lugoe wakitoa shuhuda ya malezi bora na elimu aliyoipata mtoto wao ambaye mwakani atajiunga na darasa la kwanza. Kushoto ni Mkurugenzi wa Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone, Usia Nkhoma Ledama.
Wazazi wakiendelea kushuhudia matukio mbalimbali yaliyojiri kwenye mahafali hayo.
Bw. Ally Msoya na familia yake.
Kutoka kushoto ni Victoria Martin, Thuwein Makamba na Husni Seif, LTE Specialist wa Tigo Tanzania katika mahafali shule ya Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone.
 
Dada Faiza Ally akibadilishana mawazo na mmoja wa wazazi katika mahafali ya shule hiyo.
Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Eda Sanga akimtunuku cheti, Joylyn Marandu mhitimu wa Laurel Class katika mahafali ya nne ya shule hiyo.
Wahitimu wakiendelea kutunikiwa vyeti.
Mhitimu Patrick Kasanga akipokea cheti chake. (Picha zaidi ingia hapa)

Comments