- Get link
- X
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- X
- Other Apps
MKURUGENZI
Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Geofrey Mwambe, amewataka Wakuu wa
Wilaya na Mikoa nchini, kuacha mara moja kutoa adhabu, matamko mbalimbali kwa
wawekezaji waliopo nchini bali waziachie mamlaka husika kufanya kazi hiyo.
Mwambe
aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipokuwa akielezea mafanikio ya ziara yao ya
kutafuta wawekezaji, waliyoifanya katika nchi za Korea na China, mwezi huu.
''Utakuta
DC au RC anaenda kwenye ziara sehemu, anaanza kutoa maagizo ya kukamatwa
mwekezaji au alipe kodi kiasi fulani,
hiyo siyo kazi yao, kuna mamlaka husika ambazo zinatakiwa kufanya kazi
hiyo,” alisema.
Aliwataka
viongozi hao kufuata sheria na kanuni kwani wao hawahusiki na mwekezaji au
mfanyabiashara ambaye halipi kodi bali hiyo ni kazi ya Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA).
“Wajibu wa
viongozi ni kutoa taarifa kwa mamlaka husika juu ya wawekezaji wasiolipa kodi, wanataarifa kuna mtu halipi kodi, wanatakiwa
kupeleka taarifa hiyo ofisi husika na siyo kutoa matamko na vitisho.
Mkurugenzi
huyo alisema, kuna viongozi wengine wanadiriki kutoa amri kiwanda fulani
kifungwe au wanatoa siku kadhaa kiwe kimelipa kodi wakati hiyo si kazi yao.
“Kama
mwekezaji ana tatizo wanatakiwa kutoa taarifa TIC au kwa mamlaka husika iliwe
kufuatilia, kodi inakusanywa na TRA,
viongozi, tuache kila taasisi ifanye kazi yake.
“Tusiingilie
majukumu ya watu wengine, kila mmoja ana lengo la kumsaidia Raisi Dkt. John
Magufuli, lakini tunatakiwa kufuata utaratibu,” alisisitiza.
Alitoa
wito kwa viongozi wenzake, kufuata sheria na taratibu na washirikiane kukuza uchumi kwani Rais Dkt. Magufuli
anatamani kuona Tanzania ifikapo 2025 inakuwa katika uchumi wa kati.
Katika
hatua nyingine, alisema anatarakjia kumuandikia barua Kamishna Mkuu wa TRA, kwani
kuna wawekezaji wamekaa miaka 7 nchini bila kulipishwa kodi badala yake
wanakuja wageni wanadaiwa walipe kodi.
“Hii siyo
sawa, wawekezaji hao wamekaa miaka 7 nchini, hakuna mtu wa forodha aliyeenda kudai
kodi, wameondoka wamekuja wapya, wanadaiwa kodi
ya miaka saba ilioyopita,” alisema.
Comments
Post a Comment