- Get link
- X
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- X
- Other Apps
NA MWANDISHI WETU, KONDOA
MICHORO ya kale
iliyopo katika hifadhi ya Kolo wilayani Kondoa, Mkoa wa Dodoma, ipo
hatarini kufutika kutokana na matumizi
mabaya yanayotumika kwenye mila za matambiko yaliyopo katika mapango hayo.
Mkuu wa Kituo cha Michoro ya Miambani cha Kolo, Zuberi Mabie,
alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na
watumishi wa wizara ya Maliasili na Utalii walipotembelea kwenye michoro hiyo ya watu wa kale iliyopo Kolo wilayani
humo .
"Baadhi ya jamii wanaofanya matambiko hayo ya kimila
kukosa elimu juu ya umuhimu wa michoro hiyo ya kale iliyopo kwenye hifadhi hiyo
inayotambulika karibu duniani kote," alisema.
Akibainisha mkuu huyo wa kituo alitaja matumizi hayo ni
pamoja na baadhi ya jamii wanaonde kutambika wamekuwa wakifanya uchafunzi wa
mazingira kwakumwaga pombe za kienyeji kwenye kuta za michoro hiyo ya kale
wanazo endanazo.
“Baadhi ya jamii wamekuwa walifanya matambiko na wamekuwa
wakija na pombe za kienyeji, na matambiko yao wamekuwa wakimwanga pombe hizo
kwenye michoro na kusababisha kuacha
alama za pombe, vitendo hivi vinaweza kusababisha michoro hiyo kufuatia," alisema
Zuberi.
Vile vile alisema, ukataji miti hovyo katika Hifadhi ya
Michoro hiyo, maji ya mvua, uchungaji wa mifugo, vumbi na jua, inasababisha
uharibifu wa michoro hiyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa
Rasilimali watu Lusius Mwenda, aliwataka Watanzania kutumia hifadhi hiyo ya Kolo
kwa manufaa ya kuiletea taifa uchumi kutokana na michoro ambayo imekuwa kivutia
kwa ajili ya utalii wa ndani.
Mweda alisema michoro hiyo iliyopo ambayo inasadikiwa
kuchorwa na jamii ya kabila la Wasandawe na Warangi, imekuwa kivutio ambacho
kwa watu wengine wanaweza kujifunza na kufahamu historia ya babu zetu hao wa
kale.
Hata hivyo, alisema kuwa kutokana na kuimarika kwa barabara
ya kutoka Dodoma hadi Babati hifadhi hiyo imekuwa na ongezeko la watu
wanaotembelea kutoka 200 waliokuwa wakifika kwa kipindi mwezi mmoja huko nyuma
hadi kufikai 400 kwa hivi sasa.

Comments
Post a Comment