- Get link
- X
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- X
- Other Apps
NA
MWANDISHI WETU,
IRINGA
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa
Iringa, imemkuta na kesi ya kujibu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mtandao wa Wanafunzi
Tanzania (TSNP), Abdul Omary Nondo.
Akisoma hukumu ndogo jana, Hakimu
Mkazi Mfawidhi Liad Chamshama, alisema baada ya kupitia maelezo ya pande zote,
mahakama imemuona Nondo anakesi ya kujibu kulingana na kielelezo namba sita.
Kielelezo hicho ni nyaraka kutoka
Jeshi la Polisi aliyoandikishwa Nondo Mjini Mafinga akidai ametekwa na watu
wasiojulikana, kuachiwa karibu na Kiwanda cha Pareto (PCT) kilichopo Mjini
Mafinga.
Chamshama alisema, Nondo alitoa taarifa
za uongo mbele ya shahidi namba moja ambaye ni Ofisa wa Jeshi la Polisi au Serikali
mwenye namba E.2328, Coplo Salum wa Kituo cha Polisi Mafinga.
Alisema mshtakiwa ana kesi ya
kujibu kwa mujibu wa kifungu namba 231 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai
ambapo mshtakiwa anayo haki ya kujitetea.
Kesi hiyo iliyotolewa hukumu
ndogo kwa muda wa dakika 13, ambapo Nondo aliongozana na Wakili msomi, Chance
Luwoga ambaye alisema mteja wake atajitetea.
Machi 21, mwaka huu mshtakiwa hiyo
alifikishwa katika mahakama hiyo kwa kosa la jinai namba 13 ya mwaka 2018 akidaiwa
kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya kompyuta akitumia simu ya mkononi
kinyume na sharia ya makosa ya mtandao namba 16 ya mwaka 2016 na kusambaza
taarifa hiyo kwa njia ya Whatsapp.
Machi 7, mwaka huu, mshtakiwa
akiwa katika eneo la Ubungo, Dar es Salaam alidaiwa kusambaza ujumbe kwa kwa
njia ya mtandao wa Whatsapp akitumia simu namba 0659-366125 uliosomeka (Im at
risk) akibainisha yupo hatarini, baadaye
taarifa hiyo ilisambaa kuwa ametekwa na watu wasiojulikana hali iliyoleta
hamaki katika jamii.

Comments
Post a Comment