- Get link
- X
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- X
- Other Apps
NA ALOYCE NDELEIO
Jamii kuhabarishwa kuhusu kilimo ni jambo la msingi katika kupata maendeleo yanayohitajika katika
sekta hiyo inayotegemewa kwa ajili ya
chakula pamoja na malighafi inayotumika
viwandani.
Lakini ni dhahiri kuwa vyombo vya habari mara nyingine
vimekuwa vinajikita kwenye masuala
yanayohusu kilimo na ukweli unabakia kuwa
waandishi wa habari wana jukumu gumu la kuwa kiunganishi katika
jamii za mijini na vijijini.
Uhaba wa chakula, mabadiliko ya hali ya hewa, utandawazi,
bioteknolojia, utabiri kuhusu kupungua kwa kiwango cha maji ni baadhi ya mada
nyingi ambazo moja kwa moja zinabeba
maisha ya kila mtu iwe mijini au
vijijini.
Miongoni mwa nchi nyingi zinazoendelea kilimo kimekuwa mioyoni mwa mada hizo lakini
ili kuelewa kwa uwazi ni namna gani maisha yalivyo katika ulimwengu wa vijijini
ni muhimu kuboresha maisha ya jamii
katika maeneo hayo.
Wawekezaji, wafanya biashara, wapanga sera, wote wale ambao makazi ya ni mjini wamekuwa
wakijihusisha na mahitaji ya wakulima kuhabarishwa.
Hata hivyo uhabarishwaji
kuhusu sekta hii muhimu umebakia kuwa hautoshi, mara nyingine kuwa ni
uhabarishaji wa nusunusu usiokamilika na
mara nyingine kutounganishwa na sekta yenyewe.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Mfuko wa Kimataifa wa Habari wa Wanawake (IWMF)
ulibainisha kuwepo kwa tofauti kubwa kati ya umuhimu wa kilimo katika uchumi
miongoni mwa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara.
Kilimo katika eneo hilo kinachangia asilimia 34 ya pato la
ndani kwa nchi, asilimia 40 ya mauzo ya nje na asilimia 70 ya ajira lakini kwa kulinganisha na nafasi
inayopata katika vyombo vya habari ni kwamba inakejeliwa.
Katika nchi za Mali, Uganda
na Zambia vyombo vya habari
vilijikita katika kuhabarisha kuhusu kilimo kwa kiwango cha asilimia 4.0 ya
kurasa au muda wa kurushwa kipindi.
Hata hivyo kilichojitokeza ni kwamba mchango unatolewa na wanawake katika sekta ya kilimo ilikuwa ni
nadra kupewa nafasi au kutolewa katika vyombo hivyo.
Asilimia 70 ya matukio kwenye redio, televisheni na magazeti yaliyo mengi yalijikita kwenye mada
zake kwa kuandika mada ambazo zilitokana
na mazungumzo na wataalamu.
Aidha vyombo hiyo ilibainika kuwa viliripoti hotuba zilizotolewa ambapo asilimia 20 ya mada
zilitokana na kuonana na kuhojiana na wakulima na wakazi wa vijijini ambao wana
uzoefu wa moja kwa moja wa masuala hali halisi ya kilimo.
Mada nyingi zilizoandikwa
na kutanganzwa kuhusu kilimo zilionekana kuwa zinaegemea upande mmoja tu
na kuusahau uapnde wa pili.
Kwa mfano baadhi ya
mada zilikuwa zinahusu 'Wakati rais
ametembelea au kama mtu amefariki kutokana na kukosa chakula au tukio la
kutolewa misaada kwa ajili ya wahanga wa njaa.”
Mbali na matukio hayo ambayo
yaliwalazimisha wahariri wa
vyombo vya habari wawapeleke waandishi
wao kwenye matukio hayo ni mara chahche waaandishi wamekuwa wakitoka mijini.
Aidha ilibainishwa kuwa kuandika kuhusu sherehe za
kufunguliwa na kufungwa kwa semina ambako wanakuwa wamealikwa na kulipwa kuliripotiwa kwa kiwango kikubwa.
Katika mazingira ya aina
hivyo utafiti huo unadai kuwa waandishi kwa kiwango fulani walikuwa ni
maofisa uhusiano ambao walitakiwa kuhabarisha kuhusu mambo ambayo yameshafanywa
na mamlaka husika, asasi zisizo za
serikali na vyama au mashirika ya kimataifa.
Ukweli na takwimu zilizohusishwa zilitoka upande mmoja ambao ulikuwa macho kulinda
taswira yake.
Uandishi wa kweli
unajumuisha uchambuzi wa takwimu zilizotolewa
na kulinganisha na hali halisi katika mshamba ikiwa ni njia halisi
ya kuhakikisha na kuona kama miradi au
ubunifu ni kweli unafanikiwa na ni
sahihi kwa maendeleo ya kilimo ya nchi.
Mchango mwingine wa waandishi ni kukusanya habari kutoka
maeneo ya vijijini na hivyo kuziunganisha na wapanga sera na wanajamii wengine
jambo ambalo limekuwa halitokei.
Kutokana na kukosekana kwa vyanzo, mashirika ya habari ni
mara chache hupeleka waandishi wake vijijini. Usafiri na malazi huwa ni wa gharama kwa ajili ya kutafuta
mada ambayo kipaumbele chake ni cha
chini kwenye vyumba vya habari.
Matokeo yake waandishi huishia kutegemea mashirika ambayo yanaweza kuwalipia gharama za usafiri
na hivyo kuwa mateka wa wadhamini wao ambao huwaonesha ni kitu gani wanataka waaandike.
Maendeleo vijijini
yamekuwa yanapewa kipaumbele kidogo katika vyombo vya habari. Wahariri wengi wa habari
wanayachukulia masuala haya kama yana
mvuto kidogo kwa wasomaji na hivyo katika kuzipangia kurasa huziweka kwenye
kurasa za ndani.
Hata hivyo ni mara chache pia zimekuwepo chambuzi au vipindi
vilivyojikita kwenye kilimo. Mara nyingi suala la kilimo limekuwa
likishughulikiwa na kurasa zinazohusika na masuala ya fedha au biashara katika magazeti ya kila siku.
Inabainishwa kuwa
hata katika mitandao ya intaneti
ambayo inachapisha habari kutoka nchi mbalimbali imebainika ni mara
chache kumekuwepo kichwa kinachohusu
'kilimo' ambacho kinahusisha 'chakula, kilimo na masuala ya vijijini’.
Hali kadhalika ilibainishw akuwa ni waandishi wachache
waliojikita katika kilimo na mara nyingi huwa ni wachache katika vyombo vya
habari.
Hata hivyo wale wanaoshughulisha na habari za kilimo
wanakabiliwa na ugumu katika kutoa maelezo yaliyo wazi kwa wasomaji wake au
wasikilizaji hususan katika masuala magumu
kama vile mabadiliko ya hali ya hewa, bioteknolojia au katika kuwahoji
watafiti na wataalamu kuhusu masuala yanayohusu kilimo.
Hawa huishia kutumia
misamiati migumu ya kisayansi na ni
mara chache hufanya juhudi za kujieleza
wenyewe katika lugha ambayo inaweza kuwa rahisi kueleweka kwa wanaowahoji.
Kinadharia ni kwamba waandishi wanaweza kupata habari
kupitia mtandao wa intaneti lakini
wanatakiwa kuwa na fursa inayowawezesha
kufikia na kufahamu jinsi ya
kutafuta na kuchambua matokeo yao kufuatana
na kiwango kikubwa cha takwimu kinachokuwepo.
Tatizo kwa kiasi fulani huonesha kukosekana kwa vifaa vya
mafunzo kwa ajili ya uandishi wa habari za kilimo ikiwa ni pamoja na
kukusanya na kutawanya aina za habari
zinazotakiwa
Tatizo hilo husababisha kukosekana kwa uzoefu na
aina mbalimbali za stadi, ueledi wa kilimo, uchumi, lishe na mazingira yanatakiwa kueleweka kwa
waandishi wanaotaka kuelewa masuala ya
kilimo.
Tofauti na sekta nyingine kama vile afya ya binadamu, hakuna kabisa
programu ya uandishi wa habari za kilimo miongoni mwa baadhi ya nchi zinazoendelea, ambayo matokeo yake ni
kwamba kubobea kunafanywa kutokana na uendelevu wa kuifanya kazi.
Waandishi wanaalikwa kwenye semina kuhusu masuala ambayo ni magumu na hushindwa kutumia faida ya fursa hiyo kutokana na kutokuwa
na mwanzo mzuri wa masuala ya sayansi au ufundi.
Lakini ufumbuzi wa hali kama hiyo unaweza kufanywa na
taasisi kupitia semina mahsusi kwa vyombo vya habari ambazo mara nyingi hubebwa
na wahariri wa vyombo na ambao huw ana nafasi ndogo kujipa kazi ya kushughulikia masuala ya
kilimo.
Hata hivyo tasisi zinaweza kuwa na vyombo vyake ya kujikita
kwa kina katika kilimo kama ambavyo ilikuwa kwa Wizara ya Kilimo Tanzania ikiwa
na gazeti la Mkulima wa Kisasa, kama bado lipo hakuna anayejua.
Kadhalika vilikuwepo vipindi vya redio na mojawapo kikiwa na jina hilo pia
kikirushwa na Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa ni Shirika la
Utangazaji Tanzania (TBC).
Hata hivyo mchango wa vyombo vya habari ni muhimu katika
kuikuza sekta hiyo ikiwepo mikakati inayoviwezesha kufanya hivyo n kinachogomb
hapo ni kujumuishwa katika hatua mbalimbali zinazoihusu.

Comments
Post a Comment