- Get link
- X
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- X
- Other Apps
NA
CONGES MRAMBA, MWANZA
CHAMA
Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Mwanza (Nyanza Co-operative Union), kitakuwa
mwenyeji wa Maadhimisho ya Siku ya
Ushirika Duniani.
Habari
za kuaminika kutoka ndani ya Chama hiki ambazo Tanzanite imeambiwa jana
zinasema, Menejimenti ya Nyanza sasa inafanya maandalizi kuhakikisha maadhimisho haya yanafana; na yatashirikisha
vyama vyote vya ushirika hapa nchini.
Kwa
mujibu wa viongozi wa chama hicho, ambao hawakutaka kutajwa majina, maadhimisho
hayo yatafanyika katika viwanja vya CCM Kirumba jijini hapa mwanzoni mwa Julai
mwaka huu, ambapo mgeni rasmi anatazamiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Maadhimisho
hayo yatafika kilele Julai 7 hapo kwenye viwanja vya CCM Kirumba.
“Hii
hapa ni Menejimenti ya Nyanza, na hapa tunafanya maandalizi ya maadhimisho
haya, na tunaishukuru serikali kutuamini ili kuwa wenyeji wa Siku ya Ushirika
Duniani,” mmoja wa wajumbe wa Menejimenti hiyo ameliamia gazeti hili jana
katika ofisi za chama hicho.
Kulingana
na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Chama cha Nyanza ndicho kilichozaa
vyama vyote vya ushirika katika Kanda ya Ziwa.
“Nyanza
jamani, historia ya dunia ipo kwenye rekodi… ndiyo kilikuwa chama kikubwa cha
Ushirika cha pili hapa duniani, nyuma ya kile cha Sweden. Ndiyo Victoria
Federation, lakini ilikuja kuhujumiwa na watu ambao ajenda yao ilikuwa
ubadhirifu na kuhujumu tu!” Mkuu huyo wa mkoa alisema.
Mkuu
wa Mkoa alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuwaambia hujuma na ufisadi
uliokuwa ukifanywa dhidi ya ushirika huo, huku akisikitika chama hicho
kushindwa kufanya kazi.
Wakati
kikiwa katika ubora wake, kilikuwa kikimiliki vinu vya kuchambulia pamba (ginneries)
na mtaji wa zaidi ya shilingi bilioni 10, huku kikinunua pamba katika mikoa ya
Geita, Mwanza, Simiyu, Shinyanga na Mara.
Alisema,
wakati huo kilikuwa mhimili wa ajira katika Kanda ya Ziwa, kikinunua pamba ya
zaidi ya shilingi bilioni sita kwa mwaka.
Hata
hivyo, Serikali ya Rais John Magufuli imeamua kukisimamisha tena chama hicho,
ambapo katika msimu huu kinasimama kununua pamba mkoani humo.
Serikali
ilibadilisha Menejimenti ya Chama na kuweka mpya, kisha watuhumiwa waliojiuzia
mali za chama hicho kwa bei chee baadhi yao walikamatwa na kufunguliwa mashtaka.
Kaimu
Meneja Mkuu wa Nyanza, Juma Mokili amesema, msimu huu wa ununuzi wa zao la
pamba, wanatazamiwa kukusanya zaidi ya asilimia 50 ya malengo waliyojiwekea.
Comments
Post a Comment